Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,633
Reaction score
7,021
Nimepata muda wa kufuatilia mahubiri ya maisha hatimaye yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya Tanzania. Nimejiuliza mnataka tufanye nini ikiwa mafundisho yenu yana msigano unaochanganya watu.

Mmoja wenu amekuwa akifundisha kitu kinachoitwa ujasiriamali. Moja ya mafundisho ni ufugaji wa ng'ombe wa nyama na maziwa, pamoja na kuku wa mayai. Maana yake ni kwamba, watu wanahitaji mayai, maziwa na nyama.

Leo namsikia mhubiri akisema ogopa sana mayai! Mafuta ambayo hata kwenye maziwa yamo mengi sana! Pia akaenda zaidi kusema ogopa hasa nyama nyekundu. Nguruwe ni haramu lakini ni kati ya wanyama wenye nyama nyeupe!

Sasa tufanye nini! Tufuge kuku wa mayai kwa ajili ya kuuzia wengine huku sisi tukiyakwepa ama tuache kwa vile mayai ni hatari kama ulivyosema?
 
Fwatilia vizuri utazidi kuelewa! Hata hivyo sidhani kua ngurue yupo kwenye kundi la nyama nyeupe, kuhusu ujasieiamali hayo ni mafundisho ambayo yapo na hata kwa dini zote na ambao hawana dini kujikwamua kiuchumi, na moja ya mafindisho ya Afya si kwa wasabato tu, hata vitabu na madactari watakuambia nyama nyekundu si nzuri kiafya ila hawajakukataza kula, ila lazima mafundisho yawepo
 
Hawa jamaa ni waongo wakubwa ukiwafuata huishi dunia hii hata wao karibia vyote wanavyojinadi ni vibaya wanagonga

1. Wanajifanya hawanywi cocacola lakini wanagonga mitaani kama kawa

2. Wanajifanya hawanywi chai ya majani ya chai ama kahawa na badala yake eti wanajanani gani dizain ambayo hayawezi kufanya kazi ya chai lakini wanazigonga tii kama kawa

3. Wanajifanya eti mdudu ni haramu lakini wanamgonga kimya kimya

4.Siku hizi wamekuwa ni waganga wa kienyeji na wanaibia watu wenye magonjwa sugu kwa kitu wanachokiita "SANITARIUM CLINIC" tena eti wana compyuta ambayo ukishika inatbaini magonjwa yoote mwilini. Utapeli mtupu wametajirika lakini watu wanaendelea kuteseka na magojwa yao
 
Sidhani hata ulielewa mafundisho. Jaribu kuangalia bila kuwa na mawazo hasi naamini utatoka na kitu cha kukusaidia kiafya.

"Muwe na kiasi katika mambo yote". Kula na kunywa kwa kiasi, hayo mayai ukila kila siku ni hatari kwa afya yako, hayo siyo mafundisho ya wasabato bali ni mafundisho ya afya.
 
Hamuewezi kuelewa hayo mafundisho kama hamjawa tayari kuelewa. Kweli yote lazima isemwe kisha uchague wapi pa kuelekea.

Unamiliki kazi au kazi inakumiliki?

Kama unaweza kula chakula cha mifugo ( unprocessed foods) kama unga ,au maharage su akaamua kuyabadilisha ktk hali tofauti ili utengeneze ajira kwa watu wako then ule processed foods

Hivyo navyo vibaya?
Anyway shule za kata zimeumiza Taifa leo, watu wamekuwa wajinga wajinga tu hata hawana fikra sahihi, reasoning na kufanya right decisions.
 
Sidhani hata ulielewa mafundisho. Jaribu kuangalia bila kuwa na mawazo hasi naamini utatoka na kitu cha kukusaidia kiafya.

"Muwe na kiasi katika mambo yote". Kula na kunywa kwa kiasi, hayo mayai ukila kila siku ni hatari kwa afya yako, hayo siyo mafundisho ya wasabato bali ni mafundisho ya afya.
Afya ya wapi mkuu wakati hivi sasa watu wanahimizwa kutumia protein kwa wingi kuliko wanga?
 
Tatizo ni akili yako
Hatufanani akili mkuu,ila ninachojua,huwezi kuhamasisha watu wafuge kuku wa mayai hapo hapo unaua soko la mayai kwa kuwatahadharisha watu na hatari ya mayai!Si ni bora uwahamasishe wafanye kitu kingine?
 
Tatizo ni akili yako

Huyu jamaa kweli tatizo ni akili yake na wala siyo wasabato. Tangu lini nguruwe akawa nyama nyeupe? Ni fungu gani kwenye biblia linakataza kula nyama nyekundu au maziwa na mayai? Vitu vingine siyo amri kumi za Mungu, bali ni ushauri wa kiafya, madaktari wote duniani wanajua kuwa ulaji wa red meat si salama kwa afya. Lakini za kuambiwa changanya na zako. Ni kiwango gani cha ulaji huo ni hatari kwa afya yako? Hakuna palipoelezwa. Wasabato hawakatazi kula nyama nyekundu bali ni ushauri wa kitaalam kama unaweza. Kama huwezi chapa nyama kwa kwenda mbele. Isipokuwa kama ilivyo kwa watu wa nje, kuna baadhi ya watu au kundi la watu wachache ambao sijui niwaite ni extremist ambao huchukulia mambo kila kitu kwa mrengo wa kulia. Hili kundi lipo kila dhehebu, iwe kwa waislamu, wakatoliki au walokole. Ni kundi hatari sana. Na watu wa nje wanapowaona wanadhani ndo wasabato au waislamu walivyo.

Hivi mnakumbuka kuna kundi lilishawahi kwenda airport wakijiandaa kupanda ndege kwenda kuhubiri ulaya bila visa wala pasport? Siyo Wasabato kama kanisa, bali ni kundi lililojitenga na kujiwekea mrengo flani wa kiimani, kundi ambalo hata ndani ya kanisa halitambuliwi, lakini huko nje wakajua ni wasabato. Ajabu kweli.
 
Kunakipindi walikaa airport siku kadhaa kwamba wanataka kwenda ulaya bila kulipa nauli ili wakahubiri injili, hapo ndipo niliwatambua hamnazo

Ni vizuri tukawa tunafuatilia mambo kwa undani kuliko kuchukulia juu juu ukawa umedanganyika mwenyewe na nafsi yako. Kwa taarifa yako wale siyo Wasabato wa Seventh Day Adventist Church unaowafahamu. Ni kikundi kilichojimega kutoka kwenye Usabato kikajiita Wasabato masalia. Nakumbuka hiyo taarifa ilirushwa hadi kwenye TV, unaweza ukarejea kamainapatikana kwenye youtube au internet ya kawaida. Ni kundi lililoasi mafundisho halisi ya kanisa, wakaanzisha mafundisho yao mengine wakichanganya na baadhi ya mafundisho halali. Ukisoma historia ya extremist groups kwenye madhehebu yote utayakuta hayo makundi, hata kanisani mwako yapo.
 
Hawa jamaa ni waongo wakubwa ukiwafuata huishi dunia hii hata wao karibia vyote wanavyojinadi ni vibaya wanagonga

1. Wanajifanya hawanywi cocacola lakini wanagonga mitaani kama kawa

2. Wanajifanya hawanywi chai ya majani ya chai ama kahawa na badala yake eti wanajanani gani dizain ambayo hayawezi kufanya kazi ya chai lakini wanazigonga tii kama kawa

3. Wanajifanya eti mdudu ni haramu lakini wanamgonga kimya kimya

4.Siku hizi wamekuwa ni waganga wa kienyeji na wanaibia watu wenye magonjwa sugu kwa kitu wanachokiita "SANITARIUM CLINIC" tena eti wana compyuta ambayo ukishika inatbaini magonjwa yoote mwilini. Utapeli mtupu wametajirika lakini watu wanaendelea kuteseka na magojwa yao
Mkuu kweli kabisa hivi hizo kompyuta zao mbona kwenye hizi hospitality za kawaida hazipo?
Mkewangu wangu wamemuingiza king daily anahiytaji pesa za dozi za miezi 6 yani full maumivu.
 
Back
Top Bottom