leo kwenye taarifa ya habari ya channel 10, katibu mkuu kiongozi balozi seif ametangaza kwamba serikali itakifufua kiwanda cha general tyre cha arusha mapema iwezekanavyo. Tunajua kwamba mh lowasa alipoenda kutafuta wadhamini mkoani arusha alitangaza vipau mbele vyake kimoja wapo ni kukifufua kiwanda cha matairi kilichokufa kwa muda mrefu, arusha general tyre. Sasa naona serikali ya ccm imeamka na kusema kwamba watakifufua kiwanda hichi. Sasa namwomba mh lowasa aendelee kutoa vipau mbele vyake kwenye kila mkoa, serikali inamsikiliza sana na wanajua anachosema ni kweli atafanya, sasa wanaamua kuamka. Bravoo lowasa, na serikali pia kwa kumsikiliza mzee wa maamuzi