Mwana
JF-Expert Member
- Aug 6, 2010
- 5,435
- 1,967
Mabinti wakusikilize wewe ili waendelee kuwa vilema na kufa kwenye Ndoa kwa sababu ya Unyama wa Wanaume!
Imekula kwako. Ukitili wa Kijinsia Hapana hata Ndoa 1000000000 haina kwere...
Mpaka utakapojua kumpenda mkeo na kuacha vitendo vya Unyanyasaji... fyuuuuuuu
Ni vema ulivyofanya Joyce kusikiliza ushauri woote na kujibu baadae kidogo. Ukweli kipindi ni kizuri lakini kinahitaji marekebisho ambayo naamini umeyachukua na kuyazingatyia. Ukweli kitendo cha ukatili alichofanya yule baba ni kibaya sana. lakini approach iliyotumika ndio wengi wanajiuliza kwa kweli nami niliposikia mbebe mkeo kama ulivyo.... mh nilishtuka kidogo. Hivyo Joyce siskiliza mawazo ya watu ili uboreshe kipindi chako. Aidha jitahidi kuhibiti hasira il;i ulinde utu wako.
Kitu kingine elimisha jamii kufuata mambo fulani unayooona yanajenga lakini sidhani kama yote upendayo au uliyoyafanya ni shahihi kama unavyotaka watu wote waamini.
Angalia vipindi vyako uone uliopojikwaa uboreshe zaidi ili upate wadau wengi zaidi wanawake, wanaume, vijana na jamii kwa ujumla. Sidhani kama ulianzisha kipindi kuwaponda wanaume bali ni kutoa amtukio mbalimbali yanayotakiwa kupatiwa ufumbuzi kwa jamii nzima na si kuchochea mafarakano.
Kuhus hali ya yule mama ambaye hakupelekwa hospitali muda mrefu imeniachia maswaaali mengi mno na mafundisho mengi mno mno mno, si tu ukatli wa yule baba bali 'kutowajibika' kwa wengi wanaomzunguka yule mama so sad. Ni kushukuru Mungu sasa ana hali nzuri.
Mwisho kwa kazi unayoifanya jifunze saaana kudhibiti hasira.