Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

nadhani hapa umeamua tu kutoa njibu lolote maana huna jibu wala huo ufahamu unapima vp roho huwezi kuniambia.
Hapana hilo ndio jibu sahihi kama kuna tofauti na hilo liweke hapa....
 
Mkuu,haupo sahihi hata kiduchu.Umemuuliza Kiranga kama 'ana akili',yeye kataka umwambie maana ya akili unayouliza kama anayo ili akamwambie "NDIYO NINAYO AU SINA".
angetoa definition ya akili mada ingeishia hapo, maana angesema akili ni ''uwezo wa kupata, kuelewa na kutumia maarifa na taaluma'' sasa Kiranga angejibu kwa urahisi tu kwamba uwezo huo ninao, na Mshana Jr angebaki hana cha kusema. Hii argument aliyotaka kuileta Mashana ni ya kucheza na lugha na ni ya kitoto sana, it is obvious kwa watu wanao elewa lugha kwamaba ''akili'' na ''Mungu'' sio vitu vinavyokubali kuwekwa kwenye argument aliyotaka anayotaka kuitengeneza mashana, ''Mung'' anakua defined kama ''a being....'' ila "akili" inakua defined kama "an ability"....
 
angetoa definition ya akili mada ingeishia hapo, maana angesema akili ni ''uwezo wa kupata, kuelewa na kutumia maarifa na taaluma'' sasa Kiranga angejibu kwa urahisi tu kwamba uwezo huo ninao, na Mshana Jr angebaki hana cha kusema. Hii argument aliyotaka kuileta Mashana ni ya kucheza na lugha na ni ya kitoto sana, it is obvious kwa watu wanao elewa lugha kwamaba ''akili'' na ''Mungu'' sio vitu vinavyokubali kuwekwa kwenye argument aliyotaka anayotaka kuitengeneza mashana, ''Mung'' anakua defined kama ''a being....'' ila "akili" inakua defined kama "an ability"....
Hii argument aliyotaka kuileta Mashana ni ya kucheza na lugha na ni ya kitoto sana [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]lakini imewafanya watu washindwe kuijibu kabisa... Karibu kwenye mjadala
BTW mimi sio Mashana mimi ni Mshana Jr
 
Watu wanakimbia maswali kwa trick za kitoto sana

Kuna kijamaa kimoja kinapenda kuzungumzia elimu kwenye kila post yake, ajabu ni kwamba anadai kua jiwe ni kiumbe hai
Hao flat earth society mimi nilishawablock siku nyingi.

Ukiendelea kujadiliana na mtu anayesema jiwe ni kiumbe hai unashusha chini viwango vya mjadala.

Si kila mtu anafaa kujadiliana naye, wengine wana matatizo ya kisaikolojia ukijadiliana nao sana unaweza kuambukizwa.
 
angetoa definition ya akili mada ingeishia hapo, maana angesema akili ni ''uwezo wa kupata, kuelewa na kutumia maarifa na taaluma'' sasa Kiranga angejibu kwa urahisi tu kwamba uwezo huo ninao, na Mshana Jr angebaki hana cha kusema. Hii argument aliyotaka kuileta Mashana ni ya kucheza na lugha na ni ya kitoto sana, it is obvious kwa watu wanao elewa lugha kwamaba ''akili'' na ''Mungu'' sio vitu vinavyokubali kuwekwa kwenye argument aliyotaka anayotaka kuitengeneza mashana, ''Mung'' anakua defined kama ''a being....'' ila "akili" inakua defined kama "an ability"....
Mshana kajaa logical non sequitur.
 
Thibitisha kwamba hakuna maisha baada ya kufa.
Kisichopo hakithibitishiki kwamba hakipo, kwa sababu hakipo, na nje ya mantiki, kama hakipo hakithibitishiki kwamba hakipo.

Ndiyo maana huwezi kupata alama za vidole (fingerprints) za mwizi ambaye hayupo, ili uthibitishe kwamba mwizi huyo hayupo. Kama hayupo, huwezi kupata alama za vidole vyake ili uthibitishe kwamba hayupo.

Kilichopo ndicho kinathibitishika kwamba kipo, kwa sababu kipo.

Ndiyo maana unaweza kupata alama za vidole za mwizi ambaye yupo.

Sasa wewe unasema mwizi yupo, mimi nasema huyu mwizi hayupo, ni hadithi tu.

Mimi nakwambia nipe alama za vidole, au video, au ushahidi wowote kwamba mwizi yupo.

Na wewe unaniambia nikupe alama za vidole au video kutoa ushahidi kwamba mwizi hayupo.

Sasa kama mwizi hayupo, alama zake za vidole nitatzitoa wapi ili nithibitishe kwamba hayupo? Na nikitoa alama za vidole vyake si tayari nakuwa nimethibitisha yupo?

Thibitisha kwamba kuna maisha baada ya kifo.

Mzigo wa uthibitisho unamuwia yule anayesema kitu kipo, si yule anayesema hakipo.

Anayesema hakipo anauliza kuhusu ushahidi na uthibitisho. Anayesema kipo ndiye anatakiwa kutoa uthibitisho.
 
Kama inawezekana, huoni kwamba kupitia mgongo huo unaweza kutengeneza uongo kua kitu kipo wakati hakipo na mimi nikakupinga kua hakipo bila hata kujua ukweli kua kipo???
Huwezi kutengeneza isipokuwa utaonekana tu wewe ni muongo na huna akili timamu.

Na kwakini utengeneze uongo ? Ili iweje na kwa manufaa ya nani ?
 
Umezaliwa maisha yako yote umemkuta samaki anaogelea, unaanzaje kuanza kumfundisha namna ya kuogelea???

Huwa nakariri mara kwa mara ya kuwa wewe hutumii akili na mifano yako huwa unakurupuka,mpaka unawaza kuhusu samaki na silika yake kisha unaleta kama mfano ni udhaifu mkubwa kwa kutokujua kuweka kitu mahala pake. Samaki yale ni maisha yake na huwezi kuukosoa mfumo wake. Lakini wewe ni dhaifu sana katika kujenga hoja na kutumia akili,ndio nakufundosha sasa.

Hapa nazungumza na wewe. Mfano wa samaki hapa si mahala pale.

Nakufundisha wewe ambae umekiri ya kuwa jumjuo Mungu lakini bado una mzungumzia na ujinga wako hauja anza kudhihiri leo bali tangu siku ya kwanza najadiliana na wewe.
 
Basi licha ya mungu kuumba binadamu na ulimwengu kiujumla vitu hivi vyote ni lazima viwe na chanzo ikiwemo na mungu mwenyewe.
Hapana! Kwanini? Kwa sababu kati ya binadamu, yeye akijitokeza bora zaidi, na viumbe vingine na ulimwengu, utaona na utakubali vimeumbwa. Hivyo hivi vitu ni viumbe na hivyo kuna muumba wake, ndio chanzo chao na ndio kikomo chao.
Huyu muumba wa hivi vitu, yeye ndie chanzo cha vitu hivi; kama yeye ndiye chanzo anawezaje kuwa na chanzo cha chanzo chake?
 
sawa lakini chanzo hicho kivipi kiwe ni mungu???
Ukitazama wewe binadamu uwezo wako wa akili: ufahamu, uelewa, kufanyakazi, mfumo wako, unyoofu wako na ukamilifu wako, utaona na kuelewa unatokana na chanzo chenye akili ya juu sana.
Hapo hapo tazama ulimwengu na viumbe vingine, hivi vyote havionekani kuwepo kwa bahati nasibu au mbaya, ni kwa mpangilio, unyoofu na kwa mfumo thabiti na kamilifu. Hii ni ajabu ya aina gani? Ni akili gani hii: ni nguvu gani hii iliyofanya hivi vitu kwa usahihi na ukamilifu huu, jinsi hii, akili hii ya juu kabisa, nguvu hii ya ajabu kabisa, ndio tunaiita Mungu.
 
Huwezi kutengeneza isipokuwa utaonekana tu wewe ni muongo na huna akili timamu.

Na kwakini utengeneze uongo ? Ili iweje na kwa manufaa ya nani ?
Ishu sio manufaa, uongo ukiwa na manufaa unabadilika kuwa ukweli??

Nimekuonesha namna ambavyo naweza kujua uongo wa kitu bila hata kujua ukweli halisi. Umeelewa??
 
Sasa hili inabidi uwaulize wanao mjua au wanao amini hilo.

Mimi jadili Uislamu na Qur'aan ndio nitakujibu ila hayo si yetu.
Mungu wako simjui kwasababu hayupo lakini na bado naweza kumjadiili kama yupo

Kwanini huamini invisible unicorn kua ni mungu??
 
Hapana! Kwanini? Kwa sababu kati ya binadamu, yeye akijitokeza bora zaidi, na viumbe vingine na ulimwengu, utaona na utakubali vimeumbwa. Hivyo hivi vitu ni viumbe na hivyo kuna muumba wake, ndio chanzo chao na ndio kikomo chao.
Huyu muumba wa hivi vitu, yeye ndie chanzo cha vitu hivi; kama yeye ndiye chanzo anawezaje kuwa na chanzo cha chanzo chake?
Kwanza kabisa, thibitisha Mungu yupo na kwamba habari za kuwapo kwake si hadithi tu.
 
Back
Top Bottom