Mkuu, kwani madeni yaliyokopwa na serikali ya Tanganyika hayawezi kulipwa na serikali ya Tanzania? Ukilaza mwingine huu bana!
Siamini kuwa kweli mwaka 1958 Mwingereza alikopa kujenga eti kutujengea Morogoro road. Iwapo reli ya kati yenyewe haikukopwa iweje Morogoro road? Sina data kwa hiyo nitanashangaa ntu.
wataanza kumbana kuanzia hapa JF alafu akishagundua kuwa alikuwa haongei na wajukuu zake bali taifa kama kawaida utasikia ..."washauri wangu wamenipotosha"!Hapana,naomba serikali itoe maelezo ya kina!Kama ni kweli tumelipa nadhani hii itakuwa EPA nyingine,watu wametumia fursa kupiga pesa!
Nafuata ushauri wa Professor ngoja nikashitue KIROBAMwaka 1958 kuliwa na Tanganyika. rais kweli tunaye
wataanza kumbana kuanzia hapa JF alafu akishagundua kuwa alikuwa haongei na wajukuu zake bali taifa kama kawaida utasikia ..."washauri wangu wamenipotosha"!
Sio ajabu safari hii na washauri wote wanataka kuingia ikulu wenyewe maana wamechoka kusingiziwa.
AiseeRais Kikwete amesema serikali imelipa deni lilikopwa mwaka 1958 ambalo lilitumika kuijenga Morogoro Road.
Amesisitiza hakuna nongwa yoyote kwa madeni anayoacha kuja kulipwa na mrithi wake.
Amemalizia kuwa duniani kote ili nchi iendelee ni lazima ikope kama ilivyo kwa wafanyabiashara ili kukua lazima utakopa.
Chanzo: ITV habari
Hii kauli huwa naishangaa sana. Unajua Mgabe ameiingiza Zimbabwe shimoni? Si kila udikteta ni mzuri. Actually madikteta wengi huziua kabisa nchi; angalia Congo ya Mobutu, Zimbabwe ya Mugabe, Africa ya kati ya Kina Bocassa, Nigeria ya kina Sani Abacha. Tuwe waangalifu sana. Tunachanganya udikteta na uzalendo. Zimbabwe leo hii kama huna business ya kukuletea American Dollar huna maisha - Mugabe akiwadanganya eti anapambana na wazungu.
Tuache kulilia udikteta, hapo tunalilia kisu kitakachotuchinja! Udikteta haufai kabisaa. Kumbuka wakati wa Mkapa; ununuzi wa rada na rushwa zake, Ununuzi wa Ndege ya rais na rushwa zake, EPA ilifanyika wakati wa Mkapa, Kuanzisha Kampuni from Ikulu. Mkapa angekuwa bado rais leo hii, yeye na genge lake wangekuwa mamilionea kwa rushwa za mtindo huu. Na genge lake ndo hao tunawaona wakijiandaa kuingia Ikulu kwa nguvu zote!!! God forbid.
sijafananisha utendaji wa mkapa na mugabe ila nimesema endapo angeendelea kudumu madarakan kama mugabe tungekuwa mbali kwani utendaji wa mkapa ni mzuri na naamin endapo angeendelea had sasa haya madudu ya jk yasingekuwepo kwa kiasi hiki halafu mbona hujamzungumzia kagame na mafanikio yake
Sijui hayo madeni ya kale yamelipwa kwa hela ipi, wakati madeni ya ndani yameshindikana mwaka wa tatu sasa!Rais Kikwete amesema serikali imelipa deni lilikopwa mwaka 1958 ambalo lilitumika kuijenga Morogoro Road.
Amesisitiza hakuna nongwa yoyote kwa madeni anayoacha kuja kulipwa na mrithi wake.
Amemalizia kuwa duniani kote ili nchi iendelee ni lazima ikope kama ilivyo kwa wafanyabiashara ili kukua lazima utakopa.
Chanzo: ITV habari
Mwaka 1958 kuliwa na Tanganyika. rais kweli tunaye
Naam mkuu,
Kama kumbukumbu zangu ziko sawa ni wakati wa sera Ben Mkapa ya UBINAFSISHAJI. Ilifikia kipindi wakati Mr Clean akijiandaa kustaafu kwa majigambo makuu akasema "Ndege ya uchumi wa Tanzania iko kwenye runway tayari kwa kupaa"..!!! Maweeeeeeeeee.... Laiti angejua mtu anayemfuata.....
BACK TANGANYIKA
hilo deni la mwaka 1958 litakuwa liliachwa na mkolini muingereza. Kumbe tanganyika tulianza kukopa hata kabla ya uhuru