Nigrastratatract nerve
JF-Expert Member
- Sep 4, 2019
- 1,401
- 3,937
KINANA:VIONGOZI SERIKALINI FUATENI NYAYO ZA RAIS SAMIA KUESHIMU SHERIA, KANUNI MNAPOCHUKUA HATUA DHIDI YA WATENDAJI
Na Mwandishi Wetu
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana ametaka viongozi na watenaji serikalini kuzingatia kanuni, sheria, utaratibu na Katiba wanapowakosoa watendaji.
Amesema ni vyema wakajifunza kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pamoja na kuwa na uwezo na mamaka lakini hajawahi kusimama hadharani na kuvunja haki ya utu wa mtu hususan watendaji katika ngazi mbalimbali.
Kinana aliyasema hayo jana Ushirombo, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM, viongozi na wananchi alipofungua jengo la ofisi za CCM la wlaya hiyo.
“Nataka kufafanua hili ambalo nimezungumza katika Mkutano Mkuu hapa Bukombe, ni kwamba viongozi wasimamie watendaji serikalini, wasimamie sheria, kanuni na utaratibu lakini si vizuri kuwasema hadharani na kuwafedhehesha watendaji wa serikali.
“Mfano mzuri wa kuigwa ni wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwani hatujawahi kuona akisimama hadharani akmfedhehesha mtendaji serikalini, kwa sababu yeye ni muumini wa utawala bora, unaozingatia katiba, sheria, kanuni na taratibu,” alisema.
Kinana alsisitiza watendaji wote wa serikali wanasimamiwa na kanuni, sheria, katiba na utendaji serikalini.
Na Mwandishi Wetu
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana ametaka viongozi na watenaji serikalini kuzingatia kanuni, sheria, utaratibu na Katiba wanapowakosoa watendaji.
Amesema ni vyema wakajifunza kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye pamoja na kuwa na uwezo na mamaka lakini hajawahi kusimama hadharani na kuvunja haki ya utu wa mtu hususan watendaji katika ngazi mbalimbali.
Kinana aliyasema hayo jana Ushirombo, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM, viongozi na wananchi alipofungua jengo la ofisi za CCM la wlaya hiyo.
“Nataka kufafanua hili ambalo nimezungumza katika Mkutano Mkuu hapa Bukombe, ni kwamba viongozi wasimamie watendaji serikalini, wasimamie sheria, kanuni na utaratibu lakini si vizuri kuwasema hadharani na kuwafedhehesha watendaji wa serikali.
“Mfano mzuri wa kuigwa ni wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwani hatujawahi kuona akisimama hadharani akmfedhehesha mtendaji serikalini, kwa sababu yeye ni muumini wa utawala bora, unaozingatia katiba, sheria, kanuni na taratibu,” alisema.
Kinana alsisitiza watendaji wote wa serikali wanasimamiwa na kanuni, sheria, katiba na utendaji serikalini.