Mzito Kabwela
Platinum Member
- Nov 28, 2009
- 18,904
- 7,746
Mfumo dume utachelewa sana kufutika Tanzania! Kama mijitu ndo inachangia hivi!! Dah!
Alimaliza darasa la saba na yeye alishasema kuwa elimu si muhimu katika maisha (Bofya). Tulipinga sana wakati ule ingawa na sie ni FFF (Form Four Failure) lakini tunahusudu shule ni bahati mbaya. Tusitetee udhaifu wetuAnayefahamu elimu yake aniambie.
Ninaweza kumlaumu bure wakati elimu yake ni ndogo.
Elimu ya JOYCE KIRIA ni darasa la saba (7).
Historia inaonyesha kwamba aliwahi kuolewa kwanza na mume mwingine tena kwa ndoa kabla hajaolewa tena na kufunga tena ndoa na huyu HENRY KILEO.
Joyce Kilia yupo wazi sana aliwahi kusema kabla hajawa na mpenzi wake wa sasa alishakuwa na wanaume(boyfreinds)12,nilishangaa sana kwani wanawake wengi huwa hawasemi background zao
Aliolewa na Dj Nelly then wakaachana
Mleta mada ana wivu wa kike!
Unashangaa pamoja na kwamba mwendesha kipindi Ana elimu ndogo ya darasa la saba na pamoja na history yake isiyovutia ya kupitia magumu,lakini ameweza kuwazidi nyie mlomaliza vyuo na masters na p.h.d zenu!
Acha wivu,UTAKUUA!
kaka Pasco wewe ndo yule mwandishi paschal mayalla? Yule anayependa kutembelea Boda boda yake? Yule alikuwa mwandishi baadae akasoma sheria pale Mlimani? Yule Swahiba wa Zitto? Yule wa Bonafide genuine?Mimi niliwahi kuendesha talk show enzi zangu, na kiukweli kati ya wanawake wote wanaoendesha talk show, huyu ni mmoja ambao namkubali sana ila ukweli unabaki ni ukweli ni lazima ajielimishe zaidi.
Wewe unakuja na hizi shutuma ebu naomba tuangalie kati ya vipindi hivi ni kipi ambacho kimeweza kutoa msaada kwa jamii .......
........ Ukiangalia katika vipindi hivi ambavyo vinaongozwa na wanawake ukipima utaona kabisa hiki kipindi cha Wanawake Live kimejikita zaidi ndani ya yamii na hasa kumkomboa mwanamke kama kinavyojieleza kwani tumeweza kuona maeneo mbalimbali kama vile ndoa za utotoni, manyanyaso ya wanawake na hata manyanyaso ya watoto katika familia kwa hiyo kinatoa elimu tofauti na hivi vingene vya kuonyesha umaarufu tu na matumizi ya fedha ambazo hata hazijulikani wanazitoa wapi mwisho wa siku tutasikia na wao wamekamatwa na sembe huko China wanakoenda kila mara.
Pia hiki kipindi huwa hakifuati sheria na maadili ya habari!! Kuonesha sura ya mwanamke au
mtoto aliyenyanyasika kijinsia si sawa, kuna mama mmoja alibakwa alikuwa anahojiwa na Joyce bila hata kuficha sura, kuna yule aliyekatwa mkono na mumewe pia vivyo hivyo!! Lakini kubwa zaidi kuna siku alikuwa anakahoji katoto ka kike kamenyanyaswa kijinsia wazi wazi bila kumficha sura wala nini.
Sijajua kama yupo juu ya sheria au?? Na TCRA unawatumia taarifa wala hakuna action yoyote inayochukuliwa!! Ngoja tuone mwisho wake kama kitakuwa na matokeo mazuri kwa jamii kama anvyofikiria!!
Hapana, mimi ni Pasco wa jf!, ila yule yeye pia yumo humu jf kwa majina yake kamili na ni verified user!.
No wonder hii mada imeletwa na mwanamke, maana nimeskia adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake. Kwahiyo katika talk show zote ya Joyce ndio ina lugha kali??? Badala ya kumtia moyo mwanamke mwenzio, based on her past history na elimu yake anajitahidi sana. Wanawake acheni hizo!!!
mimi kwakweli sijawahi kuangalia hicho kipindi kwa hiyo ngoja ni kae kimya ila kama ana tabia ya kuwafundisha kiburi wake zetu aache mara moja.