Kile kipindi ambacho nilipotea

Kile kipindi ambacho nilipotea

Nilirejea Nyamisati kutoka pale gezani bandari bubu jioni ya siku hiyo, nikiwa na mipango ya kwenda Mafia lakini kufika pale nikakuta boat jahazi imeshajaa hivyo nikapewa matumaini ya kuondoka mchana wa kesho yake kulingana na mahitaji ya abiria kuwa wengi
Inaendelea......
Kwa bahati nzuri siku ile ya pili (sitataja tarehe)abiria wakawa wengi hivyo ikabidi kile chombo kilichoondoka alfajiri kigeuze
Bandari ya Nyamisati sio user friendly, ili uweze kupanda chombo inakubidi uchumpe kwenye mawe yaliyoko juu ya matope na ngazi ya chombo ni mbao ambazo tayari zina majimaji na tope
Ndani ya chombo hakuna siti kuna mabenchi machache tu hivyo watu hugombania kupanda ili kuwahi sehemu ya kukaa
Mimi niliwahi kupanda na kupata seat ya benchi katikati ya chombo bila kuteleza wala kupata dhahama za matope
Abiria walikuwa wengi na walipanda kwa kugombea ili kupata sehemu ya kukaa (safari ya kutoka Nyamisati mpaka Mafia ni masaa mane)kama bahari ikiwa imetulia
Ni wakati abiria wote wameshapanda na karibia nusu wakiwa wamekosa sehemu ya kuketi aliingia yule mtu mrefu na mavazi yake yaleyale na akaenda mbele kwenye benchi la mwisho kabla ya sehemu ile ya nanga akakaa
Hiki kitendo kiliwashangaza wengi kwakuwa hakuna aliyedhani kuwa pale kuna nafasi, tulisafiri salama mpaka mafia huku tukipiga story za kawaida za kufahamiana ndani ya chombo
Huyu ndugu huyu hakuongea na mtu wala kufunua uso wake kuanzia mwanzo wa safari mpaka mwisho
Kwa kawaida mnapokaribia kumaliza safari nahodha hukagua upya tiketi na kuzikusanya, kwenye hili zoezi yule ndugu hakuguswa kabisa, niliona kwa macho yangu hilo (nilidhani ni stuff, nilikuja kumuuliza nahodha tukiwa Mafia lakini akakataa kata kata kuwa na abiria wa namna hiyo chomboni
 
nadhani lifunguliwa kundi ka wapenda story zas kichawi ok? ilo kundi mshana jr awe kiongozi, kiu kweli uchawi unaitajika hasa katika kipindi km iki cha utawala wa jiteni tunatoana vishipa tu ili mjifunze kuheshimu wat km ssi marc,
 
nadhani lifunguliwa kundi ka wapenda story zas kichawi ok? ilo kundi mshana jr awe kiongozi, kiu kweli uchawi unaitajika hasa katika kipindi km iki cha utawala wa jiteni tunatoana vishipa tu ili mjifunze kuheshimu wat km ssi marc,
 
Shusha vitu Mkuu mshana jr sijui mwenyewe unajiweka kwenye kundi lipi Mkuu? La warozi au washirikina? Nitarudi kuja kusoma vikianza kutisha nitasepa zangu si mtihani huu ili nisome kila kitu.

Nimetamani kusimulia hiki kisa muda sasa lakini waungwana walikuwa hawajatoa ruhusa bado
Nilipotea kwa vipindi viwili vyenye jumla ya siku 23, kati ya siku hizo ni siku chache sana nilikuwa nje ya Tanzania, nyingine zote nilikuwa hapa hapa ila kwenye dunia isiyoaminika na wengi, dunia ya ushirikina na uchawi katika uhalisia wake
Nitangulie kuomba radhi sitaandika kila kitu bali yale ya muhimu tu nitakayoona ni muhimu kuandika
Nilitoka Dar kwa dharura kuelekea sehemu ambako nitapata kile kinachonipeleka huko, safari yangu ikanipeleka mpaka Nyamisati, nikalala pale...
Siku ya pili asubuhi nikadamkia bandari bubu iitwayo gezani.... vituko vilianzia hapo
 
Tuendelee.....
Kile kitendo cha nahodha kumkana yule abiria ambaye hata shiva yake pale bandari ya mafia kiliniacha na maswali na tafakuri kuu! Yeye ndio alikuwa abiria wa kwanza kushuka na kwa taratibu za pale bandarini mafia gati lina urefu karibia kilometre moja (gati la vyuma)hivyo kuna magari maalum ya abiria huchukua watu kwa nauli ileile na kuwapeleka mpaka pwani! Wasiojua ama kutopenda kupanda gari hutembea kwa miguu lakini mtawapita njiani mkiwa garini
Yule ndugu hakupanda gari na sikumuona popote mpaka tunafika pwani
 
Shusha vitu Mkuu mshana jr sijui mwenyewe unajiweka kwenye kundi lipi Mkuu? La warozi au washirikina? Nitarudi kuja kusoma vikianza kutisha nitasepa zangu si mtihani huu ili nisome kila kitu.
Hahahahaaaaa BAK please don't move
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tuendelee....
Ukishuka pale kilindoni Mafia bandarini, hotel nzuri ya kwanza ambayo ni standard na bei yake ni nzuri ni IBIZA, Ni pazuri panafaa panavutia, nilifikia hapo na kuwasiliana na wana JF ambao ikiwapendeza watakuja wenyewe hapa ila kwasasa siwezi kuwataja bila ruhusa yao
Nililala Ibiza na kesho yake nikaenda visiwa vingine vilivyo karibu na mafia (nakumbuka nilitupia picha hapa bila watu wengi kujua huko ni wapi) nilishinda huko na kurejea mafia jioni ya siku hiyohoyo
Kwa bahati mbaya sana kufika Ibiza ikawa vyumba vimejaa, wapambe wa pm walikuwa wamebanana hapo kwakuwa ilikuwa ni kipindi kile Majaliwa yuko kule
Sikuwa pekeyangu niliyekosa chumba pale tulikuwa wengi, kuna gest nyuma tu ya Ibiza ila nayo ilikuwa full ya karibu vingine ilikuwa ni kama mwendo wa dk 15 na bei ilikuwa mbaya...wengi tulishindwa
Kufikia saa tano usiku tukapata kigesti change shilling 12000, vyumba sio self..nilikuwa na raia wengine wa nje tukachukua vyumba 4 kila mtu na chake
Hii gesti ilinishangaza sana
Ilikuwa ina harufu ya udongo mbichi uliochanganyikana na harufu ya ukale
Ilikuwa ni kama inaelea ukiwa ndani ni hisia isiyoelezeka
Taa zake zote zilikuwa hafifu sana
Kubwa kuliko yote ilipofika saa sita usiku(nilikuwa macho bado nafanya tahajudi)nikahisi kichwa kuvimba na nywele kusisimka..! Haikuchukua muda umeme ukakatika
Lakini pia kukawa na harufu kali ya mchele, nilichoropoka chumbani, hamad nafika kwenye korido nikamuona yule ndugu anaishia mwisho wa gesti, nilimtambua Kwa mavazi yake
 
Endelea kiongozi.....
Inaendelea
Kiukweli ni kwamba nilisizi, Lakini Sikuwa pekeyangu karibia wapangaji kama wane hivi walitoka vyumbani mwao
Mimi sikurudi tena kulala mule ndani nilichukua kibegi changu na kwenda kukesha Ibiza mpaka alfajiri nilipotimkia bandarini
Tukiwa kwenye boat kurejea Nyamisati story zilikuwa za ile gesti na vituko walivyokumbana navyo usiku mzima, hasa ile harufu ya udongo mbichi na mchele, kuna baadhi walijiapiza kuwa hawatakaa warudi Mafia
Tulifika Nyamisati saa tatu hivi asubuhi bila kituko chochote....nilipumzika mpaka mchana tulipokodi fiber boat kwenda kwenye visiwa vilivyo karibu na hapo Nyamisati
 
Back
Top Bottom