Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,222
- 53,037
Mkulima mmoja mzee kijijini alikuwa na mke aliyependa sana kumbugudhi bila huruma. Kuanzia asubuhi hadi usiku na wakati mwingine hata usiku wa manane, wakati wote alikuwa akimlalamikia kuhusu chochote.
Wakati pekee aliopata nafuu ni ule wakati aliokuwa nje shambani akilima na punda wake mzee. Alijitahidi sana kulima.
Siku moja alipokuwa shambani akilima, mkewe akamletea chakula cha mchana hukohuko shambani. Akampeleka punda wake kivulini, akakaa chini kwenye kigogo, na akaanza kula chakula chake. Mara moja, mke wake akaanza tena kumchamba mumewe.
Ni mwendo wa malalamiko, bugdha, maneno mengi makali; akaendelea na kuendelea. Mara ghafla, yule punda mzee akaruka juu na kurusha miguu yake yote ya nyuma hewani; hii miguu ilimpiga mkewe kwa kishindo kikubwa kisogoni. Na akafariki palepale.
Ilipowadia siku ya maziko siku kadhaa baadae, mtumishi wa Mungu (mchungaji) aliona kitu ambacho hakikuwa cha kawaida. Kila alipokuja muombolezaji wa kike kumpa pole yule mzee, alisikiliza kwa dakika moja, halafu akatingisha kichwa chake juu na chini ishara ya kukubali jambo; lakini kila alipokuja muombolezaji mwanaume, alisikiliza kwa dakika moja, kisha alitingisha kichwa chake upande wa kushoto hadi upande kulia kwa kukataa jambo.
Hali hii ilijirudia kila mara hadi mchungaji akatamani kumuuliza mzee kwa ufafanuzi kulikoni.
Sasa baada ya maziko, mchungaji aliongea na mzee yule mkulima na kumuuliza ilikuwaje akawa anatingisha kichwa chake juu na chini akionesha kukubaliana na wanawake; lakini kila alipokuja muombolezaji mwanaume alitingisha kichwa chake upande wa kushoto hadi upande wa kulia akionesha kutokubaliana na wanaume wote?
Yule mzee mkulima akamjibu: "Sasa, wanawake walikuwa wananijia na kusema jambo zuri juu ya marehemu mke wangu, jinsi alivyokuwa mrembo au jinsi alivyopendeza katika mavazi yake, hivyo nilitingisha kichwa changu juu na chini kukubaliana nao." "Na kwa wanaume ilikuwaje?" Mchungaji akauliza, "Walitaka kujua kama ninamuuza yule punda wangu." 🤣🤣🤔
Je, team kataa ndoa wako sahihi🤔🤔?
Wakati pekee aliopata nafuu ni ule wakati aliokuwa nje shambani akilima na punda wake mzee. Alijitahidi sana kulima.
Siku moja alipokuwa shambani akilima, mkewe akamletea chakula cha mchana hukohuko shambani. Akampeleka punda wake kivulini, akakaa chini kwenye kigogo, na akaanza kula chakula chake. Mara moja, mke wake akaanza tena kumchamba mumewe.
Ni mwendo wa malalamiko, bugdha, maneno mengi makali; akaendelea na kuendelea. Mara ghafla, yule punda mzee akaruka juu na kurusha miguu yake yote ya nyuma hewani; hii miguu ilimpiga mkewe kwa kishindo kikubwa kisogoni. Na akafariki palepale.
Ilipowadia siku ya maziko siku kadhaa baadae, mtumishi wa Mungu (mchungaji) aliona kitu ambacho hakikuwa cha kawaida. Kila alipokuja muombolezaji wa kike kumpa pole yule mzee, alisikiliza kwa dakika moja, halafu akatingisha kichwa chake juu na chini ishara ya kukubali jambo; lakini kila alipokuja muombolezaji mwanaume, alisikiliza kwa dakika moja, kisha alitingisha kichwa chake upande wa kushoto hadi upande kulia kwa kukataa jambo.
Hali hii ilijirudia kila mara hadi mchungaji akatamani kumuuliza mzee kwa ufafanuzi kulikoni.
Sasa baada ya maziko, mchungaji aliongea na mzee yule mkulima na kumuuliza ilikuwaje akawa anatingisha kichwa chake juu na chini akionesha kukubaliana na wanawake; lakini kila alipokuja muombolezaji mwanaume alitingisha kichwa chake upande wa kushoto hadi upande wa kulia akionesha kutokubaliana na wanaume wote?
Yule mzee mkulima akamjibu: "Sasa, wanawake walikuwa wananijia na kusema jambo zuri juu ya marehemu mke wangu, jinsi alivyokuwa mrembo au jinsi alivyopendeza katika mavazi yake, hivyo nilitingisha kichwa changu juu na chini kukubaliana nao." "Na kwa wanaume ilikuwaje?" Mchungaji akauliza, "Walitaka kujua kama ninamuuza yule punda wangu." 🤣🤣🤔
Je, team kataa ndoa wako sahihi🤔🤔?