Katika muktadha huo tujiulize kwanza law ni nini?
Law a statement of fact, deduced from observation, to the effect that a particular natural or scientific phenomenon always occurs if certain conditions are present.
kisha tuitazame hiyo second law of thermodynamics inasema nini
Thermodynamics states that "in all energy exchanges, if no energy enters or leaves the system, the potential energy of the state will always be less than that of the initial state."
ukitafakari utaona kuwa hiyo law ni utaratibu au kanuni fulani ambayo imekubalika kisayansi ikielezea hayo mambo ya energy exchange. Sasa tujiulize huo utaratibu ulitokea tu? Hakuna nguvu (Mungu) fulani ambayo imeweka hiyo law (utaratibu au kanuni) ili uhai uwezekane? Hufikiri kwamba huenda kuna nguvu (Mungu) yenye uwezo wa kufanya huo utaratibu uwepo? Yaani Mungu alitumia hiyo mechanism katika uumbaji?
Kwa nini unaruka kutoka nguvu na kulazimisha hiyo nguvu kuwa Mungu? Kwa nini unaiita nguvu "alitumia" kama nguvu ina nafsi?
Kwa nini unalazimisha kuiita nguvu Mungu kabla hujaichunguza na kuijua vizuri, wakati unaweza kuichunguza na kujua zaidi?
Umeme ni nguvu, unaweza kusema "umeme aliwasha taa?". Hicho ni Kiswahili au Kijaluo?
Kwa nini unalazimisha nguvu iwe Mungu hata kabla hujaijua hiyo nguvu vizuri?
Zaidi, Mungu ninayemuanzia hapa ni Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote. Unajiridhishaje hiyo nguvu si Mungu tu, bali ni Mungu mwenye sifa hizo?
Kiranga kwanini unajiminya katika mawanda ya kufikiri na unataka kuishia kwenye law peke yake pasipo kujiongeza hata kidogo tu?
Wapi nimejiminya katika law pekee? Unajua kusoma? Unaweza kunipa nukuu nilipojiminya katika law pekee?
Yaan unataka kusema law ndiyo chanzo cha uhai
Kiranga kweli!?
Wwapi nimesema hilo? Hivi wewe una brain capacity ya ku explore a hypothetical proposition without the misconception of making that hypothetical proposition as a statement of categorical unmitigated worldview?
Unaelewa tofauti ya vitu viwili hivi?
Unaelewa tofauti ya hypothetical proposition for the sake of exploring an idea on the one hand from a statement of categorical unmitigated worldview?
Unaelewa kwamba unapojadiliana na mimi kila neno lina uzito na umuhimu wake, na ukikosa kuelewa neno moja tu, unaweza kukosa kuelewa maana ya post au thread nzima?
Unaelewa kwamba wewe ushafanya kosa hili na huelewi kwamba nikikwambia "if the flat earth society is right, then the antipodes are not the antipodes" sijakuambia the flat earth society is right?
Ninachosema hapa huu uhai wetu na kila kitu kilichopo kina chanzo (Mungu) chake ambacho uwezo wetu kama binaadamu bado haujafika katika viwango vya kukielezea vizuri pasipo contradiction zozote. Mapungufu yaliyopo katika hizi imani haimaanishi kuwa Mungu hayupo ila Mungu anayeelezewa katika hizi imani hayupo maana anaji contradict sana.
Unaelewa kwamba habari nzima ya "chanzo" ni kilema kinachotokana na umasikini wetu wa asili wa kuwa katika uwiano wa kati katika ulimwengu?
Unaelewa kwamba ukizama kwa kina sana katika misingi ya ulimwengu huu, muda haupo, muda ni kitu tunachokiona hapa juu juu tu kwa uwiano wa kitu kimoja na kingine (msome Einstein katika Relativity), na kama huko chini kabisa kwenye fizikia ya kwanta, muda haupo, suala zima la "chanzo hiki kimeleta hili" halipo?
Unaelewa hayo?