Beberu
JF-Expert Member
- Jan 26, 2017
- 3,941
- 7,937
Habari za wakati huu ndugu watanzania
Kazi iendeleeiendelee
Baada ya nchi kumshinda Mwalimu mwaka 1985 aliamua kukaa pembeni na kumuachia kijiti Mwinyi ambae aliingia alikuta nchi imechakaa sana, uchumi upo hovyo, wananchi wanavaa nguo zenye viraka juu ya viraka, maduka ya ushirika yamekuwa shida, bidhaa muhimu hazipatikani, nchi haina fedha za kigeni n.k
Lakini licha ya yote hayo wananchi walimpenda sana Mwalimu kutokana na propaganda zake na hotuba zake za kulaumu mabeberu na wazungu na matajiri (ref. Kitabu cha Mengi) na hivyo kupanda mbegu kuwa shida zetu zimetokana na wazungu na matajiri.
Alipokuja Mwinyi akaanza kufungua nchi, kuruhusu watu kufanya biashara, kubinafsisha baadhi ya viwanda vilivyokuwa vinaenda kufa, akatoa uhuru wa siasa, akaanza kushirikiana na Marekani et al.
Wananchi wanyonge wote wakaanza kusema Mwinyi anatumika na mabeberu huku wengine wakisema ni dhaifu (hadi Nyerere aliandika hili) lakini deep down wote tunajua Mwinyi alikuwa sahihi na Nyerere alikuwa wrong na hii imepelekea hadi leo Mwinyi hapewi heshima anayostahili na mtaa kwa sababu watu bado walikumbuka propaganda za Nyerere wakati wa utawala wake na hivyo kushindwa kumuelewa.
Upande wa SSH naye anaishi chini ya propaganda za Magufuli na licha ya mazuri yote anatofanya eg kufungua nchi, kutoa uhuru kwa raia, kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji lakini bado anaishi kwenye kivuli cha SSH.
Licha ya mapungufu yake SSH anajitahidi kufanya kazi nzuri ila ndo hivyo jamii bado imemezwa na propaganda za Magufuli aliyefanya jamii ione bila yeye hakuna kitachofanyika.
Nahofia huko mbele kama akichoka SSH anaweza fuata nyayo za JPM ili tu naye akubalike kama mtangulizi wake kitu ambacho ni tatizo.
Thanks kwa kusoma na karibu kwa kuchangia
Nb. Nafikiria kuinunua JF mnaonaje wadau?
Kazi iendeleeiendelee
Baada ya nchi kumshinda Mwalimu mwaka 1985 aliamua kukaa pembeni na kumuachia kijiti Mwinyi ambae aliingia alikuta nchi imechakaa sana, uchumi upo hovyo, wananchi wanavaa nguo zenye viraka juu ya viraka, maduka ya ushirika yamekuwa shida, bidhaa muhimu hazipatikani, nchi haina fedha za kigeni n.k
Lakini licha ya yote hayo wananchi walimpenda sana Mwalimu kutokana na propaganda zake na hotuba zake za kulaumu mabeberu na wazungu na matajiri (ref. Kitabu cha Mengi) na hivyo kupanda mbegu kuwa shida zetu zimetokana na wazungu na matajiri.
Alipokuja Mwinyi akaanza kufungua nchi, kuruhusu watu kufanya biashara, kubinafsisha baadhi ya viwanda vilivyokuwa vinaenda kufa, akatoa uhuru wa siasa, akaanza kushirikiana na Marekani et al.
Wananchi wanyonge wote wakaanza kusema Mwinyi anatumika na mabeberu huku wengine wakisema ni dhaifu (hadi Nyerere aliandika hili) lakini deep down wote tunajua Mwinyi alikuwa sahihi na Nyerere alikuwa wrong na hii imepelekea hadi leo Mwinyi hapewi heshima anayostahili na mtaa kwa sababu watu bado walikumbuka propaganda za Nyerere wakati wa utawala wake na hivyo kushindwa kumuelewa.
Upande wa SSH naye anaishi chini ya propaganda za Magufuli na licha ya mazuri yote anatofanya eg kufungua nchi, kutoa uhuru kwa raia, kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji lakini bado anaishi kwenye kivuli cha SSH.
Licha ya mapungufu yake SSH anajitahidi kufanya kazi nzuri ila ndo hivyo jamii bado imemezwa na propaganda za Magufuli aliyefanya jamii ione bila yeye hakuna kitachofanyika.
Nahofia huko mbele kama akichoka SSH anaweza fuata nyayo za JPM ili tu naye akubalike kama mtangulizi wake kitu ambacho ni tatizo.
Thanks kwa kusoma na karibu kwa kuchangia
Nb. Nafikiria kuinunua JF mnaonaje wadau?