Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

JK, rais na CCM chairman, enough is enough. Hakuna nchi inayoendeshwa huku watu walio nje ya serikali wakicontrol sehemu kubwa ya mamlaka.

Yaani Jk ameacha nchi imefika watu wanapledge allegiance kwa Lowassa na kumtetea waziwazi EL against Jk na kuendelea kupeta. Hell no, haiwezekani hata kidogo, kwa sababu je EL akiamua ambadilishe Jk itakuwa vipi??

Usalama kazi yake kubwa ni kuprotect institution ya Presidency, sasa usalama gani huu EL anaendesha nchi nje ya mfumo waziwazi??

Tutajua ukweli kuhusu mwelekeo wa nchi hiyo next week mungu akitupa uzima.

May Almighty God Bless Tanzania.

Una maana kuna USALAMA mbili? Yaani USALAMA WA TAIFA na USALAWA WA CCM? Usalama wa Taifa ni kuhakikisha hakuna matishio ya amani ndani ya Taifa na sio kuhakikisha usalama wa wananchi. Ila kwa democrasia ya Tanzania, Usalama wa Taifa ni sawa na kusema usalama wa Rais, kwani democrasia yetu haimpi mwananchi nguvu ya kutawala, bali inampa mchaguliwa nguvu zote, thus na vyombo vyote vinakuwa vya kwake na sio vya wananchi.

Hii ni kusema kwamba, kwa mtindo huu hatuna utumishi wa UMMA, kwani waajiriwa wengi huwa hawamwogopi mlipa kodi, bali wanamwogopa mkusanya kodi, na wako tayari kutekeleza kila atakachoagiza hata kama kinakiuka sheria.

This is terrible na katiba itakayoundwa bado itaendeleea kuwaenzi political leaders wakati wananchi wanakunya moyo
 
Sitegemei maamuzi yoyote ya ajabu ambayo yatafanyika Lowassa hawawezi kumgusa hilo hata Kikwete mwenyewe anajua zaidi ya hapo zitaishia kupigwa soga na maamuzi ambayo mostly utasikia wamewapa onyo kali UVCCM.
 
Lolote litakaloamuliwa Dodoma, nimeshajua kuwa Kikwete hana ubavu wa kumvaa Lowasa. Inawezekana ni kuheshimu historia yao kisiasa pamoja au ni kwa sababu ya kumwogopa kwa kigezo chochote kiwacho.

Tatizo lililoko hapa siyo la Lowasa kuwa gamba bali ni la Kikwete mwenyewe kushindwa kujua anataka akipeleke chama chake wapi. Haja yake ilikuwa ni uraisi kusudi apate mianya ya biashara mbalimbali kwa ajili ya familia yake na ndugu zake, na vile vile kupata mwanaya wa kuitembelea dunia nzima.

Alipoanza madaraka hayo alisema kuwa yeye siyo mfanya biashara na wala hana mpango wa kuanzia biashara ukubwani ingawa ana shamba la mananasi tu kule Bagamoyo. Leo hii sidhani kama bado anaongea hivyo tena, na sabau ya kushindwa kusema hivyo huenda ndiyo inayofamya aone ugume wa kumvaa Lowasa.

Great power comes with responsibilities; hapa tuna mtu aliye na power lakini hataki responsibilities!!

Hivi, JK anamvua gamba EL kwa uchafu alionao au kutaka kujisafisha kwa umma?
Nani mchafu zaidi kati ya EL na JK?
 
Hii ni habari ambayo watu wameichangia usiku wote. mtoa habari asante kwa umakini wa kutoa maelezo ya kina. Tunakusubiri zaidi asubuhi hii, ni nini mwisho wa filamu hii?

Hakika, naona watu wamekuwa hewani kwa mda mrefu. Tunasubiri update za leo siku ya jua(sunday)
 
Mbona kuna rais wa mashabiki wa New Castle United Tanzania
Natabiri
- Lowassa atang'oka. Kung'oka kwake kutaleta mpasuko mkubwa CHADEMA wengine wakitaka aalikwe CHADEMA na wengine wakiapa "over my dead body".
- Sitta atapewa karipio kali, na kwa kuwa ni ndumilakuwili ataufyata.
- Chenge is not as powerfull as those two, yeye ataondolewa kirahisi na haraka sana.
- Itapangwa mikakati mikali ya kuhakikisha SUGU anang'oka Mbeya kwa hali na mali, haswa baada ya kuitwa Rais wa Mbeya.
 
JK, rais na CCM chairman, enough is enough. Hakuna nchi inayoendeshwa huku watu walio nje ya serikali wakicontrol sehemu kubwa ya mamlaka.

Yaani Jk ameacha nchi imefika watu wanapledge allegiance kwa Lowassa na kumtetea waziwazi EL against Jk na kuendelea kupeta. Hell no, haiwezekani hata kidogo, kwa sababu je EL akiamua ambadilishe Jk itakuwa vipi??

Usalama kazi yake kubwa ni kuprotect institution ya Presidency, sasa usalama gani huu EL anaendesha nchi nje ya mfumo waziwazi??

Tutajua ukweli kuhusu mwelekeo wa nchi hiyo next week mungu akitupa uzima.

May Almighty God Bless Tanzania.
Mkuu nashangaa ulichoandika as if haujui kinachoendelea nchi hii
 
usife moyo talifa zako tunazihitaji kama mgonjwa aliye pungukiwa damu.usisite kutujuza hata kama ni neno moja
 
Hivi, JK anamvua gamba EL kwa uchafu alionao au kutaka kujisafisha kwa umma?
Nani mchafu zaidi kati ya EL na JK?
Mkuu hapo hakuna msafi na wote wanajua. Kama NEC CCM ingekuwa angalau na nusu ya wajumbe wasafi ingekuwa rahisi kumtosa EL. Sasa hawana uhalali wa kufanya hivyo maana hakuna msafi.
 
zaidi ya kumpongeza mkulu kwa hotuba ya wazee na pia bunge kupitisha muswada wa katiba wataongea nini?
 
Kuna taarifa kwamba, vikao vya awali vya CCM mjini Dodoma vimeanza kwa kuwahoji vijana kadhaa wa UVCCM wanaotajwa kuwa karibu na Watuhumiwa wa ufisadi walotakiwa kujivua gamba.

Haijafahamika kama vijana hao watakua kafara la baba zao ama ndio kipima joto cha maamuzi magumu yanayotarajiwa kufanywa wiki hii. Hakika mwandishi mahiri wa makala katika Raia Mwema alisema, "mbele giza nyuma kaburi" na sasa uamuzi wa kurudi nyuma ni CCM kuingia kaburini na kwenda mbele ni gizani maana magamba yana nguvu za ajabu na kila kukicha yanakua magumu.

Je, CCM itaamua kuingia gizani kuvua magamba ama kurudi nyuma na kuyaacha iwe ni kaburi la CCM?

Taarifa zaidi baadae.

Mkuu! Lete Updates! Tunakutegemea,ingali tunatambua unaweza ukawa umekesha lakini MUNGU atakujaza nguvu amuka na utupe UPDATES Mkuu we2! Thankx!
 
Ni kweli hakamatiki ana watu wengi sana hapo Dodoma ambao wamesombwa kutoka maeneo mbalimbali kucheza filamu kama ile ya Igunga ya kulia na kugaragara akivuliwa gamba!!!

Millya & Group at work. Jambo la msingi ambalo siwezi kushangaa na kumtisha Mwenyekiti wao na akatishika, japo sasa naona kama mkali kidogo. Kama nilivyosema awali, "mbele giza nyuma kaburi", wakiwavua watakua wameamua kwenda gizani maana hakuna ajuae kwa hakika plan 'B', 'C' na 'D' ya ENL, na pia hakuna ajuae yatakayotokea, lakini giza haina maana hakuna njia, ni kwamba tu hakuna mwanga ila njia ipo, lakini kurudi nyuma mwanga upo kuwa ni kaburi la uongozi wa juu wa CCM chini ya Kikwete na ushindi mkubwa kwa ENL na kundi lililo "tiifu" kwake, ambalo linaendeshwa kama 'serikali ya pembeni' maana lina bajeti iliyotuna,

lina watendaji mahiri, lina vijana 'watiifu' wanaofanya kazi usiku na mchana na humu JF wamejaa tele, wana vyombo vya habari na waandishi wa habari wengine na kikubwa kabisa na cha hatari wana mfumo hatari sana ambao uko kazini wakati wote na baadhi wamo ndani ya mfumo halali, na ingekua nchi nyingine hawa wangeitwa 'magaidi' maana 'mchana wanamulika, usiku wanachoma'.

Hawa 'magaidi' ni vigumu sana kuwatambua maana baadhi wanajifanya watiifu sana kwenye mfumo halali, baadhi wanajifanya hata kushambulia na kuhujumu kundi la ENL kiana. Haya yote JK anayajua, watu wake wa Usalama wanayajua, ndio maana nasema lolote laweza kutokea kama mkuu atasema, "sasa imetosha" kauli ambayo kwa sasa iko kinywani mwake.

Nani aliyewaloga na kuwaaminisha kuwa Lowasa akivuliwa gamba ndo mwisho wa matatizo CCM? What about the Ngelejas, Kafumus you can add to the list!!
 
Nimejifunza jambo moja hapa dodoma kuwa lowasa hakamatiki kabisa; maana kwanza anawatu wengi

Hata Papa Upanga ana nguvu za ajabu akiwa baharini. Ukimleta nchi kavu baada ya muda mfupi ataanza kutapatapa na hatimaye kufa.

Tafakari!
 
Nani aliyewaloga na kuwaaminisha kuwa Lowasa akivuliwa gamba ndo mwisho wa matatizo CCM? What about the Ngelejas, Kafumus you can add to the list!!

Kila hesabu huanza na 1,2,3.... Huwezi kuanza na 5,6,11...
 
Hata Papa Upanga ana nguvu za ajabu akiwa baharini. Ukimleta nchi kavu baada ya muda mfupi ataanza kutapatapa na hatimaye kufa.

Tafakari!
Una maana Lowassa akija Chadema hatutampokea? Atakua hana maana? Hatokisaidia chama kama Sabodo? Si ana wafuasi wengi wataipandisha chati Chadema?
 
Sasa hivi tuna serikali mbili wala hili halina ubishi!. Moja inaongozwa na JK toka Magogoni, na nyingine EL from anywhere. Wakubwa hawa wanajuana vilivyo na kama mmojawao alivyosema 'wahakukutana barabarani'. Kila mmoja ana wabunge wa kutosha, mawaziri, wanachama katika jumuiya zote za chama na mbaya zaidi kila mmoja ana team nzuri kwenye usalama wa taifa.

Kauli kama ile ya Pinda bungeni kuwa nchi iko shwari sio kweli maana hata kwenye maandamano ya CHADEMA polisi wanapopiga watu na kuuwa si kwamba wanawapiga CHADEMA ila in their mind wanapambana na kundi pinzani la mkubwa wao! Maneno kama yale ya Wassira kwamba CHADEMA wanatumiwa ni kielelezo kwamba wanahofu kundi kundi liko nyuma ya CHADEMA.

Hii inanifanya nijiulize, hivi hii katiba mpya wanayong'ang'ania kusimamia kutengeneza itakuwa ni ya ccm ipi? CCM ya magogoni au ccm ya mtaani. Hata kama JK atasema kwa sasa yeye na upper hand lakini kwa historia yake (6yrs now) ni kweli anaweza kuzuisha ccm kutoingilia mchakato? Je, wananchi wa Tanzania wako wapi kwenye hili?
 
Una maana Lowassa akija Chadema hatutampokea? Atakua hana maana? Hatokisaidia chama kama Sabodo? Si ana wafuasi wengi wataipandisha chati Chadema?

Hahahaa you make a good point, ingawa to me i can smell some undertones of sarcasm. Wapambanaji wa ufisadi CHADEMA wampokee S.I Unit(I like this) ya ufisadi!!!... But under the sun never say never.

By the way, sijui mkuu una ratiba ya series za vikao vya MAGAMBA vinavyoanza this weekend. Naomba nijue NEC
yenyewe wanakaa lini?
 
jamani jamani what if hii ni mbinu ya EL na JK pamoja?.. JK anamaliza muda wake 2015, EL anakuwa vipi tishio la JK ikiwa hakusudii kuchukua ama kupindua nchi..Na hakuna kitu kizuri kama kuonyesha Upinzani na rais aliyeko madarakani ktk kujiongezea umaarufu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015..Nafikiri mchezo unachezwa kuonyesha EL na JK wana mahusiano mabaya wakati EL akiandaliwa kwa ajili ya 2015 na hivi sasa ukimwondoa EL hakuna mtu CCM anayepata umaarufu zaidi ya EL - WHY?...

Binafsi sidhani kama JK anajali tena CCM maanake kisha ona jinsi wasivyompenda na ndio maana yupo radhi kuzungumza na wazee badala ya vikao vya chama but EL has been there for him all the time ...Binafsi, I think we've been played big time! msemo wa Mwanakijiji tunaicheza ngoma yao.
 
jamani jamani what if hii ni mbinu ya EL na JK pamoja?.. JK anamaliza muda wake 2015 EL anakuwa vipi tishio la JK ikiwa hatachukua ama kupindua nchi..Na hakuna kitu kizuri kama kuonyesha Upinzani wa urais ulotangulia kujiongezea umaarufu kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015..Nafikiri mchezo unachezwa kuonyesha EL na JK wana mahusiano mabaya wakati EL akiandaliwa kwa ajili ya 2015 na hivi sasa ukimwondoa EL hakuna mtu CCM anayepata umaarufu zaidi ya EL - WHY?.

Binafsi sidhani kama JK anajali tena CCM maanake kisha ona jinsi wasivyompenda na ndio maana yupo radhi kuzungumza na wazee badala ya vikao vya chama.. Binafsi, I think we've been played big time! msemo wa Mwanakijiji tunaicheza ngoma yao.

Uko sahihi Mkuu, tunaweza kucheza ngoma yao, lakini kibaya zaidi ni kucheza ngoma ya kutetea mafisadi. Ni bora kama ngoma yao ni huko kugombana na kaka mazingira ya sasa Lowassa hawezi kupata umaarufu kwa kufukuzwa chama kwa ufisadi, angekua kama Sitta akifukuzwa kwa kupiga vita ufisadi, angepata umaarufu.

Mrema alipotoka CCM alikua na jina la mtu anayetetea wanyonge na mpiga vita ulanguzi na wezi, now Lowassa akitoka ama kufukuzwa anatoka kwa jina la wizi si utetezi, na ndio maana juzi aliibuka kujifanya anatetea ajira kwa vijana na hali ngumu ya maisha ili ajulikane kama mtetezi wa wanyonge.

Ratiba ni kwamba jana na leo Kamati ya Maadili inakaa na jana ndio iliwaita vijana kadhaa wa UVCCM na wote ni wale wa upande wa Lowassa, kesho ni Kamati Kuu kabla ya NEC, Jumanne na Jumatano.
 
Back
Top Bottom