Kikwete: Nimelipa deni la taifa la 1958

Kikwete: Nimelipa deni la taifa la 1958

Ni ajabu kudai umelipa deni lisilokuwepo, huu ni mwendelezo tu wa wizi. Kabla waropokaji hawajaanza kutoa kauli za ajabu ajabu, naomba mjue kuwa upo wakati madeni yote yalisamehewa tukaanza upya on a clean slate!
HIPC !
Paris club, mzee CD Msuya anaweza kutueleza mengi


 
Mkopo 1958!! Alikopaga nani? Maana serikali huru ilikuwepo madarakani 1961. Nyerere hakuwa Rais. Alikopa nani. Wataalam msaada jamani

Lazima atakuwa alichemka kutamka mwaka.... Wale wale #Team Mulugo at work...
Waacheni watu watie nia.... URAIS umekuwa rahisi sana!!
"Kama hadi yule kaweza iweje sisi tushindwe...???"
 
bado ni na wasiwasi na hoja hii, ikumbukwe sisi hatukuendeleza serikali ya kikoloni sisi tulianza serikali mpya kabisa, yaani ya tanganyika sina hakika sana kama tulirithi madeni ya mkoloni. na sidhani kama tulirithi deni hili wakati tunafutiwa madeni hili lazima lingekuwemo sasa mzee amelitoa wapi?
 
Hapana,naomba serikali itoe maelezo ya kina!Kama ni kweli tumelipa nadhani hii itakuwa EPA nyingine,watu wametumia fursa kupiga pesa!
 
bado ni na wasiwasi na hoja hii, ikumbukwe sisi hatukuendeleza serikali ya kikoloni sisi tulianza serikali mpya kabisa, yaani ya tanganyika sina hakika sana kama tulirithi madeni ya mkoloni. na sidhani kama tulirithi deni hili wakati tunafutiwa madeni hili lazima lingekuwemo sasa mzee amelitoa wapi?
Mkuu msome tanga kwetu alikuwepo mkutanoni haya yakizungumzwa na JK!
 
Mfa maji haachi kutapatapa!!! Jk anasoma huku jamiforum aise.

Ila nikisoma comments za hawa wengine ambao wanapinga hoja na kutetea madudu,roho yangu inaniuma sana.
Naipenda Tanzania kuliko najipwnda mwenywe. Niko radhi kufa kwa nchi yangu. Niko radhi kuitetea nchi na sio mtu;kwahiyo sielewi hapa nini.
Lakni kama ni ujinga naamini tutaelimika siku moja.
 
Laiti mh mkapa angegeuka na kuwa dikteta kama Mugabe na kagame tungekuwa mbali sana kiuchumi hawa kenya wangetusikiaga tu.
Kwa hali hii ni bora mkapa akachukue fomu
 
Nina wasi wasi kama pesa hiyo imelipwa kweli, kuna harufu ya ufisadi hapo. Yawezekana pesa imepigwa na mkoloni anasingiziwa kulipwa.
 
Lazima atakuwa alichemka kutamka mwaka.... Wale wale #Team Mulugo at work...Waacheni watu watie nia.... URAIS umekuwa rahisi sana!!"Kama hadi yule kaweza iweje sisi tushindwe...???"
Mkuu msome tanga kwetu alikuwepo mkutanoni na amefafanua zaidi!
 
Mkuu, kwani madeni yaliyokopwa na serikali ya Tanganyika hayawezi kulipwa na serikali ya Tanzania? Ukilaza mwingine huu bana!
Zanzibar inahusikaje na madeni ya Tanganyika! Huu Muungano huu!!!!!!!
 
Laiti mh mkapa angegeuka na kuwa dikteta kama Mugabe na kagame tungekuwa mbali sana kiuchumi hawa kenya wangetusikiaga tu.
Kwa hali hii ni bora mkapa akachukue fomu

Hii kauli huwa naishangaa sana. Unajua Mgabe ameiingiza Zimbabwe shimoni? Si kila udikteta ni mzuri. Actually madikteta wengi huziua kabisa nchi; angalia Congo ya Mobutu, Zimbabwe ya Mugabe, Africa ya kati ya Kina Bocassa, Nigeria ya kina Sani Abacha. Tuwe waangalifu sana. Tunachanganya udikteta na uzalendo. Zimbabwe leo hii kama huna business ya kukuletea American Dollar huna maisha - Mugabe akiwadanganya eti anapambana na wazungu.

Tuache kulilia udikteta, hapo tunalilia kisu kitakachotuchinja! Udikteta haufai kabisaa. Kumbuka wakati wa Mkapa; ununuzi wa rada na rushwa zake, Ununuzi wa Ndege ya rais na rushwa zake, EPA ilifanyika wakati wa Mkapa, Kuanzisha Kampuni from Ikulu. Mkapa angekuwa bado rais leo hii, yeye na genge lake wangekuwa mamilionea kwa rushwa za mtindo huu. Na genge lake ndo hao tunawaona wakijiandaa kuingia Ikulu kwa nguvu zote!!! God forbid.
 
Nilikuwepo mkutanoni alipoongea hili. Hajalipa bali awamu yake imemalizia deni. Kwenye schedule of payment, deni lilikuwa liishie awamu hii.
Ahsante mkuu tanga kwetu kwa ufafanuzi mzuri BTW kumalizia deni ndio kulipa kwenyewe!!
 
Kopa kwa sababu maalum sio kukopa na kununua malory na kwenda kutumia na mademu
 
Wewe Lizabon kwa unavojijua. Huniwezi darasani, maisha, wala siasa tambua hilo. Maana kama Raisi anajisifia kulipa deni wakati hapo hapo uchumi umeyumba. Si kilaza huyo Raisi. Chukulia mfano mzuri tu kwamba wewe ni mfanya biashara umechukua mkopo wenye masharti nafuu wakati huo biashara umeyumba, Je utalipa deni au utatumia kwanza hiyo hela kama Mtaji??
Sitak jibu kama la Kikwete hapa

Tatizo umemuuliza mtu ambaye hawezi kukujibu laizi ya kutetea ujinga kama alivyokaririshwa. Uchumi wa nchi umetetereka huku raisi anajisifu umeimarika na kujigamba kulipa deni hewa.
 
Upunguani umegraduate sasa.mambo gani hata JK kutugeuza wananchi wako mabozo?kodi zetu kuleni ila mtuheshimu.haya madudu ya kuwalipia kodi wakoloni iko siku mtalipia gharama za vita ya majimaji na stripend za kikao cha Berlin.huu ni upunguani of the highest order.
 
Lazima atakuwa alichemka kutamka mwaka.... Wale wale #Team Mulugo at work...
Waacheni watu watie nia.... URAIS umekuwa rahisi sana!!
"Kama hadi yule kaweza iweje sisi tushindwe...???"


Nahisi anamaanisha 1968 labda
 
Tatizo siyo kukopa, nyinyi mnakopa halafu mnapiga!
 
Back
Top Bottom