uran
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 18,420
- 30,743
- Thread starter
- #41
Good Analysis mdau.Nilichojifunza kwenye Kili Marathon na NBC Dodoma Marathon
Kwanza, Hawa wote wawili huwa wanatumia barua ( Official Letter) kwa Taasisi na Idara zote za Serikali ya JMT pamoja na Makampuni Binafsi Makubwa kuomba Wafanyakazi wao waweze kushiriki ukiwa pamoja na kuwalipia ada za ushiriki na posho za safari.
Ikumbukwe kuwa Taasisi za Serikali na Makampuni Wana Sera za Corporate Social Responsibility ( CSR) Kwahiyo kupitia fungu hilo la bajeti husaidia kuwawezesha watumishi wa Serikali na Makampuni Binafsi kushiriki.
Kili Marathon huwa anaonekana kinara kutokana Hana MPINZANI au mshindani wa biashara yupo Neutral lakini ukija kwa haya Mabenki kama imeandaliwa na NBC usitegemee Wafanyakazi wa Benki zingine kushiriki kwa maana hao wanaonekana ni washindani wao
Sasa kwa Upande wa NBC pia hamasa imetokana na ushiriki wao wa kufadhili ligi kuu ya Tanzania, ambao mashabiki wengi wa Moira wa miguu wamejitokeza na walioteka sehemu mbalimbali kwa sababu Dodoma ipo katikati ya nchi kwahiyo ni rahisi mashabiki wa Mpira wa timu mbalimbali kujichanganya na kukodi Coaster kutoka Tabora, Singida, Morogoro, Iringa, Tanga, Mbeya, Manyara, Arusha, nakadhalika kuweza kusafiri na kushiriki hiyo Marathon
So hapo Kili ni super?