Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
- Thread starter
- #61
Nimejifunza jambo moja hapa dodoma kuwa lowasa hakamati kabisa maana kwanza anawatu wengi
Ni kweli hakamatiki ana watu wengi sana hapo Dodoma ambao wamesombwa kutoka maeneo mbalimbali kucheza filamu kama ile ya Igunga ya kulia na kugaragara akivuliwa gamba!!!
Millya & Group at work. Jambo la msingi ambalo siwezi kushangaa na kumtisha Mwenyekiti wao na akatishika, japo sasa naona kama mkali kidogo. Kama nilivyosema awali, "mbele giza nyuma kaburi", wakiwavua watakua wameamua kwenda gizani maana hakuna ajuae kwa hakika plan 'B', 'C' na 'D' ya ENL, na pia hakuna ajuae yatakayotokea, lakini giza haina maana hakuna njia, ni kwamba tu hakuna mwanga ila njia ipo, lakini kurudi nyuma mwanga upo kuwa ni kaburi la uongozi wa juu wa CCM chini ya Kikwete na ushindi mkubwa kwa ENL na kundi lililo "tiifu" kwake, ambalo linaendeshwa kama 'serikali ya pembeni' maana lina bajeti iliyotuna,
lina watendaji mahiri, lina vijana 'watiifu' wanaofanya kazi usiku na mchana na humu JF wamejaa tele, wana vyombo vya habari na waandishi wa habari wengine na kikubwa kabisa na cha hatari wana mfumo hatari sana ambao uko kazini wakati wote na baadhi wamo ndani ya mfumo halali, na ingekua nchi nyingine hawa wangeitwa 'magaidi' maana 'mchana wanamulika, usiku wanachoma'.
Hawa 'magaidi' ni vigumu sana kuwatambua maana baadhi wanajifanya watiifu sana kwenye mfumo halali, baadhi wanajifanya hata kushambulia na kuhujumu kundi la ENL kiana. Haya yote JK anayajua, watu wake wa Usalama wanayajua, ndio maana nasema lolote laweza kutokea kama mkuu atasema, "sasa imetosha" kauli ambayo kwa sasa iko kinywani mwake.