Nilirejea Nyamisati kutoka pale gezani bandari bubu jioni ya siku hiyo, nikiwa na mipango ya kwenda Mafia lakini kufika pale nikakuta boat jahazi imeshajaa hivyo nikapewa matumaini ya kuondoka mchana wa kesho yake kulingana na mahitaji ya abiria kuwa wengi
Inaendelea......
Kwa bahati nzuri siku ile ya pili (sitataja tarehe)abiria wakawa wengi hivyo ikabidi kile chombo kilichoondoka alfajiri kigeuze
Bandari ya Nyamisati sio user friendly, ili uweze kupanda chombo inakubidi uchumpe kwenye mawe yaliyoko juu ya matope na ngazi ya chombo ni mbao ambazo tayari zina majimaji na tope
Ndani ya chombo hakuna siti kuna mabenchi machache tu hivyo watu hugombania kupanda ili kuwahi sehemu ya kukaa
Mimi niliwahi kupanda na kupata seat ya benchi katikati ya chombo bila kuteleza wala kupata dhahama za matope
Abiria walikuwa wengi na walipanda kwa kugombea ili kupata sehemu ya kukaa (safari ya kutoka Nyamisati mpaka Mafia ni masaa mane)kama bahari ikiwa imetulia
Ni wakati abiria wote wameshapanda na karibia nusu wakiwa wamekosa sehemu ya kuketi aliingia yule mtu mrefu na mavazi yake yaleyale na akaenda mbele kwenye benchi la mwisho kabla ya sehemu ile ya nanga akakaa
Hiki kitendo kiliwashangaza wengi kwakuwa hakuna aliyedhani kuwa pale kuna nafasi, tulisafiri salama mpaka mafia huku tukipiga story za kawaida za kufahamiana ndani ya chombo
Huyu ndugu huyu hakuongea na mtu wala kufunua uso wake kuanzia mwanzo wa safari mpaka mwisho
Kwa kawaida mnapokaribia kumaliza safari nahodha hukagua upya tiketi na kuzikusanya, kwenye hili zoezi yule ndugu hakuguswa kabisa, niliona kwa macho yangu hilo (nilidhani ni stuff, nilikuja kumuuliza nahodha tukiwa Mafia lakini akakataa kata kata kuwa na abiria wa namna hiyo chomboni