Sina hakika kama huu ni "mwandiko na fikra" toka moja kwa moja kwa Tundu Lissu!
Mpumbavu yeyote, hata hao maadui wanaomnyanyasa Tundu Lissu wanaweza kuandika chochote humu JF kupima upepo unakovumia.
WaTanzania "hawalali na hawatalala". Ni juzi tu wazalendo wameweka damu yao chini kurutubisha ardhi hii isinajisiwe milele. Hawa huwezi kusema walilala; mapambano ndiyo kwanza yameanza.
Kunyanyaswa kwa Tundu Lissu ni sehemu na kichocheo kitakachozaa ukombozi wa taifa hili.
WatTanzania hawatalala; watasimama na Tundu Lissu mpaka ukombozi kamili utakapopatikana.