Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

Nilikuwa na rafiki ya msabato kigamboni nikikutana nae ni ubishi mpaka naumwa kichwa!
 
Mkuu, sijajua tunapishana wapi.... Nimekueleza hapa tunaongelea vyakula..... Au Auoana ni vyakula...? Mbona Mimejieleza hapa
Hatupishani sana lile neno lako la kwanzq la " Hakuna kilichokatazwa na Mungu" lilikuwa general. Kama issue ni chakula jaribu kujihoji hivi.
Hivi biblia inaposema chakula inamaanisha hata kinyesi cha Paka, au nyama za wanadamu?
Kwani mfano wewe ukiambiwa utembee kwenye barabara ya lami Utajiuliza kupita zikoje?
 
Wewe ni Msabato bila shaka.....Sasa kama Msabato uliyeiva mwagika hapa...Tunaomba ufafanuzi wako
Sina muda huo mkuu maana hiyo mada siyo fupi kama unavyofikiria!
Anyway ya wasabato waachie wasabato na ya dini zingine pia waachie wenyewe
 
Hivi biblia inaposema chakula inamaanisha hata kinyesi cha Paka, au nyama za
Chakula anachokula binadamu kina tokana na nini..??

Mimea....je ni mimea gani..? Inafaa kuliwa..? Haina madhara ktk mwili kama sumu...? Kama haina madhara kula..

Wanyama...je! Ni wanayama gani..? Nyama yao inamadhara...? Inasumu...?kama haina we kula..

Sijajua kwanini umemuweka binadamu hapo
 
Hili tatizo kubwa mno....Laiti ungelielewa Hiyo Epistle Paul aliandika akiwa na lengo la kutatua tatizo gani kwa wakristo wa Korinto wala usingeuliza maswali ya kipuuzi namna hii..
Issue ya Paulo ilikuwa kuwafikia Wakorintho walipo. Ndio maana asema hivi

20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
1 Wakorintho 9 :20

21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria.
1 Wakorintho 9 :21

22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
1 Wakorintho 9 :22

23 Nami nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.
1 Wakorintho 9 :23
 
Sina muda huo mkuu maana hiyo mada siyo fupi kama unavyofikiria!
Anyway ya wasabato waachie wasabato na ya dini zingine pia waachie wenyewe
Umejibu vyema sana...

Kama kuna vyakula wasabato mmeamua kutokula kwasababu zenu, basi isiwe nongwa kwa watu wengine....
 
Chakula anachokula binadamu kina tokana na nini..??

Mimea....je ni mimea gani..? Inafaa kuliwa..? Haina madhara ktk mwili kama sumu...? Kama haina madhara kula..

Wanyama...je! Ni wanayama gani..? Nyama yao inamadhara...? Inasumu...?kama haina we kula..

Sijajua kwanini umemuweka binadamu hapo
Hapa umesema vizuri Rafiki tena saana . Sasa kipimo chako cha sumu ni kipi? Ni ile ukila unaanguka na kufa au ile sumu itachukua muda kukudhuru au daktari akithibitisha. Kama hapo unapata mkanganyiko rejea biblia Mungu si dhalimu au ana upendeleo kuwa awape hawa wale halafu kitu hicho hicho awanyime wengine.

Kingine kinachotusumbua ni Urafi
 
Ndugu auferet dominus naomba fuatana nami kwa umakini ili siku nyingine Usipotoshwe/Kupotosha kwenye hili

Nitaanza na reference zako toka biblia;

1. Matt 12:46 "Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu walipofika kusimama nje" Hapa bado biblia haijaonesha kuwa Maria mama yake Yesu alizaa baada ya Yesu,kwani ndugu zake Yesu wanaweza kuwa ni watoto wa baba au mama mkubwa/mdogo ndugu wa ukoo au Wale Waliolishika na Kulifuata neno Baba yake(Mungu),(kumbuka hata yeye mwenyewe Yesu alishawahilisema hilo sina kumbukumbu nzuri ya mstari ningeweka).

2.Matt 13:55 "Je,huyu si yule mwana wa seremala?Je, mama yake si anaitwa Maria na KAKA zake si kina Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda? Kwa tafsiri yako bwana auferet dominus..,Maria Alishazaa Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda kabla ya kumzaa Yesu..!!!!

Narudi palepale ndugu zake Yesu wanaweza kuwa watoto wa mama mkubwa/mdogo au baba mkubwa/mdogo au wale waliolishika na kulifuata neno la Baba yake(Mungu).

Ukitaka kulazimisha ya kuwa Yakobo, Yosefu, Simon na Yuda kuwa ni kaka zake wa kuzaliwa na Bikira Maria mama wa Yesu, utakuwa unapingana na andiko hili;

Luka 1:26-45(Naomba hapa nichukue mistari michache ila kwa kukusaidia soma yote kama nilivyoweka hiyo mistari)
26 " Mnamo mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya"
27 "Kwa msichana bikira aitwaye Maria mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu,wa ukoo wa Daudi..,ndugu auferet dominus utaona hapa "Msichana Bikira Aitwaye Maria" hilo ni la kwanza,mtu bikira ni mtu ambaye hajazaa..!!la pili kina Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda ni Kaka ndani ya Ukoo wa Daudi na si Kaka wa kuzaliwa na Maria mama wa Yesu...!!!!
34 "Maria akamjibu Yatawezekanaje hayo,hali mimi ni Bikira?Ndugu hapa biblia inazidi kusisitiza kuwa Maria mama wa Yesu alikuwa bikira kabla na baada ya kumzaa Yesu...,ukisema Maria alikuja kuwazaa Yakobo, Yosefu,Simon na Yuda baadae,nitakuuliza ilikuaje pale kwenye Matt 13:55 wawajue Seremala,Maria na wadogo zake yani Yakobo,Yosefu, Simon na Yuda wasimjue kaka yao yani Yesu...?????

Naomba niishie hapa ili nisikuchoshe na natumai utakuwa umepata mwanga kidogo kwenye hili la Maria mama wa Yesu kuwa bikira kabla na baada ya kumzaa Yesu, huu ni upotoshaji mkubwa umekuwa ukifanywa na vikundi mbalimbali,nafikiri kwa kutokusoma vizuri biblia au kwa makusudi.

Asante.
Wewe unajifanya kipofu bure au sijui ndo kujipagawisha hukoo? Umesoma wapi kuwa hao walimzidi umri Yesu. Nani aliyesema kuwa ikisemwa brother maana yake ni mkubwa wa mtu? Unataka kulazimisha wakina yakobo wawe wakubwa kuzaliwa hapa dunia ni kuliko Yesu ili itetee ajenda yako kuwa Maria alikuwa bikira mpaka anakufa? Mistari yote niliyokuletea kutoka kwenye maandiko hayajasema kuwa hao ni seniors kwa Yesu. Soma tena ukajitoe kutokujua na kulishwa uongo. Ninyi watu maandiko yako wazi halafu mnatisha watu na maandiko yasiyokuwepo. Acheni uongo.
 
Sasa kipimo chako cha sumu ni kipi? Ni ile ukila unaanguka na kufa au ile sumu itachukua muda kukudhuru au daktari akithibitisha
Sumu ni sumu tuu...iwe ya short term au long...Kama ikithibitishwa au baada ya kula ukapata madhara ya moja kwa moja..hakuna mjadala ni kusitisha kula hicho chakula....
 
Nimepata muda wa kufuatilia mahubiri ya maisha hatimaye yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya Tanzania. Nimejiuliza mnataka tufanye nini ikiwa mafundisho yenu yana msigano unaochanganya watu.

Mmoja wenu amekuwa akifundisha kitu kinachoitwa ujasiriamali. Moja ya mafundisho ni ufugaji wa ng'ombe wa nyama na maziwa, pamoja na kuku wa mayai. Maana yake ni kwamba, watu wanahitaji mayai, maziwa na nyama.

Leo namsikia mhubiri akisema ogopa sana mayai! Mafuta ambayo hata kwenye maziwa yamo mengi sana! Pia akaenda zaidi kusema ogopa hasa nyama nyekundu. Nguruwe ni haramu lakini ni kati ya wanyama wenye nyama nyeupe!

Sasa tufanye nini! Tufuge kuku wa mayai kwa ajili ya kuuzia wengine huku sisi tukiyakwepa ama tuache kwa vile mayai ni hatari kama ulivyosema?

Mkuu! Kwa taarifa... nguruwe sio white meat.. ni red meat kabisa
 
Wewe..!!!!?
Ndio, ni mimi. Ushatupa yale masanamu yako ya bikira na misalaba na marozari? Hivi mirozari mmefundishwa kwenye kitabu gani? Wajua wenye kutembea na misalaba na milozali na visanamu ni waoga wa mavampaya. Eti ukiona vampaya we lionyeshe tu msalaba litakimbia kaburini. Muvi zitawauweni nyie. Don’t be such superstitious people. Trust in Jesus and all your worries will be settled. Sio some tell tale maria unaefikiri anakuombea. She is dead!
 
Akikujibu niite
Usishabikie bali unatakiwa usikitike na kumuombea,mada iliyoko mezani ni vyakula hayo mengine yanatoka wapi..???

Fuatana nami;

Matendo:10:9-15 (Hapa nitaweka mistari michache ila kwa kukusaidia wewe kasome mistari yote kama nilivyokuandikia)
11 "Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka imeteremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12 " Ndani ya shuka hiyo kulikuwa kila aina ya wanyama,wanyama wenye miguu minne,wanyama watambaao na ndege wa angani.
13 "Akasikia sauti ikimwambia, Petro amka uchinje ule!
14 " Petro akajibu La Bwana mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu.
15 "Ile sauti ikasikika tena ikimwambia,usivitie najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
Rejea tena Matendo 11:9 na Rumi 14:14 ili uendelee kupata maarifa.

Naomba niishie hapa kwa sasa.
Akikujibu niite
 
sikiliza, sikiliza, sikiliza tena mafundisho ya huyo jamaa utaelewa usiwe na papara
 
Back
Top Bottom