Habari zenu,
Jaman tatizo langu ni kwamba kila nikijisomea madaftari baada ya masaa 24 nasahau nilichokisoma lakin ikifika siku ya mtihani kumbukumbu zinarudi.
Je hili tatizo linasababishwa na nini?
Je nifanyaje ili niwe nakumbuka kila mara nilichojisomea.
Asanten
Kwanza hata wenzako wanakushangaa.
Kosa la kwanza, umejiita mpalestina. Wapalestina wengi ni walemavu wa akili. BAdili hilo jina.
Pili umeongezwa mchizi. UKishakuwa mchizi huchagui uchizi. Uchizi wako unaokudandia unaanza kwenye kukamata kumbukumbu zako. Muda si mrefu utajikuta unasahau kuvaa na hata kusahau nyumban ikwenu. Acha kabisa majina ya kishetani kwa kudhani ni sifa.
Tatu, yawezekana unasoma vitu vingi kwa wakati mmoja wakati akili yako haina uwezo wa kukamata vitu vyote kwa mpigo, hivyo badala yake unapoteza. Jitahidi kuwa systematic katika kusoma lakini pia uwe na muda wa kutafkari uliyoyasoma na kama hujaelewa, utafute kuyaelewa badala ya kukariri.
Nne, yawezekana unakuwa darasani lakini akil i ziko mahala pengine ka ma Jf, michezoni, au hata katika masuala ya nyumbani, mahusiano n.k. Punguza uzingativu wa masuala yasiyo muhimu. Ondoa kichwani utitiri aw mambo masomo yawe kipaumbele chako. Vinginvyo unajichanganya.
Tano acha kusikiliza hadithi za wapotoshaji, walioshindwa shule na uache kukatishwa tamaa na watu kama bashite waliopanda gazi bila elimu. Ujue hata huyo bashite, hajisikii vizuri kuona anavurunda kila wakati. Elimu ni ufunguo wa maisha. Usikatishwe tamaa na hali ya uchumi ama mazingira uanyoyoana ya kukosa ajira n.k. Elimu itakfungua akili zako kufanya mambo mbadala kwa ufasaha na ufanisi hata kama milango mingine itakuw aimefungwa. Usipotoshwe na marafiki failures wanaokuvunja moyo. Hao ni washindwaji na hawapashwi kuwa walimu wa maisha yako. Fainali uzeeni.
Sita, jaribu kupata muda mzuri wa kutulia, kucheza michezo, kula chakula kwa muda muafaka na kulala. Mwili unahitaji balance ya vitu vingi. Usidhani kusoma mfululizo ndiyo kufahamu. Unasoma lakini pia unapata muada wa kupumzisha akli ikiwemo muda sahihi wa kulala. Panga ratiba yako vizuri.
Saba jizoeshe kula mlo uliosahihi kwa umri wako. Kuna chakula kingi sana kinauwezo wa kuimarisha mifumo y akumbukumbu kama ufuta n.k.
Lakini kubwa kuliko Yote, usisahau kuomba kwa Mungu ili azifanikishe njia zako. Kumcha Bwana Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo ni chanzo cha maarifa. Kwa heri, wengine waongezee.