Zamiluni Zamiluni
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 13,996
- 15,119
Isipolipwa leo, kesho hakuna ruzuku na misaada !!
hilo deni la mwaka 1958 litakuwa liliachwa na mkolini muingereza. Kumbe tanganyika tulianza kukopa hata kabla ya uhuru
Ndiyo mwaka 1958 kulikuwa na Tanganyika chini ya ukoloni wa Muingereza (Trustship).
Kwanza huyu jamaa kwa miaka 10 kaishi angani Mwaka 1.
Ebu mtalaam wa Route za Rais wetu JK atupe idadi, kafikisha ngapi? Je kwa sasa anaongoza Rekodi ya kusafiri au yule wa Nigeria bado ni top?
Deni 2005 Trillion 7 mwaka 2015 June Deni Trillion 35!! Daah JK unasifa za ajabu ajabu!!
bado ni na wasiwasi na hoja hii, ikumbukwe sisi hatukuendeleza serikali ya kikoloni sisi tulianza serikali mpya kabisa, yaani ya tanganyika sina hakika sana kama tulirithi madeni ya mkoloni. na sidhani kama tulirithi deni hili wakati tunafutiwa madeni hili lazima lingekuwemo sasa mzee amelitoa wapi?
Hata hilo deni la wakoloni huenda hukulipa ila alikuwa anajipandishia chati tu huku akijua hakuna atakaye fuatilia!Ameshindwa kulipa deni la wazabuni wa hapa akalipa la wakoloni?? du du ! anyway tuliyataka wenyewe na tunayataka wenyewe na mengine Octoba siyo mbali tutayakumbatia tu tena!
Mkuu msome tanga kwetu alikuwepo mkutanoni na amefafanua zaidi!
Teh teh kwi kwi kwi!! dah umenikumbusha mambo ya promo!!Hata hilo deni la wakoloni huenda hukulipa ila alikuwa anajipandishia chati tu huku akijua hakuna atakaye fuatilia!
Sasa aliyepotosha umma ni nani?Mkuu unataka kusema ili mtu kupata habari lazima uwe kwenye mkutano husika? Nini maana ya vyombo vya habari. Acheni kupotosha umma.Raisi tumemwona akisema mwenyewe kwenye TV Kuwa kalipa deni la mwaka 1958 lilokopwa kwa ajili ya kujenga morogoro road.Ningemwomba Mh waziri wa Fedha atoe ufafanuzi kuhusu hilo deni la mkoloni tulilolipa kabla ya kuhitimisha vikao vya bunge kwa kuwa kipindi hicho kodi yote ilipelekwa kwa Malkia.
Rais Kikwete amesema serikali imelipa deni lilikopwa mwaka 1958 ambalo lilitumika kuijenga Morogoro Road.
Amesisitiza hakuna nongwa yoyote kwa madeni anayoacha kuja kulipwa na mrithi wake.
Amemalizia kuwa duniani kote ili nchi iendelee ni lazima ikope kama ilivyo kwa wafanyabiashara ili kukua lazima utakopa.
Chanzo: ITV habari
Rais Kikwete amesema serikali imelipa deni lilikopwa mwaka 1958 ambalo lilitumika kuijenga Morogoro Road.
Amesisitiza hakuna nongwa yoyote kwa madeni anayoacha kuja kulipwa na mrithi wake.
Amemalizia kuwa duniani kote ili nchi iendelee ni lazima ikope kama ilivyo kwa wafanyabiashara ili kukua lazima utakopa.
Chanzo: ITV habari
Inawezekana ktk issue kuna watu wamefanya ufisadi. Watu wanatafuta madeni yasiyo na wenyewe kama epa na escrow kisha wanapiga hela ndefu. Nakubaliana na Makongoro kuwa tatizo si kikwete bali vibaka wanaomzunguka!