Hivi Mwizi akija kuiba nyumbani kwako akakukata mapanga wewe na familia yako, akiwa anakimbia akaacha baadhi ya vifaa alivyotumia kuvunjia mlango kama mashoka, mapanga n.k,
Je, aliyeibiwa ana wajibu wa kulipia hivi vitu kwa mwizi kama mwizi alivikopa hardware store?
Je, mwizi anatakiwa kulipiwa nauli aliyokopa ya kuja kukuibia nyumbani kwako?
Waingereza na wajerumani ni wezi, wametok aulaya na vifaa vya kuja kutuibia rasilimali zetu, ili kufanikisha wizi huo walikopa huko walikotoka kwa wayahudi n.k (wajerumani madeni ya wayahudi yaliwashinda wakaanzisha world war II), sasa mikopo ya hawa wezi wa rasilimali zetu kwa nini tulipe sie tulioibiwa?inaingia akilini kweli?
Hatukuwatuma wakakope ili kuja kufanikisha wizi wao. Kumbukeni, hizi barabara na reli walizojenga wakoloni, zilikuwa na dhumuni moja tu, kukusanya kila kinachoibika Africa na Tanzania na kukihamishia Ulaya.
Sasa Kuna mantiki gani sisi kulipa madeni ya hawa wezi wetu?