Kiwanda cha General Tyre cha Arusha kufunguliwa

Kiwanda cha General Tyre cha Arusha kufunguliwa

Kwani mmesahau kuwa moja ya sababu ya mvutano wa Lema na Lowasa Arusha mjini ni general tyre? Na mmesahau hoja ya mwakyembe kuhusu ununuzi wa ndege za atcl?
 
Hata mimi nimeshangaa sana kusikia hilo.
Bahati nzuri Lowassa alishalisema hilo.
 
It's working. CCM hawakumtaka Lowassa kwa sababu wanajua rekodi ya uchapakazi wake! Yeye sio msanii akisema kitu anamaanisha.
Hongera sirikali

Umeandika ukweli mtupu,mkuu aliona atafunikwa sana kisha aonekane alikuwa anachekacheka tu,kwahiyo ameogopa hilo. KURA YETU WATANZANIA NI KWA LOWASSA WA CHADEMA,UKAWA.
 
Katika hili wananchi tusiwe polarised, hapa ninachokiona ni the so called 'mtandao'umejam..vita ya panzi Furaha ya kunguru.
 
Tena anasisitiza...
Napenda kuwahakikishia kuwa sitawaangusha.Kisha anamalizia na Arincherema Arija.
Hivyo ndivyo vipaumbele vyake.

Hahaha kwakweli Magufuli anaweza uwaziri tu,lakini urais HAPANA AISEE.
 
CCM katika harakati za kukimbiza kivuli cha Lowassa. Mambo kama haya ndiyo yanayokuhakikishia kuwa CCM sasa wamepanick - yani wanasubiri Lowassa akizungumzia kitu nao wanajifanya kukifanyia kazi haraka ili wananchi wapotee maboya, ingekuwa rahisi sana wao kufanikiwa na mbinu hii kama tungekuwa tumepata uhuru mwaka 2010.

Ni juzi tu kwenye hotuba ya Lowassa ya kujitambulisha Arusha aliwaambia wananchi kuwa anafahamu tatizo la General tyre - leo serikali ghafla kutoka kusiko julikana inatangaza kutaka kununua hisa zote za General Tyre - ila mtu mwerevu atauliza wapi vilipo Mwatex, UFI, Tanganyika packers n.k.?unagundua kumbe ni danganya toto nyingine ya ccm..

Mara ya mwisho wakati JK akiwa na hali mbaya sana kwenye siku za mwisho za kampeni za 2010 ndio alikuwa kwenye hali ya panic namna hii akiwa na sauti inayotetemeka kabisa akisema atajenga fly overs Dar es Salaam..
 
Wanajua Arusha ni ngome yetu. Hawapati kitu hata wafungue fibre board na Unga Limited,

Kazi wanayo Mwanza ngome nyingine kuna MWATEX sijui nacho watakifungua ? Ngoma iko Kigoma hakuna hata mtaro wa maji machafu wa kufungua.
 
Usiwasikilize.... hao ni kuwapiga chini tu tarehe 25october!
 
Hatuwezi kuwa na raid zuzu..! Mwalimu aliwahi kusema kama mkubwa wako akikuambia kitu cha kijinga, nawe unajua ni cha kijinga lakini ukakifanya, wewe ni zuzu!kuna mtu fulani anadai eti alifanua kwa maagizo ya mkuu!ulaya mtu akipewa maelekezo na mkubwa ambayo ni kinyume na maadili, anajiuzulu kulinda heshima take siyo mpaka aundiwe time.
 
Lowassa atuambie ukweli kuhusu General tyre
 
Hatuwezi kuwa na rais zuzu..! Mwalimu aliwahi kusema kama mkubwa wako akikuambia kitu cha kijinga, nawe unajua ni cha kijinga lakini ukakifanya, wewe ni zuzu!kuna mtu fulani anadai eti alifanua kwa maagizo ya mkuu!ulaya mtu akipewa maelekezo na mkubwa ambayo ni kinyume na maadili, anajiuzulu kulinda heshima yake siyo mpaka aundiwe tume.
 
Mzeee wa arimsereeeeeeemaaaaaaaa
Upoooooooooooooooooo
Mzeee wa sitawadondoshaaaaaaa
 
Wengi watadhani kuwa mpango wa kufufua kiwanda cha kutengeneza matairi kilichopo jijini Arusha umeanza hivi karibuni baada ya Mh Lowasa kuzungumzia juu ya kiwanda hicho. Kama mdau nimeona nikanushe taarifa hizo.
Jitihada za serikali za kufufua kiwanda hicho zilianza siku za nyuma, zaidi ya mwaka na nusu sasa umepita.
Nikiwa ofisini, nilipokea taarifa kuwa tunatakiwa kwenda kwenye ofisi za National development corporation kuchukua nyaraka za tenda kwa ajili ya kufanya marekebisho kwenye mfumo wa umeme wa kiwanda hicho. Ila kutokana na kampuni yetu kutokuwa na uwezo wa kutoa huduma katika maeneo yote na kwa kwa kuwa kampuni yangu ilikataa mapendekezo niliyotoa ya kuingia Joint venture na kampuni moja wapo, niliachana na tenda hiyo. Mwishowe kulingana na kumbukumbu nilizo nazo, kampuni ya Urban and rural engineering ya jijini Dar Es Salaam, ndiyo ilishinda zabuni hiyo na fedha hizo zaidi ya milioni mia sita za marekebisho katika mifumo ya umeme kugharimiwa na NDC. Marekebisho hayo yalijumuisha kufunga mota mpya kadhaa zenye uwezo mbali mbali, kubadishisha nyaya za umeme n.k.

Kwa muhtasari huo napenda kuwajuza uma wa watanzania wasipotoshwe kwenye kila jambo linalohusu maendeleo ya taifa hili kwa kufanya kila kitu kisiasa....
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Back
Top Bottom