Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

Kipi tufanye Wasabato mnatuchanganya!

Fwatilia vizuri utazidi kuelewa! Hata hivyo sidhani kua ngurue yupo kwenye kundi la nyama nyeupe, kuhusu ujasieiamali hayo ni mafundisho ambayo yapo na hata kwa dini zote na ambao hawana dini kujikwamua kiuchumi, na moja ya mafindisho ya Afya si kwa wasabato tu, hata vitabu na madactari watakuambia nyama nyekundu si nzuri kiafya ila hawajakukataza kula, ila lazima mafundisho yawepo
Mkuu nitahitaji chumba na sebule soon, budget ya laki moja. Choo ndani.
 
Afya ya wapi mkuu wakati hivi sasa watu wanahimizwa kutumia protein kwa wingi kuliko wanga?
Mkuu tatizo ni source ya hivyo protein.. Vimelea vya madawa ya kila aina IPO kwenye GMOs ..na hawa kuku Wa kisasa.. Nguruwe pia sio vizuri..

Pia kutokujua kwako/Kwangu laws of motion hakuathiri utendaji kazi wake katika maisha ya kila siku. Ndio maana wahenga wanasema elimu haina mwisho.

Ngoja nikuibie mkuu..Nikiwa darasa LA pili..mwl alitufunza katika hesabu za (2-3) jibu lilikuwa haiwezekani.. Tulipo fika darasa la tatu tukajua hasi na chanya na jibu letu likawa -1(hasi 1)

Huwezi kuelewa kwa kuangalia somo moja kisha ukakimbia..take time kwenda na mkufunzi utaelewa tu. Hawa ni binadamu wanajenga hoja kibinadamu maana wanazungumza na wanadamu..mpe muda wako.

Maisha Hatimaye.
 
Wasabato walishalaanika....Na aliyewawafanya walaanike ni Muanzilishi wa kikundi chao Nabii Mke Ellen G White..
😀😀😀😀😱😱 Kijana wa bwana mdogo papa francis hujapona wendawazimu mpaka leo?
Kama umekunywa dawa za leo hebu jibu hili, maria bikira yule mpagani wa kigiriki aliyemimbishwa na vidume yuko wapi vile?
 
Nimepata muda wa kufuatilia mahubiri ya maisha hatimaye yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya Tanzania.Nimejiuliza mnataka tufanye nini ikiwa mafundisho yenu yana msigano unaochanganya watu.

Mmoja wenu amekuwa akifundisha kitu kinachoitwa ujasiria mali.Moja ya mafundisho ni ufugaji wa ng'ombe wa nyama na maziwa,pamoja na kuku wa mayai.Maana yake ni kwamba,watu wanahitaji mayai,na maziwa na nyama.

Leo namsikia mhubiri akisema ogopa sana mayai! Mafuta ambayo hata kwenye maziwa yamo mengi sana!Pia akaenda zaidi kusema ogopa hasa nyama nyekundu.Nguruwe ni haram lakini ni kati ya wanyama wenye nyama nyeupe!
Sasa tufanye nini!Tufuge kuku wa mayai kwa ajili ya kuuzia wengine huku sisi tukiyakwepa ama tuache kwa vile mayai ni hatari kama ulivyosema?
Mwenyewe ndo unajichanganya. Read meat hata sio wasabato tu ila ki afya sio nzuri, na mayai pia sio mazuri.
 
Hatufanani akili mkuu,ila ninachojua,huwezi kuhamasisha watu wafuge kuku wa mayai hapo hapo unaua soko la mayai kwa kuwatahadharisha watu na hatari ya mayai!Si ni bora uwahamasishe wafanye kitu kingine?
This is a scientific advice

Muulize daktari yeyote ulaji wa mayai mengi kwa siku moja, na kisha ukawa ndo mtindo wa maisha, ni hatari kwa afya yako.
 
Hahaha hawa wasabato hata akija mungu wa wote watamkataa, kwa ubinafsi wao watataka mungu wao peke yao. Wao hujiona ni special na mbingu ni yao peke yao, hata mungu wao ni tofauti na huyu wetu.

Sishanga, wakikwambia kuku wao ni tofauti na hawa kuku wengine, hata mayai wanayokula wao pia ni tofauti na mayai haya tunayokula sisi.

Wanataka wawe tofauti kwa kila kitu na binadamu wengine.
Siogopi kuwa tofauti,Ila naogopa kubaguliwa na binadamu mwenzangu kwa kigezo cha dini.
Utofauti upo kwenye mapanki yao wanayo nyoa
 
Hawa jamaa wataikosa mbingu kwa unafiq tuu. Ayatul munafiq thalatha
 
Hawa jamaa wataikosa mbingu kwa unafiq tuu. Ayatul munafiq thalatha
Mbingu ipi? Ni ipi ambayo unawajua watakaoingia na watakaoikosa? Ipi hiyo? Nina wasiwasi kama unamaanisha ile aliyoitaja YESU kuwa "... angalieni makahaba wanawatangulia ninyi katika ufalme wa mbingu..."
 
Hawa jamaa ni waongo wakubwa ukiwafuata huishi dunia hii hata wao karibia vyote wanavyojinadi ni vibaya wanagonga

1. Wanajifanya hawanywi cocacola lakini wanagonga mitaani kama kawa

2. Wanajifanya hawanywi chai ya majani ya chai ama kahawa na badala yake eti wanajanani gani dizain ambayo hayawezi kufanya kazi ya chai lakini wanazigonga tii kama kawa

3. Wanajifanya eti mdudu ni haramu lakini wanamgonga kimya kimya

4.Siku hizi wamekuwa ni waganga wa kienyeji na wanaibia watu wenye magonjwa sugu kwa kitu wanachokiita "SANITARIUM CLINIC" tena eti wana compyuta ambayo ukishika inatbaini magonjwa yoote mwilini. Utapeli mtupu wametajirika lakini watu wanaendelea kuteseka na magojwa yao
Tatizo kubwa lipo kwenye ubongo wako kushindwa kupambanua fikra sahihi na muktadha barabara pole xana.Nakufananisha na tz nchi yenye rasilimali za kutosha lkn bado maskini ifike Mahali ubadilike
 
MUNGU WA MBINGUNI AKUSAIDIE RAFIKI.....
Nimepata muda wa kufuatilia mahubiri ya maisha hatimaye yanayorushwa mubashara kutoka Mbeya Tanzania. Nimejiuliza mnataka tufanye nini ikiwa mafundisho yenu yana msigano unaochanganya watu.

Mmoja wenu amekuwa akifundisha kitu kinachoitwa ujasiriamali. Moja ya mafundisho ni ufugaji wa ng'ombe wa nyama na maziwa, pamoja na kuku wa mayai. Maana yake ni kwamba, watu wanahitaji mayai, maziwa na nyama.

Leo namsikia mhubiri akisema ogopa sana mayai! Mafuta ambayo hata kwenye maziwa yamo mengi sana! Pia akaenda zaidi kusema ogopa hasa nyama nyekundu. Nguruwe ni haramu lakini ni kati ya wanyama wenye nyama nyeupe!

Sasa tufanye nini! Tufuge kuku wa mayai kwa ajili ya kuuzia wengine huku sisi tukiyakwepa ama tuache kwa vile mayai ni hatari kama ulivyosema?
 
Back
Top Bottom