Kivuko cha MV Magogoni chaelea baada ya injini kuzima

Kivuko cha MV Magogoni chaelea baada ya injini kuzima

Nasikitika sana kwa hali iliyotokea.
Jumapili iliyopita nilitumia kivuko hiki kuvuka kuja DAR, kwanza nilistuka sana kuona moshi mzito uliokuwa inautoa, na nilipoangalia kenye sehemu za maboya ya abiria niligundua kwamba zaidi ya nusu ya maboya hayapo (chanja zote mbili) na inaonesha yalikuwa yamepunguzwa kwa makusudi ama kuibiwa.

Pia uholela wa kuruuhusu abiria wengi kusongamana eneo la magari ni uzembe mkubwa wa wasimamizi ambapo kule chini hakuna maboya na hata kuyafikia yale ya juu ni mziki mzito.

Nilishajiapia kutopanda tena pantooni tangia siku hiyo kwa sababu ya uzembe wa makusudi wa pande zinazohusika na usalama na usimamizi wa kivuko kile.

Naamini hakuna atakayepata madhara labda mali zipotee au kuibwa na wajanja. Ila tangu MV Bukoba hadi leo Watanzania hatujifunzi lolote na tunazidi kuishi maisha ya roho mkononi kama wazoefu wa majanga
 
Mungu ni mkubwa mtakuwa salama. Hiki kivuko kama mwezi mmoja uliopita nilipanda nikitoka kigamboni injini moja ilikuwa inatoa moshi wa kufa mtu. Kesho yake tena nikavuka nacho kikiwa kinatumia engine moja na ile nyingine ikawa anatengenezwa.. du kweli Dar ni tambarare...
 
Asiyejuwa kuogelea hapo ndiyo shida lakini kwa wapiga mbizi hapo hakatwi mtu.
 
hicho kivuko kimeshakuwa chakavu sana serikari aina budi itafute kivuko kipya ili kuondoa shida ya usafiri kwa wakazi wa kigamboni!!
 
Haya sasa changanya na hii ya hp A town ya Ndege. Sijui tutapata nini.

Mwenyenzi MUNGU tusaidie watu wako.
 
Haikuwa hatari kihivyo.. Abiria walikuwa watulivu na walipata ushirikiano wa kutosha toka kwa vyombo vya usalama majini.. Hata hivyo kivuko kile kinahitaji matengenezo makubwa.. Na vile vile maboya yanatakiwa ya kutosha ndani ya kivuko.. Ashukuriwe Muumba wa mbingu na ardhi..
 
Kishawekwa pembeni watu wameshushwa ma matechnician wamevaa diving suit na gesi mgongoni wanazama chini yake
 
Back
Top Bottom