Erick_Otieno

JF-Expert Member
Mar 28, 2010
624
1,020

Wakuu salamu,

Nataka kuanzisha kilimo cha umwagiliaji cha kitunguu. Naomba ushauri wenu ni maeneo gani yanayoofaa kwa kilimo cha kitunguu na hasa ambayo yanaweza kuwa na maji kwa ajili ya umwagiliaji.

Nimenunua power tiller ambayo nategemea itanisaidia sana kwenye kilimo cha umwagiliaji!
Kilimo Kwanza!


BAADHI YA WADAU WANAOHITAJI KUELEWA KILIMO HIKI
Wandugu nimeamua kuingia kwenye kilimo,ninawaza kuanza na kitunguu saumu,..naomba mnijuze wapi panafaa kulima?gharama ya kutunza hekari 1,muda mpaka kukomaa, . Pili nafikia pia maharage ya kijivu(ya mbeya) detail zake pia,, asanteni.
Wadau naombeni ushauri wa kulima kitunguu kwa yoyote mwenye uzoefu na hiki kilimo.napenda nijue mahitaji na gharama kwa heka 1


MICHANGO YA WADAU KUHUSU KILIMO HIKI
 
Realtor,'

Kuna sehemu fulani inaitwa ruaha mbuyuni, hapo bwana kilimo hakitegemei mvua, kitunguu kinakubali sana hapo mpendwa, vilevile uzuri wa hapo ni kwamba unawezakulima vitunguu marambili kwa mwaka, ukitoa kitunguu unaweza kulima mahindi mara mbili na maharage mwaka huo huo mmoja. Yaani ardhi ya hapo inakubali karibu kila kitu na serikali imeshapaendeleza.

Ukiweza kupapata hapo utafaidika sana lkn bei sio zile za elfu 50 kwa hekari, bei hapo ni kubwa na ni vigumu kidogo kupata eneo maana tayari mabebari tumeshayakamata (kidding).

Ni-PM kama unataka maelezo ya zaidi naweza kukusaidia.
 
Last edited by a moderator:
cheusimangala

Seconded.

Kijiji kinaitwa msosa to be precise. ni tarafa ya mahenge i think Wilaya ya Kilolo. Au ukiwa unatokea Dar kwenda Iringa opposite aljazeera hotel on your left. Kuna mifereji kabisa ya umwagiliaji. Nilikuwa huko last month, it's terrific, we nenda utapata mashamba ya kukodi and it pays.

Good luck.
 
Last edited by a moderator:
Shukrani Cheusimangala...Hawa mabebari:smile-big: tutabanana nao!

Sisi mabepari utatuweza lakini? Au unasema!

Kama unataka kwenda Ruaha Mbuyuni kwa ajili ya kitunguu nenda, ukiweza nenda Kibakwe Mpwapwa pia kuna bonde zuri sana na wanalima pia kibiashara. Nenda Mbeya vijijini kuna kitunguu cha kufa mtu au kajichanganye Karatu( Mang`ola),

Maeneo hayo bei ziko juu,kama hutajali nenda kafanye survey bonde moja huko Kipatimu,watu wanalima vitunguu pia,huko bei ya ardhi inaweza kuwa karibu na bure.

Shime nenda shambani leo usingoje kesho.
 
Pia jatribu kwenda mkoa wa pwani. Ukivuka daraja la mto ruvu mbele kama 1 kilomita (nadhani zamani palikuwepo na ranch ya napco) pinda kulia - nenda kama kilometere kumi hivi/pia ulizia wakazi utakutana na wanakijiji amabao watakuelekeza wapi hasa pana mashamba ya kukodi au kununua. ila chunga matapeli.

Kila la kheri.
 

Well said bro (hapo pekundu)

Maeneo hayo ni hatari, kama hela zako ni za kuungaunga, yaani kama unanunua eneo kisha upate muda mwingine wa kutafuta uwezo wa kuliendeleza, utaishia kulia. Ruvu kwa sasa inatakiwa uwe na uwezo, unanunua na kuendeleza eneo lako mara moja.

Ila usiogope, ni ushauri tu.
 
Hii ya matapeli ni tatizo kubwa sana kwenye kununua ardhi. Nilishawahi kuuziwa heka 8 na serikali ya kijiji pale mlandizi ukienda ndani karibu na reli ya kati, baadae likawa na kesi kati ya vijiji viwili wanaligombania. Nashindwa kuelewa ni namna gani tunaweza kuudhibiti huu utapeli.
 

Malila unaweza kunipa mwanga kidogo kuhusu bei za hayo maeneo ya Ruaha na hayo mengine kama unafahamu. Nataka nikasurvey na angalau kabla sijaenda huko nijue bei ya kununua kwa eka au ya kukodi kwa eka.

Kilimo Kwanza!
 
Malila unaweza kunipa mwanga kidogo kuhusu bei za hayo maeneo ya Ruaha na hayo mengine kama unafahamu. Nataka nikasurvey na angalau kabla sijaenda huko nijue bei ya kununua kwa eka au ya kukodi kwa eka.

Kilimo Kwanza!

Kwa maeneo hayo sijapata kutafiti bei zikoje,ila naona dada Cheusi anaweza kukusaidia kupata bei hizo kwa maeneo yale. Mimi nitapita maeneo ya Ruaha,nitajaribu kuuliza bei zikoje.
 
Malila hongera kaka kwa juhudi zako Mungu atakusaidia ndugu yangu nakuombea lakheri nimekukubali nimtaftaji hakuna sehem usoijua na malezoyako niuwazi bilashaka mtuasipo kuelewa atkua namatatizo naham yakukuona hoja zako zimenipa faraja na kujiamini, nisikupendele sana kuna wengi manyusi, cheusimangala, Dick, nawshukuru sana nifaidika sana na ushauri wenu bila ya ninyi kujua mungu awalinde kwa afianjema muiwezeshe jamii.

Malila naomba mualiko katika vikao vyenu mkuu.

Mbarikiwe sana
 
Mkuu Malila naomba na mini nisiwe mchoyo wa kutoa shukrani zangu!

Kwa kweli nimekuwa nafurahia sana mchango wako na umekuwa muwazi sana, na hivi ndo wajasiriamali wa Tanzania tunatakiwa tuwe! big up saaaanaaaaa!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…