Kikwete: Nimelipa deni la taifa la 1958

Kikwete: Nimelipa deni la taifa la 1958

Sidhani kama hoja yako ina mashiko. Mikopo ya serikali ipo wazi kama ile ya ujenzi wa bomba la gesi. Tatizo Watanzania tunajitia vipofu

Wewe Lizabon kwa unavojijua. Huniwezi darasani, maisha, wala siasa tambua hilo. Maana kama Raisi anajisifia kulipa deni wakati hapo hapo uchumi umeyumba. Si kilaza huyo Raisi. Chukulia mfano mzuri tu kwamba wewe ni mfanya biashara umechukua mkopo wenye masharti nafuu wakati huo biashara umeyumba, Je utalipa deni au utatumia kwanza hiyo hela kama Mtaji??
Sitak jibu kama la Kikwete hapa
 
Ni ajabu kudai umelipa deni lisilokuwepo, huu ni mwendelezo tu wa wizi. Kabla waropokaji hawajaanza kutoa kauli za ajabu ajabu, naomba mjue kuwa upo wakati madeni yote yalisamehewa tukaanza upya on a clean slate!

Bonge la fact, Asante Mr
 
Jamani kipindi cha Mkapa c tulifutiwa madeni na wahisani au hawakulifuta coz inadaiwa Tanganyika? Na 1958 deni lilikuwa chini ya serikali ya Waingireza na hao ndio wanajua ukweli na undani wa deni hilo...Shemegi fafanua vizuri umelipaje na kiasi gani
 
Duh.., akili imegota!
Kalipa deni la 1958! Hivi alizokopa kipindi chake mbona ajazilipa au ndio zitalipwa miaka 70 ijayo. ?!
 
Anafanana sana na shirika lao la umeme nyumba imebomolewa imehengwa upya na mmiliki mwingine utaaokia nyumba hii ina madeni ya nyuma!!!!
 
Kwahio hili sasa hivi litakuja kulipwa takriba mwaka 2070? Hahaaaaa hivi hia tukiwa kwenye majukwaa huwa tunawaza kweli tunachoongea??
 
1958 si alikopa mkoloni ama????
Kwa hiyo amelipa deni la mkoloni????
Serious ndio tumefikia hapa????
 
Mag3 nimeiweka "Nyerere Doctrine of state succession" kama ilivyofafanuliwa na Alpha Bisimba! Ikihitajika tafsiri yake kwa kiswahili tutafanya kwa manufaa ya umma.

My question remains unanswered! Kikwete is the Fourth Pres of URT, before then, there were three major phases of leadership. Y does this president fee obligated to pay a debt that all three predecessors felt unnecessary?
 
Last edited by a moderator:
Mag3 nimeiweka "Nyerere Doctrine of state succession" kama ilivyofafanuliwa na Alpha Bisimba! Ikihitajika tafsiri yake kwa kiswahili tutafanya kwa manufaa ya umma.
Kigarama, juhudi na mchango wa Mwalimu katika kuzitetea nchi masikini na nchi zilizokuwa bado zimo kwenye minyororo ya kikoloni ni mkubwa sana. Ni mwalimu pekee aliyeweza kukaa meza moja na viongozi wakuu wa mashirika ya fedha duniani na kuwa na mazungumzo nao on one-on-one basis na ni mara nyingi tu aliweza kuwaacha hoi huku wakikuna vichwa na kujiuliza huyu mtu vipi, katokea wapi!

content


Mwalimu aliandika kitabu kinaitwa Nyerere Doctrine of state succession and the new state of East Africa kwa hoja ambazo nguvu zake bado ziko relevant hadi leo. Kwa mtu tena Raisi, kudai analipa madeni ya mwaka 1958 Tanganyika ikiwa ni trust territory ya Uingereza ni umulugo usio na kiwango. Mwalimu pia aliongoza mapambano ya kusamehewa madeni kwa nchi masikini ambazo hazikuwa na uwezo wa kulipa.
 
Last edited by a moderator:
Duh.., akili imegota! Kalipa deni la 1958! Hivi alizokopa kipindi chake mbona ajazilipa au ndio zitalipwa miaka 70 ijayo. ?!
Huo ndio msingi wa hoja yake kwamba unapoingia madarakani unalipa kwanza madeni unayoyakuta na huo ni utaratibu wa kawaida kabisa!
 
Ni ajabu kudai umelipa deni lisilokuwepo, huu ni mwendelezo tu wa wizi. Kabla waropokaji hawajaanza kutoa kauli za ajabu ajabu, naomba mjue kuwa upo wakati madeni yote yalisamehewa tukaanza upya on a clean slate!
mkuu kwa niaba ya familia yangu iliyoko Tandika mwembeyanga karibu na transforma nakushukuru sana ; la ziada sina bali nakutakia RAMADHAN KAREEEM .
 
Sidhani kama hoja yako ina mashiko. Mikopo ya serikali ipo wazi kama ile ya ujenzi wa bomba la gesi. Tatizo Watanzania tunajitia vipofu
ujenzi wa bomba la gesi kwenda wapi na ni nani alitaka hivyo na kwa nini ? mmeua watu kwa vile walitaka kupunguza gharama kwa gesi kuchakatwa mtwara , sasa hizo gharama zenu zilizokataliwa na wananchi kwanini unazifanya ndio utetezi wako ?
 
Hapa Chama kimezingua, kinapaswa kitolee maelezo ya kina.

Haiingii akilini kulipa deni la Tanganyika ( under colonialism).

Na imekuwaje alipe deni la Tanganyika wakati yeye ni raisi wa Tanzania?

Znzbar wanataarifa?
 
Back
Top Bottom