Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,492
Nadhani Jasusi amekujibu vizuri. Kwa kuongezea tu haiwezekani Mtanzania aliyeishi nje kwa muda mrefu ambaye ameshakuwa ni mchapa kazi hodari akirudi aanza tena kuzembea eti kwa kuwa yuko Bongo. Tatizo ni kama hilo alilokwambia Jasusi na wakati mwingine Bongo unatakiwa kuwa na kigod father ambacho kitajidai kinakkupigia debe kwa 'wakubwa' ili upate promotion.
Uzuri wa nje juhudi za kazi zako zinaonekana na wakubwa wala huhitaji kuwa na kigod father mambo yanajipa yenyewe na unaona unapanda tu kutokana na vyei vyako na utendaji mzuri wa kazi zako. Bongo hili hakuna bila kuwa na God Father utachapa kazi mtindo mmoja lakini juhudi zako kamwe hazitakuletea mafanikio ya kupanda cheo.
BAK BAK:
Ndio Jasusi ameeleza vizuri lakini u-kienyeji haupo kwenye kufanya kazi pekee yake. Hupo kwenye ubadhirifu wa mali za umma pia.
Chukua mfano wa Balali. Alikuwa anafanya kazi, lakini hakusahau kujiandikia cheki. Lakini sidhani kuwa angekuwa kwenye nchi ya watu, angefikiria kuvuta kisicho chake.