Vijana inabidi mjitahidi kuijua nchi yenu ilipitaje pitaje. Alichosema mtoa mada ni sahihi kabisa. Nchi ilikuwa imekwisha Hadi Nyerere anaondoka na infact, ndio sababu akaondoka maana sera zake na uchumi wake ulifeli miserably. Na ukitaka kuthibitisha hilo, ni paper iliyowasilishwa Bungeni na Mzee Marehemu Amir Jamal mwaka 1985 (Economic Recovery Program). Unadhani kwanini ilibidi mpaka pawepo na mpango wa kunusuru/kuokoa uchumi? Ni kwasababu uchumi ulikufa kabisa. Nchi haikuwa na uwezo wa kuzalisha wala kuagiza bidhaa nje. Uzalishaji wa kilimo ulififia kabisaa. Uzalishaji wa viwandani ulishaanza kufa ikiwa ni impacts ya kuwanyang'anya (nationalization) viwanda wahindi waliokuwa wanaviendesha na kuchukuliwa na serikali ambayo haikuwa na uwezo wa kuviendesha. Lakini pia alikuwa akifanya sera za ubabe kuuzuia vipuri kutoka nje na badala yake kulazimisha vitengengenzwe ndani huku kuliwa hakuna uwezo. Mtabisha sana watanzania lakini huo ndio ukweli. Nyerere alifanikiwa kwenye kuwaunganisha watanzania na kuwajengea Elimu ya uoga lakini kwenye uchumi, ndio chanzo cha matatizo yote haya.
Kwa kuwa uchumi ulikufa kabisa, hakukuwa na namna nyingine zaidi ya kuwaangukia WB, IMF na baadhi ya nchi za kiulaya Ili kutoa support (hususan ya kuweza kuagiza bidhaa kwa ajili ya matumizi ya ndani). Unasema Mwinyi alimuachia nchi Mkapa eti haikopesheki, Nyerere alimuachia nchi Mwinyi sio haikopesheki tu, bali haina chakula, haina nguo, haina bidhaa hata chumvi na sukari na mbaya kuliko yote, hata maelewano na hayo mataifa makubwa hayakuwa mazuri. Kwa kipindi cha miaka mifano hadi anaondoka alishindwa kukamilisha majadiliano ya msaada kutoka kwa hao mabeberu.
Tafuta Economic Recovery Program paper (kama ipo online) uisome, hope kama ni mwenye kufikiri utapata kitu kidogo.