Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Mkuu huyu Mungu asiyekuwepo lakini anajipinga mwenyewe ndio yupi?
Mungu hayupo, maelezo yanayomuelezea huyo Mungu, dhana ya huyo Mungu, ambayo kimkato inaitwa "Mungu" badala ya kusema "dhana ya kuwapo huyo Mungu", kama ninavyoweza kuhadithia hadithi ya Willy Gamba na kumuita "Willy Gamba"badala ya kumuita "the Aristablus Elvis Musiba character created as Willy Gamba" kila wakati, inajipinga yenyewe.

Ushaelewa?
 
Nimetumia akili yangu nimefahamu Mungu hayupo, ni hadithi tu.

Kwa sababu ana contradictions nyingi sana.

Unaambiwa eti Mungu ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.Ana haki ya juu kabisa.

Halafu unaambiwa eti kahukumu wanyama katika gharika, wamekufa sana kwa mafuriko, kwa makosa waliyoyafanya watu.

Sasa Mungu gani wa haki anahukumu wanyama kwa makosa ya watu?

Tunaambiwa Mungu ni wa haki, lakini anahukumu vitukuu na vitukuu vya vitukuu kwa makosa ambayo hata havijafanya, yamefanywa na wazee wao zamani sana huko.

Sasa huyu Mungu wa haki kwa nini anahukumu vitukuu hivi kwa makosa ambayo havijafanya? Mungu anashindwa kwa haki na hakimu ambaye sheria inamkataza kumhukumu mtoto kwa kosa la baba?

Tunaambiwa eti Mungu anapata hasira. Hasira ni udhaifu ambao unaonesha kukosa control, kukosa kujua mambo vizuri, kupata matokeo ambayo hukutegemea, ni udhaifu. Sasa huyu Mungu aliyekamilika kila kitu hasira anaanzaje kuipata?

Tunaambiwa Mungu anapanga mpango, halafu unaenda tofauti na alivyotaka, anataka kughairi.

Sasa huyu Mungu anayejua kila kitu inakuwaje hakujua mpango huu utaenda hivi, mpaka anataka kughairi?

Tunaambiwa Mungu ana taifa lake teule, sasa Mungu mwenye upendo wote inakuwaje atoe upendeleo kwa taifa lake teule?

Tunaambiwa kuna watu Mungu atawaziba mioyo, masikio na macho, hata wajitahidi vipi kumjua hawatamjua, hao msihangaike nao. Sasa inakuwaje Mungu awazibe masikio, macho na mioyo watu wasimjue? Na hawa nao atawahukumu kwa kutomjua?Au atawasamehe tu kwa sababu ni yeye mwenyewe aliwaziba mioyo, masikio na macho na hivyo anajua wasingeweza kumjua?

Tunaambiwa Mungu yeye ndiye anatoa neema ya kumjua, sasa wale ambao hajawapa neema ya kumjua atawahukumu kwa kutomjua au atawachia tu kwa sababu ni yeye mwenyewe hakuamua kuwapa neema ya kumjua?

Tunaambiwa mti ambao hauzai matunda utakatwa na kuchomwa moto kama adhabu ya kutotoa matunda, sasa Mungu mbona anauhukumu mti kwa sababu haujazaa matunda, wakati yeye ndiye anatoa rehema ya kuzaa matunda?

Contradictions allover the place.

Ukichunguza unaona huyu Mungu katungwa na watu tu, ndiyo maana kapewa tabia za watu.

Nakuhurumia sana Mkuu kiranga, inshort umepotea! Yani hutambui uwepo wa Mungu!!! Subhanallah!
 
Nkiiulizwa kujua ni nini siwezi kujibu,sijaelewa kwa maana haujaeleza kujua ina maana gani.
Kujua ni kukubali jambo baada ya kuhakikisha kwa namna iliyo logically consistent, isiyo na contradiction, iliyo evidence based, iliyo testable.

Kuamini ni kutarajia kitu bila kujua.
 
Nakuhurumia sana Mkuu kiranga, inshort umepotea! Yani hutambui uwepo wa Mungu!!! Subhanallah!

Kama nimepotea, kupotea kwangu nako kunathibitisha Mungu hayupo.

Kama Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote,upendo wote, angekuwepo,hakuna kiumbe wake hata mmoja ambaye angeweza kupotea.

Una ji contradict.
 
Kama nimepotea, kupotea kwangu nako kunathibitisha Mungu hayupo.

Kama Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote,upendo wote, angekuwepo,hakuna kiumbe wake hata mmoja ambaye angeweza kupotea.

Una ji contradict.

Sawa Mkuu! Ila kitambo ulipotea humu..kwema lakini?
 
Sawa Mkuu! Ila kitambo ulipotea humu..kwema lakini?
Nilipotea kwa sababu Mungu hayupo, nilipandamilimanihuko kumtafuta sijamuona.

Angekuwepo ningemuona hapahapa JF, wala nisingehitaji kupanda milimani kumtafuta.

Nisingepotea.

Hahaaaa.

Mimi kwangu kwema, naeneza wema kwa wengine kupitia mijadala ya kuhabarishana mambo mazito hapa.
 
Hapana, ninajikita kwakina zaidi ndani ya mada, nataka kujua.

Wewe unaelea juu juu yamjadala,unaona nikijikita kwakinanatokanje ya mjadal.

Umesema imani ya Mungu ipo naturally kabisa kwenye akili.

Kwamba kila mtu anayo hiyo imani kichwani, naturally.

Na ili tujue mambo yaliyo kichwani naturally na tuyatofautishe na tunayojifunza baadaye, tunayojifunza baada ya kuzaliwa, inabidi turudi kwa mtoto anapozaliwa.

Ndiyo maana nakuuliza mtoto anapozaliwa, kwa mujibu wako, ana akili na anajua Mungu yupo?

Kwa sababu kama ana akili na anajua Mungu yupo,na unaweza kuthibitisha hilo, maneno yako yanakuwa na msingi wa kuendelea kuyachunguza.

Lakini kama hana akili, au ana akili lakini anakuwa hajamjua Mungu, tunaona kwamba hizi habari za kumjua Mungu watu wanajifunza tu baada ya kuzaliwa, lakini mtoto anapozaliwa anakuwa hajui habari hizi.

Sasa nikichunguza kwa kina zaidi, nijue, kwa mujibu wako, mtoto anapozaliwa, anakuwa ana akili au hana, kusudi tujue kama ana akili ana amini Mungu au haamini, utasemaje maswali hayo ni kutoka nje ya mjadala, wakati mimi najikita deep kabisa kwenye mjadala?
Kila mwanadamu ana akili na mtot pia ni mwanadamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu hayupo, maelezo yanayomuelezea huyo Mungu, dhana ya huyo Mungu, ambayo kimkato inaitwa "Mungu" badala ya kusema "dhana ya kuwapo huyo Mungu", kama ninavyoweza kuhadithia hadithi ya Willy Gamba na kumuita "Willy Gamba"badala ya kumuita "the Aristablus Elvis Musiba character created as Willy Gamba" kila wakati, inajipinga yenyewe.

Ushaelewa?

Nimeelewa ulichokiandika, jibu zuri lenye mifano ya kuongezea uelewa.

Kwanza, wewe ndio umeamua kusema dhana ya Mungu na sio Mungu unaesema hayupo.

Pili, endapo mtu ataandika habari inayomhusu Kiranga ambae simfaham, akaeleza sifa zake na mambo mengi kuhusu Kiranga.

Nikisoma au kusikia hizo habari za hicho kitabu, ntakuwa sahihi kusema hakuna mtu mwenye sifa hizo mlizompa Kiranga na kuhitimisha Kiranga hayupo?
 
Nimeelewa ulichokiandika, jibu zuri lenye mifano ya kuongezea uelewa.

Kwanza, wewe ndio umeamua kusema dhana ya Mungu na sio Mungu unaesema hayupo.

Pili, endapo mtu ataandika habari inayomhusu Kiranga ambae simfaham, akaeleza sifa zake na mambo mengi kuhusu Kiranga.

Nikisoma au kusikia hizo habari za hicho kitabu, ntakuwa sahihi kusema hakuna mtu mwenye sifa hizo mlizompa Kiranga na kuhitimisha Kiranga hayupo?

Nimesema Mungu hayupo kwa sababu dhana ya kuwepo kwake ina contradictions.

Umeacha kuelezea suala moja muhimu sana.

Hizo habari za Kirangaulizozitolea mfano, zina contradictions nyingi sana na za wazi sana au hazina contradiction yoyote?
 
Siwezi kukuthibitishia hilo ila akili ako inaweza kuthibitisha hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana, nataka wewe unithibitishie hilo.

Kunya unye wewe halafu unaniambia mavi nizoe mimi? Kwa nini? Unanifananisha na mtumwa wako?

Umeweka claim hapa, thibitisha, ni wajibu wako. Usinisukumie mimi kazi yako.

La sivyo sema umedanganya, umesema jambo ambalohuwezikuthibitisha na hujatuelezeakwa nini huwezikuthibitisha.

Akili yangu hainithibitishii hilo, hata sikumbuki chochote kuhusu nilivyozaliwa, sembuse kuweza kukumbuka kama niliamini Mungu au sikuamini.

Kama huwezi kuthibitisha unalazimisha jambo ambalo hulijui.
 
Umeacha kuelezea suala moja muhimu sana.

Hizo habari za Kiranga zina contradictions nyingi sana na za wazi sana au hazina contradiction yoyote?

Contradiction na mapungufu mengine yatakayokuwepo yanategemea uwezo na uelewa wa huyo msomaji, anaweza kuona makosa au matatizo mengi zaidi ya ulichokisema contradiction. Tufanye hayo yote yapo kwenye post ya mwanzo uliyonikumbusha kwa kuwa nilisahau.

Swali langu lipo hapa, ni sawa huyo msomaji kuhitimisha kwamba Kiranga hayupo?
 
Hapana, nataka wewe unithibitishie hilo. Akili yangu hainithibitishii hilo, hata sikumbuki chochote kuhusu nilivyozaliwa, sembuse kuweza kukumbuka kama niliamini Mungu au sikuamini.

Kama huwezi kuthibitisha unalazimisha jambo ambalo hulijui.
Sijakulazimisha mkuu ni tunajadiliana na kamwe siwezi kukuthibitishia hilo kwa kuwa nina uhakika unalifahamu kwa sababu kila mwanadamu kwenye akili yake ipo hivyo labda kwa kuwa nadharia nyingine zimekupumbaza na umebaki na kupingana kilicho kwenye akili ako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipotea kwa sababu Mungu hayupo, nilipandamilimanihuko kumtafuta sijamuona.

Angekuwepo ningemuona hapahapa JF, wala nisingehitaji kupanda milimani kumtafuta.

Nisingepotea.

Hahaaaa.

Mimi kwangu kwema, naeneza wema kwa wengine kupitia mijadala ya kuhabarishana mambo mazito hapa.

Nashkuru upo mzima...usiku mwema mkuu!
 
Contradiction na mapungufu mengine yatakayokuwepo yanategemea uwezo na uelewa wa huyo msomaji, anaweza kuona makosa au matatizo mengi zaidi ya ulichokisema contradiction. Tufanye hayo yote yapo kwenye post ya mwanzo uliyonikumbusha kwa kuwa nilisahau.

Swali langu lipo hapa, ni sawa huyo msomaji kuhitimisha kwamba Kiranga hayupo?
Ondoa uwezo wa msomaji as an issue, ukileta habari za uwezo wa msomaji na mimi naweza kulalamikiauwezo wako muandikaji kwa sababu hujazungumzia habari ya contradiction tangu mwanzo.

Suppose msomaji ana uwezowa kuona contradiction kama contradiction na habari isiyo na contradiction kama habari isiyo na contradiction.

Hizohabari za mfanoza Kiranga, kazisoma na kuona zina contradictions za wazi na nyingi? Au hazina contradiction?
 
Sijakulazimisha mkuu ni tunajadiliana na kamwe siwezi kukuthibitishia hilo kwa kuwa nina uhakika unalifahamu kwa sababu kila mwanadamu kwenye akili yake ipo hivyo labda kwa kuwa nadharia nyingine zimekupumbaza na umebaki na kupingana kilicho kwenye akili ako

Sent using Jamii Forums mobile app
Unasema hujanilazimisha halafu unanilazimisha zaidi?

Kubali umeandika kitu ambaco huwezikuthibitisha.

Umeandika hogwash, malarkey, calumny, abracadabra, phoney baloney.
 
Ondoa uwezo wa msomaji as an issue, ukileta habari za uwezo wa msomaji na mimi naweza kulalamikiauwezo wako muandikaji kwa sababu hujazungumzia habari ya contradiction tangu mwanzo.

Suppose msomaji ana uwezowa kuona contradiction kama contradiction na habari isiyo na contradiction kama habari isiyo na contradiction.

Hizohabari za mfanoza Kiranga, kazisoma na kuona zina contradictions za wazi na nyingi? Au hazina contradiction?

Sasa umetoa wapi contradiction kwenye mfano wangu wa habari ya Kiranga? Ni wewe umesema nimesahau wakati mwandishi kaandika habari zake kuhusu Kiranga.

Kitu gani kilipelekea useme nimesahau contradiction? Vinginevyo uwe unamfaham Kiranga fika ndio utasema kuna conteafiction na mapungufu ya uandishi, hapo ndio nilpoweka uwezo na uelewa atakavyoamua.
 
Back
Top Bottom