Kipindi cha 'Wanawake Live' na madhara yake

Kipindi cha 'Wanawake Live' na madhara yake

Joice analazimisha watu wote wasifanye sherehe za harusi eti ni anasa eti oooh watu wanacheza kwaito wanakunywa kama yeye hapendi asilazimishe na wengine wawe kama yeye!, alafu anakuwa mkali na kuwaona wanaofanya sherehe hizo ni wajinga yeye ndio mjanja zaidi! Pia anawafundisha wanawake wawe na kiburi kwa waume zao. Kweli inabidi abadirike

Hapana, halazimishi tatizo linarudi pale pale kuwa anashindwa kucheza na lugha na mazingira!! Watanzania wengi tuna lugha fulani ya kubembeleza zaidi (nimeshindwa kupata neno moja hapa) ila mfano mzuri ni kwamba Mtanzania akienda dukani kununua kitu badala ya kusema 'nipe' atasema 'naomba' as if anapewa bure!!! Nahisi utakuwa umenielewa mpaka hapo.

Back to the point, Joyce Kiria amegundua tatizo kubwa sana kwenye jamii yetu na tunapaswa kumuunga mkono kwa kila hali, watu wangapi wanaomba misaada kwenda kutibiwa kwa gharama za shilingi milioni moja tu lakini katika mtaa/jumuiya au ukoo huo huo wakati huo huo kuna mtu unakuta anafunga harusi yenye kugharimu milioni 30 tena kwa kuchangisha!! Kwa nini nafasi kubwa ya kuchangiwa asipewe huyu mgonjwa anayepigania uhai wake?? Ni hoja ya msingi sana isipokuwa lugha anayotumia Joyce Kiria kushawishi watu kuacha kutumia fedha nyingi kwenye sherehe na kutumia fedha nyingi kwenye matatizo ya kijamii ndiyo inayomfanya aeleweke vibaya kama wewe Yusuphsabury ulivyomuelewa.

Kama nilivyosema, Watanzania tuna lugha yetu ingawa kuna baadhi ya makabila wako tofauti kidogo kama Wachaga na Wakurya na ndiyo maana makabila haya watu wengi hudhani kuwa wanapenda sana ubabe ubabe lakini kumbe sivyo, wao hiyo ndiyo ongea yao ya kawaida kabisa!


Hivyo basi, kazi ya Joyce Kiria ingekuwa nyepesi sana kama angefuata matumizi ya lugha yetu ambayo ni ya kama kubembeleza hivi!!! Joyce ameathiriwa na lugha mama ambapo kwa watu wa pembeni ya mlima Kilimanjaro huwa hawana sana lugha ya kushawishi kwa kubembeleza (nahisi ni sababu ya kuwa karibu na Kenya).

Na hii ndiyo inayosababisha alaumiwe na wengi humu kwa kuongea na yule baba lugha fulani hivi ya ukali kuwa ambebe mkewe. Ile kwake anaona ni sawa kabisa, lakini hadhira yake inasemaje juu ya swala lile?? Hasa ukizingatia alikuwa anaongea na mtu mzima, si heshima kuongea nae maneno kama yale.

Kikubwa anachotakiwa kufanya ni kusoma mazingira ya anaowafikishia ujumbe yakoje? Atumie lugha gani kuwafanya watu wamuelewe hasa ukizingatia kuwa kipindi chake kinahusu sana maswala ya mahusiano.

Wengi watabisha lakini ukweli utabaki pale pale, presenter unaposhindwa kueleweka kwenye jamii husika ujue umefeli!! Kama unamwambia mwanaume ambebe mkewe ikiwa ni njia ya kurudisha upendo lakini ukawa umetumia lugha ambayo jamii imeelewa kuwa umemnyanyasa mwanaume ni wazi kuwa umefeli!!!

Ukifeli kutumia media kushawishi jamii, ni dhahiri kipindi chako kitafeli pia!! Marekebisho ni muhimu sana

cc:Ntakasi
 
Kama kweli Wachangiaji tunalo lengo Chanya kuona kuwa mabadiliko yanapatikana katika jamii kama lengo na muelekeo wa kipindi cha JOYCE unavyotuelekeza naona, Mtoa Mada na sisi Wachangiaji tungejikita katika kutoa hoja ama kukosoa hoja zake juu ya uendeshaji wa kipindi.
Sisi kama walaji wa habari zake ni haki na Wajibu wetu kulifanya hilo.
Na si kuanza kushambulia personality ya muendeshaji kipindi kama baadhi wanavyofanya.
**Tuongee issues SIO Personality vinginevyo tutakuwa hatujengi.

-Na hatujui pengine wengine wanaweza kuwa wanaendeshwa na maugomvi yao huko Uswahilini na kuona pengine hii ndio njia nzuri na nafasi ya kuchafuana (Huu ni mtazamo wangu baada ya kupitia baadhi ya michango yenye kila dalili hizo)

HATA HIVYO, Kwakuwa wengine wameshavunja 'Mwiko' wa Staha na Ustaarabu na kuanza kumshambulia Mdada wa watu,
Kwa kuweka hoja za Chekechea zisizofaa hata kwa kuripea nalazimika kujivisha Bomu kuwajibu.

Note: Simjui na wala yeye Hanijui huyo mdada. Kwa hivyo silifanyi hili kwa maslahi yangu binafsi.

1.ELIMU-Ni kweli kuwa kuyaelezea, ama kuyafafanua vyema,kutafuta ufumbuzi,kushauri ama kushughulika nayo kwa ujumla baadhi ya mambo hasa yanayoihusu jamii moja kwa moja ni muhimu Mhusika kuwa ni Mbobezi kwenye eneo husika.
Lakini pia, Unaweza ukawa umebobea (Una elimu husika)katika eneo hilo ukawa pia huna uwezo wa kuliwakilisha ama kulitangaza kwenye jamii (Utangazaji)Kama joyce anavyofanya na ndio maana kwenye vipindi vingi hao Wataalam huwa wanaaalikwa ikibidi na wakihitajika.
Haiyumkiniki pia kuwa eti, Joy anaendesha hivyo vipindi bila kufuata ama kuongozwa na Utaalam, ama uzoefu kutoka kwa watu wenye ufahamu mzuri wa mambo hayo pia.

Tufahamu pia kuwa, Hivi vipindi vinarushwa kwenye Vyombo ambavyo vipo kihalali (yaani TV) ambazo zinaendeshwa kwa kufuata miiko na maadili na pia vina wasimamizi wake pia nje ya vyombo hivyo pia.
Sasa kama binadamu anaweza akawa na makosa yake madogomadogo simtetei Lakini,
Tujiulize chombo kinachomsimamia (Kinachorusha kipindi chake) Kiko wapi kwenye ukumbi wa lawama hizi?
Kwa nini lawama zimuangukie yeye peke yake?
Vipi kuhusu mamlaka zinazosimamia chombo ambacho yeye anatumia kuwakilisha ujumbe wakekwa walaji na wao vipi?

Inabidi ujiulize maswali mengi kabla ya kumshambulia mtu-Kama wewe ni mtu makini lakini...

***Eti kasoma Kaishia.....
Maana yake nini hii?? UTUMBO ULIO OZA.(Bure kabisa)

Ingekuwa hivyo basi vipindi vyote vingekuwa vinaendeshwa na-Maprofesa,

Kwa Ushauri tu:
Kama wewe unayo Masters yako huzuiliwi kuanzisha kipindi chako mwenyewe ili tuuone uweledi wako.

Vinginevyo haya ni MAJUNGU ya KITOTO yenye HOJA LEGEVU zinazopumulia Mipira miaka nenda rudi.
Na yana kila dalili ya chagizo za chuki binafsi

2.Haya, Hoja ya eti 'aliwahi kuolewa' na sasa... Upuuzi-Sihitaji hata kupoteza wino wangu.

Nawakilisha.
 
mpatie maoni yenu atayafanyia kazi msirumbane,nobody is perfect
 
Ahsanteni wachangiaji pamoja naDa Joyce Kiria mwenyewe; kwanza nimwombe samahani kwa kukosea jina lake mara kadhaa. Wengine nimeona wanalinganisha kipindi hiki na vingine; halikuwa lengo langu hasa maana dadangu kabuni na kuanzisha kipindi kizuri na muhimu hasa katika wakati huu,. Lengo langu halikuwa kushambulia elimu ya Da Joy kwa maana ya vyeti. Kuna elimu inapatikana bila vyeti (informal) na watu hawa wana uwezo mzuri wa kufikiri na kutafuta suluhisho la tatizo bila kuathiri maadili husika. na kuna gap kati ya vyeti na uwezo wa kufikiri; hivo si mara zote wasomi kuwa na elimu na wasiowasomi kutokuwa na elimu. Mengi yamesemwa ambayo da Joy anatakiwa arekebishe na hiyo ni aina moja wapo ya elimu amepata maana kufundisha ni kutoa maelekezo, na kujifunza ni kupokea maelekezo kuyachambua na kubadili tabia kwa ujumla nae kasema atapokea mnayompa na kuyafanyia kazi. Hiki kipindi kama mwanamke nakihitaji; lakini niliona hatari ya kuathiri taasisi muhimu katika taifa yaani FAMILIA
 
Sijui mleta maada ulitaka kutuaminisha nini!?kulinganisha kipindi cha Wanawake live kinachoelimisha na kusaidia jamii,na vipindi vya akina Wema,Lady Jaydee na wengine wanaoongelea mambo yao binafsi na utoto mwiingi!!Joyce usikatishwe tamaa keep it up'
 
Katika Wanawake ninaowahurumia ni hao wanaojiuza. Kwa sasa bado natafakari jinsi ya kuwasaidia. Bahati mbaya sana Kuna WANAUME ambao wanawafanya hawa WANAWAKE waendelee na hiyo kazi huku vidole vikiwaelekea Wanawake kwa majina ya CHANGUDOA, KAHABA n.k

Naomba Mungu anipe maono jinsi ya kuwafikia...

BIG UP Joyce Kiria. pamoja kuna wanao kukashifu umeishia la saba, wakidhani hilo ni tusi kwako kumbe sivyo.

Ni mengi wengine wame kushauri jinsi ya kuboresha kipindi ni vyema ukayafanyia kazi.

Ni wazi wana kukashifu lakini ni wengi unawazidi upeo na maandishi yako ni ushahidi.
 
Last edited by a moderator:
Elimu yangu ni std7, nilikuwa Housegirl zamani.

Ni Historia ambayo siionei Haya hata kidogo.

Wasomi wengi wanalalamika pamoja na PHD zao. Tumia historia yangu Joyce Kiria kutafakari umeifanyia nini nchi yako.

Kama we ni msafi chukua Mawe unirushie...

daaaa we kiboko yani wana kuita std 7lakini kuandika na kuchambua mambo una washinda.
 
nadhani watu kama ninyi kuna element ya wivu inawanyemelea. Joyce mwenyewe anakiri ameanza maisha katika hali duni sana hata aliwahi kuwa house girl. Amejitambua ,amejiendeleza na amebadili maisha yake. Na sasa ana inspire wanawake wengine katika ujasiliamali kujitambua na kupigania haki yake.aliwahi kujaribu kuongea sentensi kadhaa za kiingereza na kusema iko siku atakuwa hodari wa lugha hiyo adhimu na kukiri kuwa bado anajifunza. Sasa mtu aliyekuwa housegirl, leo ni activist mkubwa katika jamii yetu, kama kuna mahali anakosea mshaurini sio kumtuhumu na kukejeli eti hana elimu.elimu haina mwisho achene wiiiiiiivuuuuu. Joyce kwa historia yake anafanya makubwa!! Big up my seper woman!!

mkuu hawa watu ni wa ajabu sana,wana shindwa kumshauri mtu kuboresha kipindi wao wana mkashifu wakati hata wao awajui kuandika pamoja na hizo elimu.

Hebu mkuu angalia anavyo andika huyo uliyo mjibu na uangalie nani ana upeo.
 
Kwa ushauri tu joyce jaribu kupata kakozi ka sycology ili uweze kuwasoma vizuri na kufikisha ujumbe msimvunje nguvu darasa la saba sio mwisho wa upeo ajiendeleze tu
 
Kijana juzi hujui kuwa ukimuelimisha mwanamke umeelimisha jamaa jitazame vizuri mawazo wanawake wana upeo mkubwa kuliko wanaume kwenye asilimia kubwa ya mafanikio ya wanaume lazima atakuwa mwanamke bora kachangia usitukane wanawake wote mama yake alivyokuzaa na kukulea angekuwa mburumatange usingedika hapo ulipo mheshimu mwanamke
 
acheni fitina.super women anajitahidi kufichua maovu na unyanyasaji unaofanywa na baadhi ya watu katika jamii.amesaidia watu kibao kuacha tabia za unyanyasaji ktk jamii.big up super women
 
Kijana juzi hujui kuwa ukimuelimisha mwanamke umeelimisha jamaa jitazame vizuri mawazo wanawake wana upeo mkubwa kuliko wanaume kwenye asilimia kubwa ya mafanikio ya wanaume lazima atakuwa mwanamke bora kachangia usitukane wanawake wote mama yake alivyokuzaa na kukulea angekuwa mburumatange usingedika hapo ulipo mheshimu mwanamke
Wanawake wote wapu..mb.avu
 
Mi mgeni kweli nji hii, maana huaga sina mda na haya maushuzi/
 
Huyu dada Joyce Kiria amesaidia sana kuwafichua watu wasio na chembe ya ubinadamu akiwemo mtoto wa miaka 8 alieajiriwa na mama mtu mzima akamfanyie kazi za ndani dar.hebu jaribu kufikiri kama angekuwa mtoto wako..wewe mleta mada akili zako hazina tofauti na za Nape Nnauye,katibu wa itikadi na uenezi CCM!
 
daaaa we kiboko yani wana kuita std 7lakini kuandika na kuchambua mambo una washinda.

Na mungu angemjaalia akapata na elimu ya darasani hakika huyu dada angekuwa ni zaidi ya hapa embu fikiria kwa elimu hiyo aliyo itaja na hapa na uwezo wake alio nao ,,hakika munhgu yu pamoja nawe dada ila kama mapungufu ni kidogo tu yanahitajika epuka kuendesha kipindi kwa hisia zaidi kwa presenter huwa sio nzuri sana mf .kuongea na mtu kwa mfumo kama wa kusutana hasa nliliona hilo kwa yule dada aliye kuwa amekaajiri katoto kama ka house girl halafu akawa anada bwana aake ni mwanasheria so huwezi kumfanya lolote, lile tukia kwa presenter kama wewe haikupaswa kuongea naye kama umamsuta mbele sababu hali ile itamfanya ashindwe kutoa ushirikiano vizuri.. Bt kwa mengine tupo pamoja dadaangu.
 
binti mwenyekuendesha kipindi elimu hana...wafikiri uwezo wake wa kupambanua mambo utakuwa mkubwa...? naamini hata malezi mazuri hajapata toka kwa wazazi wake....

Na weng wanaoandama wanaume ni wale walioachwa kwa matabia yao yasiyoeleweka...alafu ndio anamalizia hasira huko...kwanza ana mume huyo??
 
NI JOYCE KIRIA SIO KIWIA.huyu mdada hoja zake hazina usawa kabisa,mara zote anajikita ktk shutuma dhidi ya wanaume,anashawishi wanawake wawe na kibri,pamoja na kujifanya yeye ni hakimu,
namshauri ajiendeleze kwanza kielimu maana ukimsikiliza uzumbukuku wake uko wazi kabisa.

Kwanza kaolewa? Na je yupo hapa jukwaani!!! Kuna wanawake ambao ni umiza kichwa...na hamna mwanaume anaeza kaa nae..sasa usijekuta na huyu nae yumo humo na anmalizia hasira kwenye kipindi!!
 
Back
Top Bottom