Kilimo cha kisasa cha maembe

KUBOTA,

Tembea uone, hasa wakulima kuona ndio kuamini. Kuna hata parachichi kubwa kama mti wa mchungwa unazaa embe hadi elfu tano sikuamini mpaka nilipoona, mti huo wa parachichi unaanza kuzaa baada ya miezi 16, tunda lake(parachichi) linaweza kukaa hadi siku 21 bila kuoza kwenye mazingira ya kawaida (nje ya fridge). Nenda wilaya ya SIHA kwenye shamba la AFRICADO LTD utaona.

Kwa upande wa embe kati ya mwaka wa 3 hadi wa 7 ndio inafikia hiyo potential na kama pruning yake inafanyika vizuri
usiuachie ukue mkubwa kama mnayofanyia vikao vya kijiji. Reccommended height sio zaidi ya 5m.
Yapo mashamba mengi na kwa bahati mbaya hukuweza kuhudhuria week ya kuonja embe ilifanya mnazi mmoja week ya kwanza January mwaka huu ungepata maelezo zaidi.

Hivi Mapalachichi yanastawi kwenye ukanda huu wa pwani?

Miche inapatikana wapi?
 
Ukiwa Morogoro huwezi kupotea. ni kambi ya jeshi lakini wana garden matata sana na kumbi za sherehe. Uliza mtu yeyote. Ni kama Km 5hivi toka njia panda ya SUA, uelekeo wa SUA.
Siku za nyuma nilito ushauri kuhusu miche ya miembe, kwa bahati mabay sikuweza kusoma maoni yaliyo nitaka nitoe contacts zangu kwa wakati.

Nipo tayari kuchangia yale ninayo yajua katika kilimo cha embe na nitarudi na majibu kwa maswali yalioyo ulizwa ingawa siku zimepita kidogo. Hato hivyo msimu wa kupanda umeisha maana mvua ndo zimeisha hadi mwakani. KWa anayetaka kunitumia email tumia info@noveltz.org nitajibu mail yako. Au nipigie 0715571343
 
Hilo jibu hapo chini ni location ya shamba la miembe , nikimjibu muuliza swali
 
Kama jamaa atachelewa kutoa contacts zake, mtwangie huyu jamaa wa SUA, kwake kuna miche ya matunda hadi karanga miti 0712099434 au hapa Dar mtwangie huyu 0784284800, wote wana vitalu vya uhakika. Yule wa pale Mapinga sina simu yake, lakini naye yuko vizuri.

Malila,

Huyo wa Mapinga contacts zake zingepatikana ingekuwa poa sana maana mi napita sana pande hizo
 
Ukiwa Morogoro tembelea Magadu Officers mess. Ni club nzuri sana na wana garden ya maembe kama ekar 2. pale utakosha macho yako.

Bro hakuna kitu kinachoitwa garden ya maembe. Inaitwa mangoes orchard. All in all unayosema ni sawa magadu jeshini wamejipanga kuna jamaa yangu m1 nilimaliza nae Horticulture SUA anaitwa lucas yupo hapo.
 
Miaka mitatu, hapo utapata kiasi tu, miaka mitano ndo unaanza kupata faida kamili, hapo ndo unaweza kupata hadi matunda 3000 kwa mti mmoja

Miaka mitatu maembe 3000? hii inatia mashaka maana vimuembe vyenyewe havina hata kimo mazee.
 
Asante mheshimiwa! Maelezo yako yanatoa mwanga na ninaiona picha ya kilimo hiki vizuri. Ninavutiwa sana na kilimo cha miembe! Nitakutafuta unielimishe zaidi sina uzoefu na hasa uzaaji wa miembe hasa hii aina ya miembe ya kupandisha (grafted). Hivi unayajua mashamba ya miembe ya kupigiwa mfano ambayo ninaweza kwenda kujionea nikavutiwa, yako maeneo gani?

Mkuu upo mpaka huku??

Vipi matanuru yako ya kuchoma mka mkuu bado unaendea nayo???
 
Mkuu upo mpaka huku??

Vipi matanuru yako ya kuchoma mka mkuu bado unaendea nayo???
Kaka matanuru ya mkaa yamenifikisha level nyingine, nimeagiza mashine ya kutengenezea mkaa unaotokana na pumba za mpunga (rice hull briquettes), nimechoshwa na kelele za bwana miti. Nitakuwa na-pack fresh na kusambaza hadi supermarkets. Kaka kwenye biashara ya nishati hakuna anayelala njaa kuanzia muuza kuni, mkaa, gesi, petrolleum products hadi Tanesco, nishati ni pesa mara moja !! Aaah sitasahau matanulu........
 
Kaka matanuru ya mkaa yamenifikisha level nyingine, nimeagiza mashine ya kutengenezea mkaa unaotokana na pumba za mpunga (rice hull briquettes), nimechoshwa na kelele za bwana miti. Nitakuwa na-pack fresh na kusambaza hadi supermarkets. Kaka kwenye biashara ya nishati hakuna anayelala njaa kuanzia muuza kuni, mkaa, gesi, petrolleum products hadi Tanesco, nishati ni pesa mara moja !! Aaah sitasahau matanulu........

Mkuu i salute you!ndicho nachoweza kusema
 
Naomba kujua jinsi ya kupanda mmea wa emba hasa umbali kutoka mmea mmja hadi mwingi, ni mita ngapi?
 
naomba kujua jinsi ya kupanda mmea wa emba hasa umbali kutoka mmea mmja hadi mwingi, ni mita ngapi?

Mkuu kama utakuwa na Muda nenda SUA pale morogoro. Wana kitengo chao cha miti. watakupa shule ya kutosha pamoja na aina bora ya miche. wanatoa ushauri bure kabisa
 
Naomba kujua jinsi ya kupanda mmea wa emba hasa umbali kutoka mmea mmja hadi mwingi, ni mita ngapi?

Suala lolote la kilimo ndugu linategemea na uliko,hali ya hewa na aina ya miembe pia kuchagua aina ya miembe itategemea dhumuni la kupanda hiyo miembe na eneo ulilonalo,so swali lako haliko kamili kwa urahisi watumie wataalam wa kilimo walioeneo lako maana

nitakuelekeza fika chuo cha kilimo Tengeru utapata ushauri na miche ya miembe ya kuungwa aina kama Tommy Atkins halafu kumbe wewe uko Mtwara ikawa kazi nyingine ndugu pia naweza kukuelekeza miembe ya kupanda sijui udongo wala hali ya hewa ya uliko inakua ngumu sana hapo
 
Wakuu

Nimepita Kibiri kwenye kile kikundi cha wakulima wa kitalu cha embe. I tell you wako vizuri saaaaaaana kuliko hata nilivyo tarajia.

Wameanzisha kampeni yao ya '' Lima miti kumi ya embe upate Shillingi millioni moja. Kampeni yao ni kwamba nunua miche kumi (30,000) chimba mashimo na kuweka samadi (5,000x10= 50,000), mwagilia kwa mwaka ni assumption dumu moja miche 5 na dumu moja la maji ni TZS 300 na kwa wiki nyeshea mara 2 (2x2x300x52 = 62,400) na garama nyinginezo 30,000. Jumla 172,400

Mapato: kila mti unayo potential ya kuzaa hadi embe 3,000 kwa msimu lakini wao wamechukua average ya 500/tree
hivyo unaweza kupata embe 5,000 kwa miche kumi na kila mmoja unaweza kuuza kwa sh 300 = 1,500,000 ukitoa garama laki 2 unapata faida ya sh 1.3million minimum.

Eneo kwenye compaign yao wanasema hata kama kuna eneo la bustani kima 5 meters kuzunguka nyumba yao unaweza kuotesha embe utapata kivuli lakini pia matunda yake ni fedha.

Naomba tuwaunge mkono. wao ni wakulima wadogo wa miche bora ya embe (Dodo, bolibo, Tommy, Keit, Kent, Alfonso, red Indian, Palmer, n.k) pia wanatoa ushauri kwa kweli nimevutiwa nao saaaaaaaaaaaaaana.
sikutarajia kama ningeweza kupta elimu niliyopata kwao, ukipata nafasi ya kuwa KIBITI

please pita kwenye hiki kikundi ujionee.
Naweza kupata mawasiliano yao
 
Back
Top Bottom