BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,331
- Thread starter
- #281
Simple. Kuna uwezekano mkubwa watu wako kwenye desperation ya kupata mabadiliko. Na anapoona mabadiliko hayatokei yupo tayari ku-compromise principles zake.
Mabadiliko unayataka yaje tena kwa haraka. Lakini hakuna wasemaji. Wabunge wameshindwa kusema. Wananchi wanajirusha kwenye mdundiko. Na kilichobakia ni wewe kukubaliana na mtu yoyote mwenye guts.
Hii sawa na mwanamke aliyesubiri mchumba au mume mwenye sifa fulani kwa muda mrefu. Lakini kutokana na mwenye sifa anazotaka kuwa in short supply anahamua kukubali mtu yoyote yule kwa mategemeo kuwa anaweza kumbadilisha baadaye. Anasahau kuwa watu wazima ni vigumu kubadilisha tabia zao.
You can put lipstick on a pig, but it's still a pig.
Zakumi kwa kifupi ni kwamba Ktine ni fisadi na Watanzania wengi tutaendelea kumuweka katika kundi la mafisadi walioweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Taifa na kutumia mianya iliyopo ili kukidhi haja yao ya kujipatia utajiri wa haraka haraka. Pamoja na hili la Kitine kuwa fisadi mimi kwa maoni yangu aliyoyasema Kitine yana ukweli mtupu na umuhimu mkubwa kutokana na hali halisi ilivyo nchini mwetu na hakuna sababu zozote za msingi za kuyapuuza aliyoyasema Kitine. Kutoyapuuza yaliyosemwa na Kitine hakubadilishi wala kuondoa ukweli kwamba Kitine ni Fisadi.