Ndugu CDM,
Nawasifu sana kwa mkutano huu. Lakini napenda kuwaomba kwanza kufanya tathmini. Idadi hiyo niliona hapo ni ndogo sana. Hatuwezi kuanzisha move kama hii. Haitatusaidia maana vichaa polisi watakapofika watauwa watanzania bure. Tafadhali naombeni fuateni tu sheria hata kama ni mbovu tumieni tu hizo sheria mbovu naamini mtawashinda. Ukiangalia Msiri, libya, na Tunisia idadi ya watu ilikuwa kubwa na watu walijitolea kweli kweli. Tanzania bado na watu wengi hawaungi mkono mbinu hii ambao watu wengi huenda wakapoteza maisha yao. Ukweli ni kwamba nina wasiwasi hata viongozi wetu wata wekwa ndani na hapo ndo itakuwa mwisho wa pilika pilika hizo.
Nawa sihi sana acheni kushabikia hii hali maana tanzania bado hatujafikia hali ya kukata tamaa kiasi cha kushinda tukiandamana.