Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Nimeandika kuuliza andiko lina contradiction nyingi mama chache? Chache? Nyingi ama chache? Nimeandika hivyo?

Unaweza kunipa nukuu ya nilipoandika hivyo au unaniwekea maneno ambayo sijayaandika?

Nikisema hunielewi na unanipa maneno ambayo sijayaandika utakataa?

Sawa mkuu, "Hayo maelezo ya mfano uliyoyasema yana contradictions za wazi na nyingi au hayana?"
ntakua naenda kwa huo mtindo.
Sasa naomba upitie tena haya maelezo kisha unipe jibu.

"...endapo mtu ataandika habari inayomhusu Kiranga ambae simfaham, akaeleza sifa zake na mambo mengi kuhusu Kiranga.

Nikisoma au kusikia hizo habari za hicho kitabu, ntakuwa sahihi kusema hakuna mtu mwenye sifa hizo mlizompa Kiranga na kuhitimisha Kiranga hayupo?"

Huyo msomaji yuko sahihi?
 
Hujathibitisha Mungu yupo.

Hujaondoa contradictions nilizosema kuhusu uwepo wa Mungu, kama hata umezielewa.
Hivi Mkuu, unamaanisha ya kwamba huu ulimwengu ulitokea tu bila ya yeyote yule aliye mastermind viumbe na vitu vyote kutokea?

Nieleze kisayansi, vitu vyote ulimwenguni origin yake ilikua ni nini? .. Pia useme kbl ya dunia na sayari zote, jua, mwezi nyota na kila kitu kuwepo kulikua na nini? ... Kila kitu ueleze kisayansi
 
Kujua ni kukubali jambo baada ya kuhakikisha kwa namna iliyo logically consistent, isiyo na contradiction, iliyo evidence based, iliyo testable.

Kuamini ni kutarajia kitu bila kujua.

Kila jambo ambalo tunajua binadamu lazima liwe logically consistent?, evidence based?, na testable?
 
Sawa mkuu, "Hayo maelezo ya mfano uliyoyasema yana contradictions za wazi na nyingi au hayana?"
ntakua naenda kwa huo mtindo.
Sasa naomba upitie tena haya maelezo kisha unipe jibu.

"...endapo mtu ataandika habari inayomhusu Kiranga ambae simfaham, akaeleza sifa zake na mambo mengi kuhusu Kiranga.

Nikisoma au kusikia hizo habari za hicho kitabu, ntakuwa sahihi kusema hakuna mtu mwenye sifa hizo mlizompa Kiranga na kuhitimisha Kiranga hayupo?"

Huyo msomaji yuko sahihi?
Akijibu nitag
 
Sikubali ,Mimi namkubali Mungu Mkuu niliyemgundua kwa utashi wangu mwenyewe.

Sio yule Mungu uchwara wa kwenye tuvitabu twa uongo uongo
Kwanini haukubali kama Beyonce ni mungu?

Unaposema kwa utashi wako mwenyewe una maana gani?
Hivi mfano ungezaliwa kwenye jamii ambayo hawajui lolote kuhusu mungu unadani ungeweza kuwa na huo utashi?
 
Hivi Mkuu, unamaanisha ya kwamba huu ulimwengu ulitokea tu bila ya yeyote yule aliye mastermind viumbe na vitu vyote kutokea?

Nieleze kisayansi, vitu vyote ulimwenguni origin yake ilikua ni nini? .. Pia useme kbl ya dunia na sayari zote, jua, mwezi nyota na kila kitu kuwepo kulikua na nini? ... Kila kitu ueleze kisayansi
Kwanza kabisa, simaanishi ulimwengu ulitokea tu.

Pili, kuongelea "yeyote" ni kuongelea mtu/ nafsi. Hii ni bias inayotokana na udhaifu wa mawazo yetu kwa sababu tunaangalia mambo kwa scale yetu ya universe.

Tatu, suala zima la "cause and effect", linalozaa swali la ulimwengu umeanzaje, ni suala linalokuja kwa kufikiri kwamba time is a real and absolute thing.It is not. In quantum physics, at the singularity inside a black hole, time can begin in a new baby universe. Some aspects of quantum physics, especially through the Copenhagen interpretation, allow for causality to break and effects to happen before or outside the lines of causes.

Nne, mtu kutojua jibu sahihi la swali haina maana hawezi kujua jibu fulani si sahihi. Usifanye kwamba mtu kutojua chanzo cha ulimwengu basi maana yake umeumbwa na Mungu. Mtu anaweza kuwa hajui ulimwengu umeanzaje, lakini akajua kwamba ulimwengu haujaumbwa na mtoto wake. Kwa sababu mtoto wake alipozaliwa,huyo mtu tayari alikuwepo.

Katika base 10 math, mtu anaweza kuwa hajui square root ya 2 ni nini. Lakini akajua kwamba ni lazima iwe ndogo kuliko 2. Hivyo ukimwambia square root ya 2 ni 10, hata kama hajui square root ya 2 ni nini, anaweza kujua haiwezi kuwa 10. Kwa sababu kwanza 10 ni kubwa kuliko 2 na kwa hivyo haiwezi kuwa square root ya 2, lakini pia test ya ku square 10 haitupi 2, inatupa 100.

Kwa hiyo, maswali tusiyoyajua majibu yake, tusiyape jibu la Mungu tu, tuyachunguze tuyajue vizuri. Na tunaweza kuyachunguza kwa "elimination method". Kama vile uunavyoweza kusema "natafuta square root ya 2 kwa elimination method.

- Square root ya 2 haiwezi kuwa kubwa zaidi ya 2 (kwa sababu namba ikiwa kubwa zaidi ya 2, uki i squared jibu litakuwa kubwa kuliko 2)
-Square root ya 2 haiwezi kuwa ndogo zaidi ya 1 (kwa sababu 1 squared ni moja)
- Square root ya 2 ipo kati ya 1 na 2

Tutafute square root ya 2 to 3 decimal places

Tuchukue namba iliyo kati kati ya 1 na 2 tuijaribu

1.5 squared ni 2.25 hii bado ni kubwa kuliko 2

Tuchukue namba iliyo kati ya 1.5 na 1 tuijaribu.

1.25 squared ni 1.5265 hii ni ndogo kuliko 2, tunahitaji kubwa zaidi

Tuchukue namba iliyo kati ya 1.25 na 1.5, tuijaribu

1.375 squared is 1.890625, we are getting there, but not quite there yet. It needs to be bigger.

Tuchukue namba iliyo kati ya 1.375 na 1.5

1.4375 squared is 2.06640625. It needs to be a little bit smaller.

It needs to be between 1.4375 and 1.375

1.40625 squared 1.9775390625. Getting there. It needs to be just higher.

It needs to be between 1.40625 and 1.4375.

1.421875 squared is 2.021728515625. Almost there. Let's make our answer accurate to 4 decimal places.

It needs to be between 1.421875 and 1.40625

1.4140625 squared is 1.99957275390625. Pretty close, but let's nail it higher.

It needs to be between 1.4140625 and 1.421875

1.41796875 squared is 2.010635375976563. It needs to be a tad smaller.

It needs to be between 1.41796875 and 1.4140625

1.416015625 squared is 2.005100250244141. It needs to be a teeny bit smaller.

It needs to be between 1.416015625 and 1.4140625

1.4150390625 squared is 2.002335548400879. It needs to be a teeny weeny bit smaller.

It needs to be between 1.4150390625 and 1.4140625

1.41455078125 squared is 2.000953912734985.

Kwa nini nimeandika namba zote hizi.

1. Kuonesha kwamba, unaweza kujua jibu lisilo sahihi hata kama hujui jibu sahihi, kama unajua kanuni fulani za msingi.

2. Kuonesha kwamba unaweza kuona convergence kuelekea kwenye jibu sahihi inaelekea wapi, na wapi pa kuachana napo, hakuna jibu sahihi.

Habari za Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aliyeumba dunia hii yenye mabaya mengi ziko nje ya convergence ya jibu sahihi. Tuachane nazo, zina contradiction.

Tutafute majibu katika habari zilizo katika convergence ya majibu sahihi.

Hutakiwi kutafuta square root ya 2 kwenye namba zilizo kubwa kuliko 2.

Ukifanya hivyo hutapata jibu sahihi.

Hutakiwi kutafuta chanzo cha ulimwengu kwenye habari za Mungu.

Ukifanya hivyo, hutapata jibu sahihi.
 
Sawa mkuu, "Hayo maelezo ya mfano uliyoyasema yana contradictions za wazi na nyingi au hayana?"
ntakua naenda kwa huo mtindo.
Sasa naomba upitie tena haya maelezo kisha unipe jibu.

"...endapo mtu ataandika habari inayomhusu Kiranga ambae simfaham, akaeleza sifa zake na mambo mengi kuhusu Kiranga.

Nikisoma au kusikia hizo habari za hicho kitabu, ntakuwa sahihi kusema hakuna mtu mwenye sifa hizo mlizompa Kiranga na kuhitimisha Kiranga hayupo?"

Huyo msomaji yuko sahihi?
Umekubali sijataja contradictions chache, hilo jambo umeweka wewe.

Mimi nimetaja "yana contradictions nyingi na za wazi au hayana".

Unakubali kwamba ume misrepresent maneno tangu kwanza kabla hatujaendelea?

Unaona jinsi gani ninavyopata tabu kujadiliana na wewe kwa sababu hunielewi.

Huna nidhamu ya kuheshimu maneno ya watu.

Mtu kaandika "yana contradictions nyingi na za wazi au hayana" wewe unasema kaandika "yana contradictions nyingi au chache".

Unaelewa hayo ni mambo mawili tofauti?

Cc Mjina Mrefu
 
Sikubali ,Mimi namkubali Mungu Mkuu niliyemgundua kwa utashi wangu mwenyewe.

Sio yule Mungu uchwara wa kwenye tuvitabu twa uongo uongo
Unajuaje kwamba Mungu wa utashi wako yupo na si wishful thinking?

Mungu wa utashi wako ana sifa gani?
 
Naona hoja yako unataka kuijenga kwenye kutafsiri kila kitendo kinafanywa na Mungu dhidi ya viumbe.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote, mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kabla chochote hakijaumbwa, alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauwezi kuwa na baya lolote.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huo?

Na kama hakuumba huo, kaumba huu ambao mabaya yanaweza kutokea, utasemaje mabaya hayakuachiwa na Mungu yawaathiri viumbe wakati alikuwa na uwezo kuyazuia?

Kitu ambacho unakosea na utaendelea kukosea

Ninakosea wapi? Kivipi?

Kama mtu akitaka kujiuliza kwa nini mwanamke abebe mimba miezi tisa halafu ajifungue kwa uchungu na mwanaume kwa nini asibebe?

Utampa jibu gani?

Nikikwambia moja ya sababu ni kwa kuwa ulimwengu haujaumbwa na Mungu, ungeumbwa na Mungu kungekuwa hakuna uchungu wala haja ya laborious sexual reproduction utasema nini?
 
Ndiyo maana nikasema kuwa watu wanatoa maelezo yenye kujipinga kuhusu Mungu,na ndiyo maana wewe unaonesha maelezo hayo jinsi yanavyojipinga.

Ukisema mungu hawezi kujieleza mwenyewe kwa sababu hayupo, hapa panahitaji ushahidi kuhusu kutokuwepo kwake.
Ushahidi nimeutoa wa proof by contradiction.

Unachosema hapo ni sawa na mtu aseme "pembe tatu duara ipo, ila wanaoisema ndio wanakosea na unapata sehemu ya kuipinga, ila pembettu duara ipo, yenyewe haisemi, ila ipo tu".

Nikikwambia hivyo utakubali?
 
Naona hapo fikra yako ndio inapinga.

Kama anaweza yote kwa nini asifanye chochote?
Na jee upendo ndio sifa pekee ya Mungu?
Kama anaweza yote, kwa nini hakuumba ulimwengu ambao hauna mabaya?

Ukiuliza upendo ndiyo sifa pekee ya Mungu una maana gani kutafuta upendo kama sifa pekee?

Kwa nini unauliza sifa pekee, badala ya sifa zote?

Nikichanganya mkojo na maji kwenye glasi, halafu nikakupa unywe, nikakwambia glasi ina maji yaliyochanganyika na mkojo, halafu ukaniuliza "mkojo ndiyo kitu pekee kilicho kwenye hii glasi?" mimi ambaye nishakwambia glasi ina maji na mkojo nilitafsiri vipi hilo swali?

Nilitafsiri kwamba unataka nikujibu "hapana, glasi ina mkojo na maji".

Kwa sababu unataka kusema "ahaa, kumbe glasi ina maji pia, basi mimi nitakunywa maji yaliyomo katika glasi" bila kufikiri kwamba maji yamechanganyika na mkojo na huwezi kunywa maji bila mkojo?

Kwa nini unaulizia sifa pekee, badala ya kuulizia sifa zote na kuzichambua katika ukamilifu wake?

Dhana ya Mungu ikiwa na sifa za uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kama nilivyotaja hapo awali, halafu dunia iliyopo yenye mabaya ikaonekana ku contradict kuwepo kwa Mungu anayesemwa ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kwa nini unaulizia upendo tu, wakati contradiction ina contradict combination ya uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?

Unaelewa objection yangu iko wapi?
 
Umekubali sijataja contradictions chache, hilo jambo umeweka wewe.

Mimi nimetaja "yana contradictions nyingi na za wazi au hayana".

Unakubali kwamba ume misrepresent maneno tangu kwanza kabla hatujaendelea?

Unaona jinsi gani ninavyopata tabu kujadiliana na wewe kwa sababu hunielewi.

Huna nidhamu ya kuheshimu maneno ya watu.

Mtu kaandika "yana contradictions nyingi na za wazi au hayana" wewe unasema kaandika "yana contradictions nyingi au chache".

Unaelewa hayo ni mambo mawili tofauti?

Cc Mjina Mrefu

Unaweza kurudi kwenye hoja ya msingi kujibu nilichokuuliza tokea mwanzo?

La kutokua na nidhamu niachie mimi.
Wewe unaeheshimu mawazo au maandishi ya watu ulithubutu vipi kusema kuna kitu muhimu sana nimeacha kukiandika?

Kwa vile nimeandika tofauti na mawazo yako ndio niwe nimeacha kuandika kitu?

Hii post namba 1361 inahitaji jibu lako bado.

Usingeanza kuweka hisia zako kwenye mfano wangu tokea awali tusingefika huku.
 
Una ushahidi gani kuwa vilivyomo humu ni vya kuumbwa na mungu huyo ambaye umeshndwa kuthbitisha uwepo wake?

Kwa nini unaamini kuna chanzo cha ulimwengu na uhai?
Sasa tuthibitishie wewe kwamba vilivyomo havijaumbwa na Mungu na pia tuthibitishie kuwa hakuna uwepo wa Mungu
 
Kama Mungu ndiye muumba wa yote, mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kabla chochote hakijaumbwa, alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauwezi kuwa na baya lolote.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huo
Hakuumba kwa sababu anaamua atakavyo yeye sio utakavyo wewe.

Ukiuliza upendo ndiyo sifa pekee ya Mungu una maana gani kutafuta upendo kama sifa pekee?

Kwa nini unauliza sifa pekee, badala ya sifa zote?

Wewe umesimamia zaidi kwenye mungu kukosa upendo sababu kuna mabaya duniani.

Mungu anazo sifa nyingine ndio maana kuna vitu vingine unashindwa kuvitafsiri sababu una base kwenye upendo tuu.

Mfano
Mimi nina mtoto wangu yuko kwenye 20's
Kafanya kosa ambalo mahakama ikamkuta na hatia. Ikamuamuru alipe fidia 5m ambayo iko ndani ya uwezo wangu.
Lakini mimi sijalipa na yule mtoto wangu akafungwa miaka 2.

Hapo nimekosa upendo kwa kutolipa faini na kumwepusha na ubaya wa kwenda jela?
 
Unaweza kurudi kwenye hoja ya msingi kujibu nilichokuuliza tokea mwanzo?

La kutokua na nidhamu niachie mimi.
Wewe unaeheshimu mawazo au maandishi ya watu ulithubutu vipi kusema kuna kitu muhimu sana nimeacha kukiandika?

Kwa vile nimeandika tofauti na mawazo yako ndio niwe nimeacha kuandika kitu?

Hii post namba 1361 inahitaji jibu lako bado.

Usingeanza kuweka hisia zako kwenye mfano wangu tokea awali tusingefika huku.
Unaweza kukubali kwamba umeandika nimeandika kitu ambacho sijaandika?

Unaweza kukubali kwamba uliacha kuandika kama maelezo yana contradiction au hayana, jambo ambalo bila ya kuliandika, hatuwezi kufikia conclusion yoyote ya kueleweka?
 
Ulivyojibu unamaanisha halipo?
Kama lipo, silijui. Ndiyo maana nikakupa nafasi unifahamishe tulijadili kama unaona lipo.

Maana na mimi naweza kujifunza kitu kipya ambacho sijakijua hapo awali.
 
Hakuumba kwa sababu anaamua atakavyo yeye sio utakavyo wewe.

1. Unaelewa kwamba sijabisha kuwa hajaumba anavyotaka yeye, nimekuomba unieleze sababu za yeye kuumba hivyo?
2. Unaelewa kwamba sijataka aumbe ninavyotaka mimi, nimeuliza kwa nini hana logical consistency, hajaumba anavyotaka yeye mwenyewe, haeleweki, anajipinga?


Wewe umesimamia zaidi kwenye mungu kukosa upendo sababu kuna mabaya duniani.

Mungu anazo sifa nyingine ndio maana kuna vitu vingine unashindwa kuvitafsiri sababu una base kwenye upendo tuu.

Mfano
Mimi nina mtoto wangu yuko kwenye 20's
Kafanya kosa ambalo mahakama ikamkuta na hatia. Ikamuamuru alipe fidia 5m ambayo iko ndani ya uwezo wangu.
Lakini mimi sijalipa na yule mtoto wangu akafungwa miaka 2.

Hapo nimekosa upendo kwa kutolipa faini na kumwepusha na ubaya wa kwenda jela?

Wewe una uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?

Kwa nini Mungu wenu mnayesema ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote ana contradiction?
 
Back
Top Bottom