Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Leta hapa tuuone

Unaenda benki kukopa halafu unasema wewe unanyumba ya kuweka dhamana hivyo wakupe mkopo bila kuonesha hati miliki halafu unashangaa kwanini unakataliwa?
Hapa ndio unachanganya mambo sasa
Dhamana na hati miliki ni paper work ya kuandika kuthibitisha umiliki ama kuweka kama dhamana... Huu ni utaratibu tu wa kisheria
 
Kivyovyote vile haimaanishi kilicho undwa/umbwa kiwe na chanzo halafu kilicho unda/umba kisiwe na chanzo

Yaani gorofa lililo undwa/umbwa liwe na mjenzi, halafu huyo mjenzi asiwe na chanzo????
Hapana usichanganye sana
Kuumba
Kuunda
Kujenga
Kutengeneza
Vyote hivi havifanani matokeo hata kama kimsingi asili ni moja ya kuleta kitu kipya... Ambacho hata hivyo ni upya wa sura/umbo tuu lakini si malighafi

 
Raisi wa tz namfahamu lakini babako simfahamu hivyo nimekuoneshea kua naweza nikapinga uongo huo hata kama simfahamu

Sio tu hivyo

Naweza hata nisimjue baba yako lakini ukiniambia anavichwa saba na miguu nane na anadamu yakijani nitakataa. Sitahitaji kuhoji kujua ushahidi wa vipimo vya kisayansi wala picha

Naweza nisimjue babako lakini haimaanishi kwamba ukiniambia alisha wahi kufa na akafufuka nikubali. Niatakataa bila hata kumjua kiundani baba yako

Ukiniambia wewe umezaliwa mwaka 1970 halafu baba yako mzazi kazaliwa 1992 nitajua huu ni uongo ilihali sijui umri sahihi kati yako na baba yako

Umeelewa???
 
Dhana ya UUMBAJI soma hapa hatua kwa hatua

 
Maswali yako yanaonyesha wewe mwenyewe hajajijua. Vipi ukianza kujiuliza: wewe ni nani? Kutoka hapo jitafiti.
wewe ushajiuliza hilo swali?? umehisi hilo swali ni la msingi?.kwangu mimi sio swali la msingi mimi ni mtu inatosha sana
 
Kweli kabisa mkuu!
Sahihi kabisa lakini pía ni ngumu kutafuta ithibati ya kimwili kwa kitu cha kiroho... Ni makosa makubwa kufanya hivyo kwakuwa ni vitu viwili tofauti kabisa lakini vyenye kuunganishwa pamoja kutengeneza kimoja
Ni kati ya hivyo viwili kimoja kinaonekana na kingine hakionekani... Kimoja kina ukomo na kingine hakina ukomo...
 
Unatambua vema kwamba, licha ya mwanadamu kufanya au kuumba magari, majumba na kadhalika, lakini hivi vyote vina chanzo chake ikiwemo na mwanadamu mwenyewe.

Kama binadamu kuumba magari, majumba na kadhalika lakini hivi vyote vina chanzo chake ikiwemo binadamu mwenyewe

Kwa principle hiyo hiyo

Basi licha ya mungu kuumba binadamu na ulimwengu kiujumla vitu hivi vyote ni lazima viwe na chanzo ikiwemo na mungu mwenyewe. Utakubali??

Hapa kwa hakika unaelewa vitu hivi vyote: ulimwengu na binadamu chanzo chake ni kimoja.

sawa lakini chanzo hicho kivipi kiwe ni mungu???

Mashaka yako ni, vipi vitu hivi viwe na chanzo, lakini chanzo kisiwe na chanzo?
mashaka zaidi ni kivipi kila kilichopo kisiwe na chanzo??
Chanzo ndio uwepo wenyewe
uwepo wa nini??
Ni nguvu ambayo imevifanya vitu hivi vyote: vinavyoonekana na visivyoonekana, pasipo kutumia kitu chochote (utupu) vikapata kuwepo.
umejuaje kwamba nguvu hiyo ipo?? Hiyo nguvu ilitoka wapi??? Na kivipi nguvu hiyo iwe mungu na sio kingine tofauti??? Wapi makazi yake kabla ya kusababisha viwepo vingine??? Kabla ya nguvu hiyo kufanya vingine viwepo hali ilikuweje kabla nguvu hiyo haijafanya kazi???

Hivi vitu kwa sababu vinatokana na nguvu fulani vina uwamo wa nguvu hiyo ndani yake.
naweza nikakubaliana nawewe kua ni nguvu fulani ambayo haijulikani vizuri lakini haimaanishi nayo haina chanzo au nguvu hiyo ni lazima iwe mungu

Ulimwengu na binadamu, uwepo wake ni, kwa njia ya nguvu hiyo.

Ni hivi ikiwa Kama uwepo wa magorofa, uwepo wake ni kwa njia ya binadamu. Na binadamu na ulimwengu uwepo wake umechangiwa kwa nguvu hiyo, je uwepo wa nguvu hiyo umechangiwa na njia ya kitu gani????

Hivyo ukimtazama, ukimchunguza: kumtafiti mwanadamu, unagundua anampangilio, mnyoofu na amefumika kiasi ambacho kuaribika kwa mfumo mmoja ndani yake huwa na madhara kwa mfumo mwingine.

hapana
Usitumie experience unayoiona kua ni bora kwasababu hujaona kinyume chake

Umejuaje kwamba mtu ana mpangilio mnyoofu?? Ikiwa kama tungezaliwa na race ya bluu ungepata wapi wazo la kusema kua binadamu angezaliwa kwa mpangilio tofauti na huu angekuwa bora zaidi???

Mpangilio mnyoofu uko wapi wakati watoto wanazaliwa na upungufu wa viungo??

Jinsi hii ya binadamu inakuwa ya kipekee ukilinganisha na viumbe wengine.
Vilevile utaona viumbe vingine vikiwa kamilifu, nyoofu na kwa mfumo uliyo wa ajabu.

Na vilevile utaona voumbe vikiwa havina ukamilifu wala unyoofu kwa mfumo unaopinga dhana ya unyoofu, kuonesha kua havija dzainiwa na kitu kisichokosea


Hivi ndivyo pia ilivyo kwa dunia: mpangilio wake, unyoofu wake, uzuri wake na mfumo wake, ni wa ajabu na wa kustajabisha!
Unajuaje hiki kimenyooka bila kujua kilichopinda???

Masunami pia nao yanakamilisha unyoofu wa dunia mbona hujayataja??

Unyoofu wa dunia uko wapi wakati watu wana suffer kwa matetemeko ya ardi ya sunani???

Hii yote "ya ulimwengu, binadamu, na viumbe vingine" jinsi yake, namna yake na ndani yake kila kimoja kinavyofanya kazi inatupa kufahamu kwamba, "NGUVU HII" Iliyovifanya Hivi Vitu ni, HAI, KAMILIFU na UPENDO, ni Mungu.

Kwanini nguvu hiyo iwe mungu???

Huwezi ukakuta ghorofa mahali bila hata kujua nani amelijenga unaanza kwa kusema kua haiwrzekani likawa limejijenga, basi kwasababu hiyo litakua limejengwa na mohhammed builders lmtd

Kivipi ghorofa hilo liwe limejengwa na mohamed builder na sio kampuni lingine???
 
wewe ushajiuliza hilo swali?? umehisi hilo swali ni la msingi?.kwangu mimi sio swali la msingi mimi ni mtu inatosha sana
Hapana kabisa wewe ni nafsi tatu ndani ya moja... Ikikosekana moja tu.. Utakoma kuwa huyo mtu
 
Nithibitie uwepo wa akili na roho nikuthibitishie uwepo wa Mungu
It sounds like

Nipe mkopo kwanza nikatumie kwenye shughuli zangu ndio nikuoneshe hati miliki ya nyumba yangu ambayo nitakupa kama dhamana
 
Hapana kabisa wewe ni nafsi tatu ndani ya moja... Ikikosekana moja tu.. Utakoma kuwa huyo mtu
Hiyo ni Kwa mujibu wako

Kuna mji uko japan unaitwa kumamotto, kibongo bongo ukisikika unaongea neno hilo watu watajua unatukana lakini ukiwa japani huo ni mji
 
It sounds like

Nipe mkopo kwanza nikatumie kwenye shughuli zangu ndio nikuoneshe hati miliki ya nyumba yangu ambayo nitakupa kama dhamana
Hapana kila kitu kina taratibu zake.... Kwenye sekta za fedha na mambo ya mikopo hakuna rivasi kama hiyo
 
Hiyo ni Kwa mujibu wako

Kuna mji uko japan unaitwa kumamotto, kibongo bongo ukisikika unaongea neno hilo watu watajua unatukana lakini ukiwa japani huo ni mji
Hapana hizi ni tamaduni tu kulingana na jiografia ya kidunia hasa kwenye mila na desturi... Hivi ni vitu vyepesi mno kwenye ulimwengu wa roho kwahiyo hatuwezi kuvitumia kama mfano
 
Raisi wa tz namfahamu lakini babako simfahamu hivyo nimekuoneshea kua naweza nikapinga uongo huo hata kama simfahamu

Sasa kwanini ulitolea mfano wa jambo ambalo liko wazi,wakati tunaongelea jambk ambalo hulijui vipi unawezaje kuujua uongo wake ?


Sasa usipate shida ndio utoe sasa mfano kama huo kwa mtu mabae humfahamu halafu ujue uongo wake uko wake.

Nataka unipe mfank kando kwa mtu usie mfahamu,unajuaje uongo wake,maana hapo kama mimk siwezi kusema baba angu ni raisi sababu raisi anajulikana,aidha nitakuwa nina matatizo ya akili,na mwenye matatizo ya akili ushahidi wake hauchukuliwi wala hoja zake hazifanyiwi kazi mpaka atakapo kuwa sawa.

Unatakiwa uwe unatuliza akili,sio unakurupuka.
 
unaweza kunitajia hizo nafsi tatu nizifahamu??
 
unaweza kunitajia hizo nafsi tatu nizifahamu??
Nimetangulia kukuwekea link mbili kwanza.. Lakini hizo nafsi 3 ni
Nafsi mwili
Nafsi roho
Nafsi jina (utambulisho)
Mwili unapoungana na roho ndio hupatikana wewe
 
Naweza hata nisimjue baba yako lakini ukiniambia anavichwa saba na miguu nane na anadamu yakijani nitakataa. Sitahitaji kuhoji kujua ushahidi wa vipimo vya kisayansi wala picha
Ukiwa unakurupuka hata unachokiandika unakuwa huelewi,nazungumzia jambo ambalo hulijui. Umbile la kawaida la binadamu linakulikana mzee na damu rangi yake inajulikana.

Haya yote yanajulikana,naongelea jambo na dhati yake,sasa unaposema kuhusu baba angu kwa dhati ya binadamu umbile linajuliakana.

Rudi kwa Mola ambae humjui kwa lolote wala huna marejeo yake,ngoja nikusaidie hapa naona umevamia hoja ndio maana unashindwa kuitetea mifano unayoitoa dhati yake inajulikana.

Tukiza kichwa,usiwe unakurupuka hapa utahangaika bure.
 
Sasa kwanini ulitolea mfano wa jambo ambalo liko wazi,wakati tunaongelea jambk ambalo hulijui vipi unawezaje kuujua uongo wake ?
nimetoa mfano kukuonesha katika mazingira yeyote ile unaweza ukapinga uongo wa kitu hata kama hujui ukweli wake, kwa kukutolea mfano huo na ile mingine ambayo umeikwepa kujadili


Sasa usipate shida ndio utoe sasa mfano kama huo kwa mtu mabae humfahamu halafu ujue uongo wake uko wake.
Shida unapata wewe kwa kudai mfano wakati nishakupa zaidi ya mmoja

Nataka unipe mfank kando kwa mtu usie mfahamu,unajuaje uongo wake,maana hapo kama mimk siwezi kusema baba angu ni raisi sababu raisi anajulikana,aidha nitakuwa nina matatizo ya akili,na mwenye matatizo ya akili ushahidi wake hauchukuliwi wala hoja zake hazifanyiwi kazi mpaka atakapo kuwa sawa.
mifano niliyokupa umeieleweje kwanza??

Unatakiwa uwe unatuliza akili,sio unakurupuka.
Nikituliza akili hatutaelewana, inawezekana wewe umetuliza akili ndiomana unarudia kuomba mifano niloyokupa. Umeona tatizo lipo kwa nani mpaka hapo?
 
Back
Top Bottom