Inaendelea
Kiukweli ni kwamba nilisizi, Lakini Sikuwa pekeyangu karibia wapangaji kama wane hivi walitoka vyumbani mwao
Mimi sikurudi tena kulala mule ndani nilichukua kibegi changu na kwenda kukesha Ibiza mpaka alfajiri nilipotimkia bandarini
Tukiwa kwenye boat kurejea Nyamisati story zilikuwa za ile gesti na vituko walivyokumbana navyo usiku mzima, hasa ile harufu ya udongo mbichi na mchele, kuna baadhi walijiapiza kuwa hawatakaa warudi Mafia
Tulifika Nyamisati saa tatu hivi asubuhi bila kituko chochote....nilipumzika mpaka mchana tulipokodi fiber boat kwenda kwenye visiwa vilivyo karibu na hapo Nyamisati
Sorry kwa kupotea hewani si kweli kwamba jitu refu lilinitumbua...
Tuendeleee
Pale Nyamisati kuna fiber boats nyingi za kukodi ila sisi tulipata shida kweli kupata moja, mwishowe kijana mmoja akatuambua boat inayotufaa sisi ni ya jamaa anaitwa rasta nyoka
Basi akatafutwa na ndani ya dakika kumi akawa kafika
Huyu jamaa ni mrefu mweusi mwembamba mwenye rasta zilizofungwa kitambaa kote ndefu karibia na kiuno
Tulipatana na kuondoka Nyamisati saa saba mchana, nilikuwa nimeshamweleza kuwa tunataka kufanya ziara kwenye visiwa visivyopungua kumi, akasema hakuna shida kwakuwa kote anakufahamu vema
Ni baada ya kupanda ile boat na kuondoka pale ndio mwili wangu uliota vipele kwa taharuki, na hii ni baada ya kusikia ile harufu ya udongo na mchele, nilimwangalia nahodha wetu kwa kuibia na kugundua ni yule yule bwana
Hata wale raia niliokuwa nao niliweza kuona hofu ya wazi kwenye nyuso zao! Tuliangaliana wote bila kuongeleshana chochote
zile harufu za udongo na mchele zikawa zinakuja na kutoweka hapo tayari tukiwa kwenye mapori ya mikoko ndani ya bahari kuu
Ilibidi niweke hofu pembeni na kuanza kuongea na nahodha! Hakuwa mtu wa kawaida anafahamu mengi ya bahari mengi sana na ilikuwa akipiga story ya kutisha kuna wakati alikuwa anarusha mate kama nyoka...hii niliishuhudia si chini ya mara kumi
Visiwa hivi vilivyoko karibu na Nyamisati karibia vyote vimezungukwa na mikoko na kwa baadhi ya sehemu kuna vijiji na kwingine kuna kambi za uvuvi na kilimo, ni visiwa ambavyo viko naweza kusema nje ya utaratibu wa dunia, huko dili kubwa ni uchawi na kusafirisha mikoko
Rasta nyoka nahodha wetu ni mtu maarufu huko huko visiwani lakini unaweza kufika Nyamisati ukawaulizia kuhusu yeye na hakuna mtu anaweza kukiri kumfahamu! Yeye ndio mwamuzi wa kutaka akumbukwe au adahauliwe
Tulikuja kuweka kambi kisiwa kimoja kinaitwa Kilwani karibu na meli kubwa ya wajerumani iliyoachwa hapo wakati wa vita ya pili ya dunia, kwasasa haionekani tena imezama kabisa