Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Hahahaaaaa!!! Si kwa nondo hizi aise,sijutii kusoma sayansi!!

Kuna mercenary mmoja alivamia huu uzi juzi na kijipande chake cha quantum theory toka wikipedia,naona toka aseme anakwenda kulala hajaonekana mpaka leo.Sijui bado kalala!!

Mshana Jr, yuko wapi jamaa yako aliyesema amevurugwa na kipa wa Liverpool!?
Inabidi walale tu.

Maana tukija kwenye kujibu hoja kwa hoja,kwa mantiki, hakuna anayeweza kupinga ukweli.

Na mimi nikionekana mjanja sana,mjuzi sana, mwerevu sana etc, napata sifa za bure.

Mini sifa yangu kubwa ni kusimamia ukweli, hata pale ambapo si mjuzi sana.
 
[emoji3] [emoji3] [emoji3] kisomo cha kukariri misamiati na kuiweka bila mpangilio usioleweka almradi tu uonekane unajua
Hapana.

Mimi sijasema najua.

Mimi nimesema sijui.

Nimesema sijui chanzo cha ulimwengu ni nini.

Nimesema sijui chanzo cha maisha ya dunia hii ni nini.

Wewe umesema unajua.

Umesema unajua chanzo cha ulimwengu ni Mungu.

Umesemaunajua chanzo cha maisha ya dunia hii ni Mungu.

Mimi nimesema sijui.

Wewe umesema unajua.

Tafadhali usijaribu kunifanya mimi ndiye najifanya najua, wakati nimesema sijui,na nimesema ni muhimu tutafute majibu ili tujue, na wewe umesema unajua.Umesema unajua chanzo cha yote ni Mungu.
 
Mr. Kiranga , unaonekana upo vizuri sana kwenye physics, ni kama vile Mr. mshana alivo vizuri kwenye ulozi. Yote hayo, sisi watazamaji tuna jifunza vitu vipya!! [emoji119][emoji119]
Asante,

Hapo unaweza kujifunza Physics na ulozi katika thread moja.

Sijawahi kusikia Chuo Kikuu kinachotoa kozi hii.

Certainly katika Kiswahili.

Ni ChuoKikuu cha JF pekee.
 
Pengine Kiranga na wengine kama kina Immanuel, wanaweza kawa na imani kuwa Mungu yupo iwapo labda mtaziondoa zile sifa za upendo wote, uwezo wote, na nguvu zote, maana ndio contradiction nyingi wanaziona kutokea hapo!!
Ndugu yangu nimengojea comment hii kwa muda mrefu sana nikawa sijaiona.

Nilikuwa nasubiri tummalize huyu Mungu wa sifa hizo, ili tupande ngazi na kumjadili Mungu anayeweza ku make sense zaidi.

Nimefurahi sana kuona comment hii.

Imepandisha Least Common Denominator ya mjadala huu kwa 50% kwa maneno 34!
 
Unakumbuka nilikuomba ufanye nini? matokeo yake badala yake baada ya kufanya hivyo umeishia kuniuliza maswali halafu unasema sijajibu.
Uliniomba nifanye nini?

Unaelewa kwamba wewe kuniomba mimi nifanye chochote kunaonesha kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote na ujuzi wote hayupo?
 
hii kali mshana kiranga anaakili ndio maana hajajibu maana ya akili na akijibu maana ya akili bhasi mjadala utaisha na ww ukitaka kujuua huyu jamaa anaakili wtu kadhaa wamejaribu kutoa maana ya akili lakini hajazikubali anataka ya kwako tuu.. na ww ukijibu atakuongezea maswali ambayo yatataka yatataka ufafanuzi....kuna wakati unamuliza swali anakuuliza swali ni nini...mm nimegundua kumuelezea mungu yupo ni ngumu sana ila hoja za hayupo ni nyingi na zinanguvu..mjadala uishe
 
Uliniomba nifanye nini?

Unaelewa kwamba wewe kuniomba mimi nifanye chochote kunaonesha kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote na ujuzi wote hayupo?
Hapana mkuu,bali inaonesha ya kwamba mie ni binaadamu na si mungu na ndiyo maana ninaomba kwa sababu sina uwezo wote na ujuzi wote,ila Mungu mwenye uwezo wote na ujuzi wote ndio haombi kwa sababu yeye ana ujuzi wote na uwezo wote.
 
hii kali mshana kiranga anaakili ndio maana hajajibu maana ya akili na akijibu maana ya akili bhasi mjadala utaisha na ww ukitaka kujuua huyu jamaa anaakili wtu kadhaa wamejaribu kutoa maana ya akili lakini hajazikubali anataka ya kwako tuu.. na ww ukijibu atakuongezea maswali ambayo yatataka yatataka ufafanuzi....kuna wakati unamuliza swali anakuuliza swali ni nini...mm nimegundua kumuelezea mungu yupo ni ngumu sana ila hoja za hayupo ni nyingi na zinanguvu..mjadala uishe
Dah! kweli lazima ziwe nyingi,maana unaweza kumuuliza mtu swali akakwambia wewe kuniuliza swali ni ushahidi hakuna mungu.

Mtu akikosea kuandika ni ushahidi hakuna mungu,ukimkosoa pia ni ushahidi kuwa hakuna mungu.

Sasa kwa hali hiyo unaweza kujenga hoja hata 10000. Hivyo nakubaliana na wewe hoja nyingi.
 
Ukisoma vitabu vizuri utakuta simulizi za watu wa nyuma huko wakiadhibiwa na mungu,na mungu akijisifu kwa ukali.
Lakini pua kuna wengine huamini kuna moto huko mwisho wa siku kwa wale waliyotenda maovu.

Sasa mtu anapokuja na suala la sifa ya upole tu kwa mungu na kuanza kutaja iki sijui kisingekuwepo kisa upole wa mungu unashindwa kujua unamsaidiaje,kufa ni jambo la lazima ila mtu anakwambia mungu mwenye upendo hawezi kuruhusu watu wake wafe.
Bwana Tz mbongo , hicho pengine ni kitabu cha biblia au Quran tu, lakini kuna dini nyingi sana tofauti na hizi Abrahamic Religions!!

Je, ipi ni sahihi!?

Nilishawahi kusikia mahali kuwa dini si uthibitisho kuwa Mungu yupo, ila ni michakato tu ya mwanadamu katika kumtafuta Mungu(Mwanzo/chanzo/mwanzilishi) wa huu ulimwengu!!

Kwa maoni yangu ni kuwa Mungu yupo/kipo/vipo, huku nikimaanisha kuwa mungu ni chanzo cha ulimwengu huu(kama ni bing bang au kingine), maadam ni chanzo cha ulimwengu!!

Watu tunakosea sana, kumuona mwenzako kuwa hayuko sahihi kwenye kile anachokiamini na kuona kuwa sisi ndio tupo sahihi na hivyo kumlazimisha afuate ninayoamini, ni makosa makubwa sana, kwa sababu dini ni nyingi na hakuna hata mmoja aliyeleta uthibitisho hususa, kuhusu dini yake.

Mfano nimesikia maeneo flani kule zanzibar, watu wanapelekwa polisi wanapoonekana wakila chakula hadharani, muda wa mchana, haya ni makosa, kumlazimisha kila mtu afwate unachokiamini!!
 
Bwana Tz mbongo , hicho pengine ni kitabu cha biblia au Quran tu, lakini kuna dini nyingi sana tofauti na hizi Abrahamic Religions!!

Je, ipi ni sahihi!?

Nilishawahi kusikia mahali kuwa dini si uthibitisho kuwa Mungu yupo, ila ni michakato tu ya mwanadamu katika kumtafuta Mungu(Mwanzo/chanzo/mwanzilishi) wa huu ulimwengu!!

Kwa maoni yangu ni kuwa Mungu yupo/kipo/vipo, huku nikimaanisha kuwa mungu ni chanzo cha ulimwengu huu(kama ni bing bang au kingine), maadam ni chanzo cha ulimwengu!!

Watu tunakosea sana, kumuona mwenzako kuwa hayuko sahihi kwenye kile anachokiamini na kuona kuwa sisi ndio tupo sahihi na hivyo kumlazimisha afuate ninayoamini, ni makosa makubwa sana, kwa sababu dini ni nyingi na hakuna hata mmoja aliyeleta uthibitisho hususa, kuhusu dini yake.

Mfano nimesikia maeneo flani kule zanzibar, watu wanapelekwa polisi wanapoonekana wakila chakula hadharani, muda wa mchana, haya ni makosa, kumlazimisha kila mtu afwate unachokiamini!!
Hata kinachoendelea hapa ni kwamba atheists wanatumia maelezo ya vitabu vya dini kupinga uwepo wa mungu,wakati kama ulivyosema dini ziko nyingi na maelezo hutofautiana.

Ndiyo maana mie nimekuwa nikiwaambia kuwa hizo sijui contradictions haziwezi kutumika kusema hakuna mungu kwa sababu ni mambo yenye kuhusu maelezo ya baadhi ya vitabu vya dini.
 
Maneno yako yanazidi kunithibitisha kuwa mungu amedanganya maana unajua wazi huo uwongo uliopo ktk biblia ww huna mamlaka ya kurekebisha maana huna asili ya kiyahudi ww wa kwetu

Hivi kumbe maneno yanaweza kuthibitisha?

Nimekuuliza mara kwa mara kwamba Mungu amedanganya? Unajibu amedanganya na kuleta maandiko.

Kwa kuwa unadai Mungu AMEDANGANYA, alikudanganya namna gani?

Ulichokileta hapa ni vitabu kisha unasema Mungu amedanganya.

Unaweza kuthibitisha alivyokudanganya? (Japo wakati huohuo unadai hayupo).
 
mpatto

Tena mkuu kama utachunguza vizuri utagundua kuwa hata jinsi atheists humu wanavyoziwakilisha hoja zao kuhusu mungu zimeegea sana kutoka kwenye mafundisho ya biblia.

Labda pengine kwa kuwa mtu kama Kiranga ametokea huko.
 
Back
Top Bottom