Kipindi cha 'Wanawake Live' na madhara yake

Dada Joyce ni jeeeeembe.........Amethubutu na Ameweza.....Oprah said"With D's(Diplomas,Degrees)or NO D's....You Can Be Who You Want To Be In Life................"
,,,,,People Will Always Have Something To Say But Who Cares?
Bury 'Em Haters With Success Mom........

Na wewe umevurugwa??
 
Kwanza kaolewa? Na je yupo hapa jukwaani!!! Kuna wanawake ambao ni umiza kichwa...na hamna mwanaume anaeza kaa nae..sasa usijekuta na huyu nae yumo humo na anmalizia hasira kwenye kipindi!!

hajaolewa mkuu yeye ndio amemuoa jamaa mmoja wa chadema anaitwa henry kilewo nasikia jamaa ndio analishwa na kufanya kazi zote za ndani kama hausigelo
 
Elimu yangu ni std7, nilikuwa Housegirl zamani.

Ni Historia ambayo siionei Haya hata kidogo.

Wasomi wengi wanalalamika pamoja na PHD zao. Tumia historia yangu Joyce Kiria kutafakari umeifanyia nini nchi yako.

Kama we ni msafi chukua Mawe unirushie...


Bravo joyce! Umefanikiwa na ni mfano wa kuigwa kwa kufikia hapo! Kaza buti usiyumbe endelea kuboresha kipindi.
Je mnaweka vipindi vyenu online au you tube ili tulio mbali tuweze kufuatilia?? Asante.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
[h=1]Joyce Kiwia joycekiwia: Fun, outgoing, very motivated, love making money (kinda hate people who don't) & great believer in God!!![/h]
 
Last edited by a moderator:
Mtoa post huna lolote!, una wivu wewe. Kabla hujapost humu ndani ulishawahi kumshauri!?, alikujibu nini? Ndio maana mwishoni mwa tv programs nyng huwekwa contacts kwa ushauri, maswali n.k., ulishawah kuzi2mia? Jitumeni kufanya kazi, acheni wivu wa kike huo..
 
Kijana juzi hujui kuwa ukimuelimisha mwanamke umeelimisha jamaa jitazame vizuri mawazo wanawake wana upeo mkubwa kuliko wanaume kwenye asilimia kubwa ya mafanikio ya wanaume lazima atakuwa mwanamke bora kachangia usitukane wanawake wote mama yake alivyokuzaa na kukulea angekuwa mburumatange usingedika hapo ulipo mheshimu mwanamke

Nahisi umenichanganya mkuu, niombe radhi!! Post zangu zote soma vizuri hakuna nilipokashfu au kutoa lugha yoyote mbaya kwa wanawake!

Hebu hakikisha uliyetaka kumjibu ni nani, mimi au mwingine???
 
Kwa ushauri tu joyce jaribu kupata kakozi ka sycology ili uweze kuwasoma vizuri na kufikisha ujumbe msimvunje nguvu darasa la saba sio mwisho wa upeo ajiendeleze tu

Off Topic: Hapo kwenye red na bold, hiyo ni elimu gani?? Inatolewa wapi na sie tukaipate??
 
Ni kweli, aliwahi kutoa historia ya maisha yake, yeye ni Standard Seven leaver, alikuja mjini Dar kama "tx" namwanzo aliolewa na DJ!.

Nawaombeni sana nikiri wazi kuwa huyu dada anastahili pongezi, incouragement na kusaidiwa ili awe bora zaidi!. Kwa mtu wa darasa la saba kufika pale alipo, ni hatua na inahitaji hard work kujituma na kupambana!.

Katika kile kipindi chake cha ushuhuda ameeleza amejiendeleza kwa masomo ya jioni, na kwa sasa amepumzika kidogo ili kwanza kujenga familia, atataendelea mpaka kufika chuo kikuu na wale wahadhiri wanawake wa UDSM wamekubali kumsaidia kutimiza ndoto yake!.

Mimi niliwahi kuendesha talk show enzi zangu, na kiukweli kati ya wanawake wote wanaoendesha talk show, huyu ni mmoja ambao namkubali sana ila ukweli unabaki ni ukweli ni lazima ajielimishe zaidi.

Mpaka sasa tuna wanawake zaidi ya 20 bongo wanaoendesha vipindi vya talk show lakini vingi havina impact kama wanawake live!. Hawa ni baadhi yao.
  1. Joyce Kiria-Wanawake Live
  2. Salama Jabir-Mikasi
  3. Zamaradi Mketema-Bongo Movies
  4. Hoyce Temu-Tanzania yetu
  5. Sphora Mushi-Sphora Show
  6. Mboni Mhita-The Mboni Show
  7. Judith Wambura-Diary ya Lady JD
  8. Kanky Mwaigomole-Daladala Show
  9. Wema Sepetu- My shoes
  10. Christina Manongi-Sintah-Wedding Lounge
  11. Mayrose Kavura-The Mayrose Show
  12. Amabulis Batamula -Fema TV Talk Show
  13. Elizabeth Shirima-Mapishi
  14. Irene Uwoya-Paradise
  15. Shamim -Sherehe yetu
  16. Rose Ndauka-The Family Talk Show
  17. Kuna mmama mtu mzima anaendesha talk show fulani mpya TBC
  18. Kuna yule dada anaendesha kipindi cha wanawake ITV
  19. Kuna yule dada anaendesha kipindi cha EATV
  20. Kuna yule dada wa Star TV anaendsha talk show ya bongo beat
Happy New Year
Paskali
Rejea
P
 
Hahaha elimu gani mnayoizungumzia jamani?! Huyo dada mlitaka awe na elimu ipi ili aweze kuendesha hicho kipindi?! Hii elimu inayowafundisha watoto eti mother ni Momy na Father ni Daddy?! Hahaha mnamuonea bure kumtaka awe na elimu, hii elimu ninayoiona kwenye madaftari haitamsaidia huyo Joyce Kiria. Mgesema awe na busara lakini siyo elimu.
Hivi ni mtangazaji gani wa kituo gani anayetumia elimu kutangaza?! Hahaha siku hizi wanauza sura hakuna cha elimu studioni.
Mimi nimewahi kumuangalia mtangazaji kamualika mtu kumuhoji, lakini kipindi kizima mtangazaji ndiye alikuwa anaongea yani hadi mwisho wa kipindi nilibaki nashangaa ni nini kilitokea alafu akasema eti tukutane siku nyingine.
Hakuna elimu ya kutangazia ni bora mkono uende kinywani.
Hahaha eti hana elimu, hii elimu hii msinivunje mbavu.
 
Katika television zetu pamekuwa na utitiri wa uanzishwaji wa vipindi vyenye kuongozwa na watu binafsi Mfano Jenerali on Monday, This week in perspective, je tutafika, mimi na tanzania-Hoyce Temu, Diary ya Lady Jay Dee, Wema Sepetu in My Shoes, WANAWAKE LIVE-CHA JOYCE KIWIA Kileo na vingine.

Uanzishwaji wa vipindi hivi sijui unazingatia nini lakini kipindi cha wanawake live ni kipindi Muhimu hasa ambapo wanawake tunahitaji usawa na wanaume lakini SI kuwa sawa., ni kipindi sensitive kinachohitaji mwongozaji makini pengine mwenye uelewa wa hali ya juu ya Gender, Sociology, Sheria, Pschology n.k mi sijui Joyce Kiwia ana elimu gani maana hiki kipindi kitageuka janga siku sio nyingi. Anatumia maneno makali kwa wanaume mf Aliwahi kumwambia mzee mmoja "mbebe mkeo kama ulivyokuwa unamtongoza"! ha-balance story (kusikiliza pande mbili) yeye anahukumu tu.

Lakini anaongea na mambo ambayo yanaweza kusababisha chuki kwenye familia hasa ambazo hazina uwezo wa kuchambua mambo vizuri na ndoa zitavunjika na kusambaratika nyingi. Lakini baadae itaathiri hata siasa za Henry Kilewo negatively kama mambo hayatabadilika.

Wanawawake tunahitaji utetezi bila kuathiri ndoa zetu au kudhalilisha waume zetu.

sijawai kuona likes nyingi jf kama izii itakua ni kweli ila cc wanaume tumekaa vyema nyie mazoa zoa-watu na kazi zao -et waamasishaji ukifika nyumbani mashavu ya mekuvimba et umetoka wanawake live-elmu ya mapenzi ina utofauti na mafunzo mchwara tunayo peana vichochoroni-
na ndo maana manyakanganga wengi ndoa uwashinda
 
Katika kubadili chanel za TV yangu kuna siku huwa najikuta nimeweka hiki kipindi kiukweli huyu dada anawafundisha vibaya sana wanawake hasa kutowatii waume zao yaan mumeo akikutuma amekunyanyasa huyu Dada ni janga sidhani kama kichwani kuna kitu.
hii ina ukweli wowote??
 
kaka Pasco wewe ndo yule mwandishi paschal mayalla? Yule anayependa kutembelea Boda boda yake? Yule alikuwa mwandishi baadae akasoma sheria pale Mlimani? Yule Swahiba wa Zitto? Yule wa Bonafide genuine?
kaka Pasco wewe ndo yule mwandishi paschal mayalla? Yule anayependa kutembelea Boda boda yake? Yule alikuwa mwandishi baadae akasoma sheria pale Mlimani? Yule Swahiba wa Zitto? Yule wa Bonafide genuine?
Duh...!.
Kumbe....
P
 
Back
Top Bottom