Hahaha haya, kumbe huna proof hata moja, basi endelea kuamini, acha kuchamba wenzako ambao wanaamini tofauti na wewe. Ni msimamo tofauti tu, sio wote wanafatafata tu mambo yasiyo na proof. Na unavyomsema jamaa kua anafuata wikipedia huku imeandikwa na binadamu, unasahau kua vitu vilivyoandikwa kwenye wikipedia tunaweza kuviprove, wewe unatumia simu unapost JF dunia nzima tunaona, hiyo ni proof enough kua tunachofanya tunakijua hatuendi kwa imani, tunaenda kwa proof.
Twende mdogo mdogo
1. Umeuliza swali nami nimekujibu
2. Jibu langu pengine halijakufurahisha sana.. Mpaka umetumia neno KUCHAMBA WENZAKO! hapa umepotoka vibaya sijamchamba mtu bali tumeendelea kubishana kwa hoja
3. Umesema kila mtu ana imani yake hii inaweza kukugharimu maelezo ya kina kama nikiamua kukuuliza kama Atheism ni imani ama sio imani..
4. Kitu kinachoitwa imani hakina ithibati za kidunia kwakuwa ni cha kiroho....
5. Umezungumzia kuhusu smart phone... Hapa nimepapenda mno na labda unijibu kama unaweza kujua kwa hakika kwanini tunaweza kuwasiliana mimi na wewe kupitia hizi simu janja....
Je ni hizi vitu tulivyoshika na kubofya ndio vinafanya tuwasiliane?
Vipi kuhusu chaji
Vipi kuhusu network
Vipi kuhusu bundle
Vipi kuhusu software
Vipi kuhusu number ya simu
Vipi kuhusu IP address
Vipi kuhusu User ID
Mpaka tunaweza kuwasiliana hivi ni mchakato mrefu usioonekana... Zaidi ya
Siku tulizoshika mikononi
Maandishi tunayoandika
Minara ya simu nknk
Kwenye kila kitu kuna software na hardware...
Software haina ithibati ama proof ya kuonekana kwa macho so the God, hardware inaweza kuonekana kwa macho, na ukaipima kwa vipimo, ukaipa uzito na ujazo, ukaipa rangi nk
Na hapa ndio tunapopishana uelewano