Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Anayewayawaya nani sasa? Mara ngapi mimi na wewe tumejadili hili suala kujua na kuamini?
Tumekadili mara zote hizo kwa sababu hutaki kukubali kwamba unaamini usichojua.

Ndiyo maana huwezi juthibitisha Mungu yupo.
 
Tumekadili mara zote hizo kwa sababu hutaki kukubali kwamba unaamini usichojua.

Ndiyo maana huwezi juthibitisha Mungu yupo.
Kama mie naamini nisichokijua basi na wewe unapinga usichokijua,unapinga kuwepo kwa kitu ambacho hata haukijui.
 
kiranga kuna siku aliniuliza thibitisha kama Mungu na shetani wapo kweli?
duuh nilichoka sana nikasema kumbe kuna watu wa namna hii?

akanikumbusha historia ya mwanasayansi mmoja hivi aliyekuwa anamtafuta Mungu ili ajionee kwa macho...alianza safari ya kuzunguka dunia nzima sasa alifika mahari papo kimya sana alafu kuna bahari kubwa ila cha ajabu kulikuwa na mtoto mdogo kachimba kashimo kadogo pembezoni mwa bahari alaf ana kikopo mkononi anachota maji kwenye bahari anakuja kutia kwenye kale kashimo....mwanasayansi huyo alistaajabu sana kuona vile ikabidi amsogelee yule mtoto na maongezi yalikuwa hivi

mwanasayansi:we mtoto huku unaishi na nani mbona sioni watu wengine?

mtoto:niko pekeyangu

mwanasayansi😱oh ok sasa hapo unafanya nini?

mtoto:nataka hayo maji yote ya baharini niyajaze kwenye kashimo haka nilikochimba

mwanasayansi:we kweli hauna akili unafikiri hayo maji yote yatajaa kwenye kashimo hako?

mtoto:na wewe hauna akili unadhani unachokitafuta utakipata?

mwanasayansi alipigwa na butwaa kusikia hivyo mara kufumba na kufumbua yule mtoto alipotea tu kwa mazingira ya utata.....tangu siku hiyo yule mwanasayansi hakufuatilia tena habari za kumtafuta Mungu


ila binafsi napenda sana kiranga anavyotufanya tufikirie sana juu ya uwepo wa Mungu
huyo mwanasayansi anaitwa nani mkuu?
 
Kwanza kabisa, nataka ksema kwamba, mimi sina nia ya ku bughudhi watu wanaoamini Mungu, wanaoamini dini.

Nina kawaida ya kuandika vitu kwa nuance, kama huelewi, kunichanganya ni rahisi sana.

Narudia, sina tatizo na wanaoamini dini, wanaoamini Mungu.

Naelewa imani ni jambo la faragha, ni jambo la uamuzi wa mtu binafsi.

Na zaidi, nikiona watu wanaoamini Mungu na dini wanaonewa, wananyimwa haki yao hiyo ya kimsingi, nitawatetea.

Nitawatetea hata kwenye jambo nisilokubaliana nao, kuhusu wai kuabudu Mungu anbaye sikubali yupo. Kwa sababu kwangu mimi, uhuru wa kuabudu kwa watu wote ni kitu cha msingi kuliko kama wanachoabudu ni kweli au si kweli.

Hivi karibuni rais Kagame wa Rawanda alisema atapiga marufuku makanisa ywenye wachungaji wasio na degree. Nilishutumu kauli ile kwamba inaingikia uhuru wa kuabudu, na watu wanatakiwa wawe na uhuru wa kuabudu kanisa lolote wanalitaka bila vikwazo.

Ungawa sikubali Mungu yupo, natetea uhuru wa juabudu wa watu wanaoamini Mungu yupo.

Mimi napenda uhuru wa kuabudu. Katiba ya Tan,ania inatoa uhuru huu.

Naoenda sana "The Universal Declaration of Human Rights" iliyopitishwa December 10 1948. Hii ni document ya UN inayotoa uhuru wa juabudu, iki nradi watu wasiingikie uhuru wa wengine na kuvunja sheria.

Kwa hiyo, nataka nikuhakikishie, sinatatizo na mtu anayesema ana imani fulani.

Nina tatizo na mtu anayesema anajua ukweli huyo Mungu wake yupo.

Huyu sasa anakuwa kajitoa katika imani, kajiingiza katika fact.

Na akishajiingiza katika fact tu, kanipa ruhusa kumuhoji.

Kwa hiyo ukiniambia niamini ninavyotaka, mimi sitaki kuamini vyovyote, nataka kujua.

Na ukiniambia nikuache unavyoamini, watu wanaoamini sijawahi kutaka kuwagusa, nawagusa wanaosema wanajua Mungu yupo.

Ukisema unaamini tu, that is not so special kwangu. Unaruhusiwa kuamini chochote.

Ukisema unajua Mungu yupo kweli, hapo nakuomba uthibitisho.
UTHIBITISHO WA UWEPO WA MUNGU.
Mungu yupo kwa wanaoamini. Wewe kama huna hiyo IMANI, siyo rahisi kuuona uwepo wake [hapa hatuna deni](period)

Wanaoabudu ng'ombe na wanyama wengine, wanakiona wanachokiabudu. Nenda ukawaulize ni kwa jinsi gani 'huyo' wanayemwabudu anajibu 'maombi' yao! Kisha omba uthibitisho. Ukipewa uthibitisho wa jinsi wanavyojibiwa 'maombi' yao (nje ya imani) karibu tena mezani tujadili.

Unajua Simba ni mnyama wa porini ambae ni hatari sana. Eagle ni ndege mkubwa mwenye nguvu na vipawa vya pekee miongopi mwa viumbe vya jamii yake. Ukitaka kuwapambanisha fahari hawa wawili ili umpate 'A stand-out winner' kati yao (to be fair) utalazimika utafute 'fair ground' kwaajili ya 'Pambano'...usimpeleke Simba angani akapambane na Eagle, atapigwa, kwasababu mazingira siyo rafiki kwake (fairly). Usimpeleke Eagle porini akapigane na Simba, atachakazwa vibaya mno, kwasababu mazingira siyo rafiki kwake (fairly). Swali ni mazingira gani yatakua 'fair ground' kwa miamba hii miaili kupambana ili mshindi apatikane fairly?!

Now, kwakua wewe bwana #Kiranga ni (Simba) na watu wanoamini uwepo wa Mungu ( Mi ntawaita Eagle, for the sake of this case) ili watu wa kiroho/kiimani (spiritual folks) waweze kukuelezea wewe uwepo aa Mungu, naomba utafute 'fair ground' ya discussion(pambano) ili mshindi apatikane on a fair basis! Ukwel usipingika ni kwamba #Kiranga you're not spiritual, why are you demanding the proof of a Spiritual feature (God)?! Be fair, mtu wa kiroho aki claim uwepo wa Mungu, assume kwamba haongei na wewe because you aren't into their profile! And apparently, they may not be into your profile either!

EXTRA
Kwavile CONTRADICTIONS ndizo zinakufanya u question uwepo wa Mungu, na unaamini pia kua Uwepo wa Mungu upo tu by CONTRADICTION, kwa kutumia maswali haya hapa chini naomba uondoe contradictions unazoziona kwenye holly books ulizozipitia...

1. Assuming umepewa nafasi ya kumchagua your 'Ideal God'...angekua na sifa gani?!

2. Assuming wewe ni Engineer mkuu na CEO wa kampuni kubwa inayomiliki viwanda vya utengenezaj wa robots na kuuza robots hapa duniani, what will be the essential features of your creation.
(essential feature of God's creation is a 'will'-your will which place at hand even the ability of choosing against God who gave u the will-Mungu hakutaka uwe robot-hakutaka aku programme ili uishi (kwa lazma) in accordance with His will.
 
Kwa hiyo na wewe unataka kuwafuata babu zako eeeh. Wafuate tuuu.. Aadhibiwi mtu kabla ajaletewa ujumbe. We we ujumbe umeletewa na unatumia nguvu nyingu kuupinga. Sasa nakwambia endelea hivyo hivyo mwisho wake utaujua. Uzuri Mimi na we we tutakufa upende usipende hakuna atakae Baki milele.

Hawa wanafuata mababu mkuu, ni wakuwaonea huruma wallahi, wamepotea.
 
Hajaelewa swali na wewe huna hata utashi wa kuuliza sehemu ambayo hajaelewa ni wapi mueleweshwe.
Mkuu AKILI ZAKO HAZINA AKILI.

We utafuti unachikitaka bali unatafuta ubishani usioo na tija na wewe huwezi kufaulu na hii kutokana na unavyojiona kuwa kichwa wakati ndani yake hakuna kitu.
 
Unaelewa kwamba hata hujaelewa swali nililouliza, na hivyo hujaweza kulijibu.

Umejibu kitu tofauti kabisa.

Unaelewa hilo?
Angalia swali lako ulilouliza alaf unambie kuna maswali mangapi uliyoyajenga katika sentensi moja. Ngoja nikufundishe kiswahili mkuu.
 
Mkuu Mi na upagani mbali mbali. Mi ni Muslim.


Kama kweli ww muislam kwanini unazidi kumpoteza mwenzio Mshana maana unamsifia kwa ujinga wakati ataingia Jehanam KHALIDIINA FIHA ABADA ameshakuwa addicted na uchawi

Huoni hiyo jehanam unayoitaja mwenzako ndio inamngoja kwanini usimshauri halafu unamuona Kiranga ndio ataingia jehanam wakati Kiranga yupo ktk haki ya kutaka kujua habari za kweli

Unajua uchawi kauleta nani?
 
Huyu ni Muislamu safi na sio mpagani kama unavyofikiria, na ukitaka kujuwa kuwa huyu ni muislamu fuatilia comments zake no zenye kueleweka na ushahidi kamili.


Hawezi kuwa muislam safi anamsifia mtu anayefundisha watu uchawi

Unaweza kuniambia asili ya uchawi ni upi ili uone nani aliyeleta uchawi duniani?
 
Kama kweli ww muislam kwanini unazidi kumpoteza mwenzio Mshana maana unamsifia kwa ujinga wakati ataingia Jehanam KHALIDIINA FIHA ABADA ameshakuwa addicted na uchawi

Huoni hiyo jehanam unayoitaja mwenzako ndio inamngoja kwanini usimshauri halafu unamuona Kiranga ndio ataingia jehanam wakati Kiranga yupo ktk haki ya kutaka kujua habari za kweli

Unajua uchawi kauleta nani?
Yaani ukimchukua Kiranga na mbwa. Mwenye thamani apo ni mbwa Huyo mwengine hana thamani kabisa.

Yaaani unamfananisha mshana na huyu mkosefu.


Mku huyu kiumbe kapewa macho, masikio, Akili lakini kashindwa kutanabai uwepo wa muumba.

Anashindwa kuelewa kuwa yeye katokana na maji dhaifu kabisa tena yenye kuchupa, akakalishwa kwenye tumbo la mama yake na siku ya kutoka akatoka kupitia sehemu za siri zinazofichwa kwa nguvu zote.

Huyu mtu hata neema ya pumzi hajaiyona na bado anaitumia kupoteza watu hapa kwa ubishi wake.

Na akiendelea hivyoo atayazomba mazambi ya kuwapoteza watu na yake na mafikio yatakuwa ni motonii.
 
Kama mie naamini nisichokijua basi na wewe unapinga usichokijua,unapinga kuwepo kwa kitu ambacho hata haukijui.
Nisichokijua ni nini?

Na unajuaje unachosema sikijui, ni kweli kipo na sikujui, kwa sababu ya mapungufu yangu tu, na si kwamba hakipo na siwezi kukijua, kwa sababu hakipo ili kijulikane.

Unaweza kuthibitisha unachosema sikijui kipo at all?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Hakuna mmoja wa wanaosema Mungu yupo aliyeweza kuthibitisha Mungu yupo.

Kwa nini?

Nikikwambia ni kwa sababu Mungu hayupo, utajibu vipi?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
 
Yaani ukimchukua Kiranga na mbwa. Mwenye thamani apo ni mbwa Huyo mwengine hana thamani kabisa.

Yaaani unamfananisha mshana na huyu mkosefu.


Mku huyu kiumbe kapewa macho, masikio, Akili lakini kashindwa kutanabai uwepo wa muumba.

Anashindwa kuelewa kuwa yeye katokana na maji dhaifu kabisa tena yenye kuchupa, akakalishwa kwenye tumbo la mama yake na siku ya kutoka akatoka kupitia sehemu za siri zinazofichwa kwa nguvu zote.

Huyu mtu hata neema ya pumzi hajaiyona na bado anaitumia kupoteza watu hapa kwa ubishi wake.

Na akiendelea hivyoo atayazomba mazambi ya kuwapoteza watu na yake na mafikio yatakuwa ni motonii.
Unaelewa kwamba ulimwengu ambao kiumbe kimoja kinaweza kuwa na thamani zaidi ya kingine unaonesha kwamba hakuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote?

Unaelewa kwamba ulimwengu ambao mtu ana uwezo na thamani zaidi ya mbwa unatuhuzunisha watu wengine wenye fikra kubwa ambao tungetaka mbwa wote wawe na uwezo wa kufikiri sawa na watu?
 
Back
Top Bottom