Sasa ni maandiko hayo ndio yanasema mariam alizaa watoto wengine as per Matt. 12:46; 13:55; Mark 6:3; John 2:12; 7:3, 5, 10; Acts 1:14; 1 Cor. 9:5; Gal. 1:19. Wewe lete ushahidi kuwa hakuzaa na yusufu.
Uwezo wa Mungu naufahamu lakini nafahamu pia uwezo wa shetani kutunga vitu vya kishetani ili awapoteze wateule. Alianza hayo toka pale eden. Moja ya uongo mkubwa aliowahi kutunga shetani ni kuwa huyo mariamu yuko anaishi mbinguni.
Ndugu auferet dominus naomba fuatana nami kwa umakini ili siku nyingine Usipotoshwe/Kupotosha kwenye hili
Nitaanza na reference zako toka biblia;
1. Matt 12:46 "Yesu alikuwa bado anasema na umati wa watu wakati mama yake na ndugu walipofika kusimama nje" Hapa bado biblia haijaonesha kuwa Maria mama yake Yesu alizaa baada ya Yesu,kwani ndugu zake Yesu wanaweza kuwa ni watoto wa baba au mama mkubwa/mdogo ndugu wa ukoo au Wale Waliolishika na Kulifuata neno Baba yake(Mungu),(kumbuka hata yeye mwenyewe Yesu alishawahilisema hilo sina kumbukumbu nzuri ya mstari ningeweka).
2.Matt 13:55 "Je,huyu si yule mwana wa seremala?Je, mama yake si anaitwa Maria na KAKA zake si kina Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda? Kwa tafsiri yako bwana auferet dominus..,Maria Alishazaa Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda kabla ya kumzaa Yesu..!!!!
Narudi palepale ndugu zake Yesu wanaweza kuwa watoto wa mama mkubwa/mdogo au baba mkubwa/mdogo au wale waliolishika na kulifuata neno la Baba yake(Mungu).
Ukitaka kulazimisha ya kuwa Yakobo, Yosefu, Simon na Yuda kuwa ni kaka zake wa kuzaliwa na Bikira Maria mama wa Yesu, utakuwa unapingana na andiko hili;
Luka 1:26-45(Naomba hapa nichukue mistari michache ila kwa kukusaidia soma yote kama nilivyoweka hiyo mistari)
26 " Mnamo mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya"
27 "Kwa msichana bikira aitwaye Maria mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu,wa ukoo wa Daudi..,ndugu auferet dominus utaona hapa "Msichana Bikira Aitwaye Maria" hilo ni la kwanza,mtu bikira ni mtu ambaye hajazaa..!!la pili kina Yakobo,Yosefu,Simon na Yuda ni Kaka ndani ya Ukoo wa Daudi na si Kaka wa kuzaliwa na Maria mama wa Yesu...!!!!
34 "Maria akamjibu Yatawezekanaje hayo,hali mimi ni Bikira?Ndugu hapa biblia inazidi kusisitiza kuwa Maria mama wa Yesu alikuwa bikira kabla na baada ya kumzaa Yesu...,ukisema Maria alikuja kuwazaa Yakobo, Yosefu,Simon na Yuda baadae,nitakuuliza ilikuaje pale kwenye Matt 13:55 wawajue Seremala,Maria na wadogo zake yani Yakobo,Yosefu, Simon na Yuda wasimjue kaka yao yani Yesu...?????
Naomba niishie hapa ili nisikuchoshe na natumai utakuwa umepata mwanga kidogo kwenye hili la Maria mama wa Yesu kuwa bikira kabla na baada ya kumzaa Yesu, huu ni upotoshaji mkubwa umekuwa ukifanywa na vikundi mbalimbali,nafikiri kwa kutokusoma vizuri biblia au kwa makusudi.
Asante.