SoC02 Kila maendeleo ya mtu basi kuna mtu nyuma yake kasaidia

Stories of Change - 2022 Competition

EfrahimMabena

New Member
Aug 29, 2022
1
1
Mwandishi Efrahim Mabena
mawasilino:0745323576
mahali: Makambako_Njombe

Kundi la watalii walikuwa wakitembelea bwawa la ziwa na walikuwa kwenye jengo linaloelea katikati ya ziwa la mamba.

Mmiliki wa bwawa hilo alipiga kelele: "Yeyote anayeruka ndani ya maji na kuogelea hadi kutoka, atapata dola milioni 10. Kimya kilikuwa kikatanda.

Ghafla, mtu mmoja akaruka ndani ya maji. Alikimbizwa na mamba, lakini kwa bahati nzuri hakudhurika. Mmiliki alitangaza: "Tuna mshindi !!!".

Baada ya kupokea zawadi yao, mwanamume huyo na mkewe walirudi kwenye chumba cha hoteli. Mwanamume anamwambia mkewe: "Sikuruka ndani ya bwawa ... Mtu alinisukuma !!!" Mkewe alitabasamu na kusema kwa kunongo'oneza: "Ni mimi ndio nilikusukuma!"

Funzo la hadithi: "Nyuma ya kila mwanaume aliyefanikiwa, daima kuna mwanamke wa kumpa msukumo kidogo" .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom