Kikwete awadanganya watanzania - TENA

Kwanza kabisa mtu akinipa heshima ya ukada mimi naipokea kwa taadhima kabisa sina noma wala nini, enzi za Nyerere jamaa mmoja alisema Nampendekeza Julius kuwa Raisi wa jamhuri anayepinga anyooshe mkono, hakuna aliyenyoosha mkono basi Nyerere akawa raisi wa jamuhuri;)

Aisee kwamba jua ndio limewachosha mimi sikubaliani kabisa, mbona wanene wa CCM hawajachoka?wakati wao wapo kwenye nchi hii pia na jua si linawamulika wao pia? mbona California jua linapiga mwaka mzima lakini watu hawajachoka? mwenye njaa huchoka, mwenye shibe hunawiri.

hao watu wa california wana rangi gani ?
watu wa nyumbani bana sio wengi wanaojua/hata kama wanajua hawatilii maanani mambo ya manukato na uturi bobu, sasa utakuta mtu anaamka asubuhi mswaki jiti, hapaki mafuta, nywele hachani, unategemea aonekane sawa na wewe unayepaka uturi kila siku, deodorant ya nguvu, unanyeshewa na maji ya mvua kila siku bafuni ! wakati nyumbani mtu anatumia ndoo na maji utakuta sana sana mtu yanamwagikia kichwani, lakini kwenye magoti husahau njia na yakifika hadi kwenye magoti basi ujue mvua siku hiyo imenyesha tena ya nguvu ! bana wee, manukato, na joto kali hufanya watu wachoke ! Nadhani hapa tutaende mbali na hii mada kama tutaendelea kuzungumza kuhusu hali ya hewa !
 
Maneno yako yana msingi wa kujilinda lakini naona kipindi cha kumpima hakijafika wala hajatimiza nusu ya awamu ya kwanza,huyu mtu ndio kwanza ameanza kujenga si kweli hakuna mabadiliko katika uwajibikaji wa ahadi zake.lakini waswahili wanasema akutukanae hakuchagulii tusi,mnavyotaka nyinyi kuwa mkisema tu basi achukue hatua za kuwakamata na kuwapeleka jela,hilo halipo isipokuwa kwenye nchi za kidikiteta.Muungwana ni kiongozi muadilifu na ni binadamu kama binadamu wengine ,hakuna asiekosea na kila unapokosea ndipo unapojifunza mbinu mpya za kukabiliana na matatizo Tanzania mkae mkijua si kisiwa kama kama kisiwa cha Shelisheli,hivyo kinachotakiwa ni subira ya miaka mitano,hapo Watanzania ndio watampima uwezo wake wapi aliahidi na wapi amefikia na kipi kimekamilika.Haraka haraka haina baraka.


Hiyo kauri ya kusubiri miaka 5 kupima uwezo wa President utafiti wake umeufanyia wapi?
kwa nini si miaka 7 au miaka 3?

Hivi kigezo cha uadilifu ni muda wa kukaa madarakanai au Strategy za kupambana na matatizo?

Tangu aingie madarakani Kikwete kafukuza kazi mtumishi 1 tu wa serikali, yule Polisi aliyeacha Lindo kule Kinondoni na kwenda kupendeza kwa ulabu.

Mwiba maelezo yako yanaonyesha matobo ya system iliyopo yanakunyea pengine ndiyo sababu kimoyomoyo unaomba rais achuke hata miaka 10 kuyaziba! Bisha?
 
Bongo rhumba kali.........

Mwanzoni mwa mwaka 2007 kilo ya sembe shs 250 kwa sasa ukienda dukani kwa mpemba kilo ya sembe ni shs 500

Upande wa nyama ndio usiseme, kwa sasa nyama mchanganyiko bucher za mwenge ni shs 3,700 - 4,000 nilipouliza wauzaji kwanini bei imepanda sana, jibu lao ni kuwa ng'ombe wengi wanasafirishwa kwenda commoro, soko la ndani linapungikiwa kwa hiyo bei inakwenda juu.

Kuku wa kienyeji hashikiki kwa sasa Jogoo soko la buguruni anauzwa 13,000 - 16,000
 
kada acha mchezo wewe bongo watu wana njaa ile mbaya mpaka wanatia huruma,does it make sense to you makada wenzako wanatanua na landcruisers za milioni mia mia huku wengine hata hawajui watoto wao watakula nini? na ubaya hizo pesa ni za walipa kodi ndio zinanunua hayo magari ...fikiria vizuri kuna umafia mbaya sana unaendelea nchi ile sio kushabikia tuu,kada najua unakaa nchi za watu ulishawahi kuona seriakli huko ina matumizi ya kununulia maofisa wake magari,mafuta,madereva na nyumba kama Tanzania...its unheard kwa wenzetu na kila mtu aende finance gari lake na mafuta yake na apige gear mwenyewe,lazima ukubali umaskini mwingi umesababishwa na serikali ya CCM inabidi waondoke tuu maana kwa mwendo huu umaskini utazidi...can you believe jengo la BOT cost 350m USD? hata California lisingecost hivyo ni wizi tuu na rushwa imejaa
 
...can you believe jengo la BOT cost 350m USD? hata California lisingecost hivyo ni wizi tuu na rushwa imejaa

Mze Koba hapo umesema kweli kabisa, hawa jamaa bongo wanaexagerate sana!mpaka wanaua. yaani pale dar sa nyingine unataka kiwanja jamaa akishasikia umetoka nje anataka akupige bei kubwa kuliko hata kiwanja Manhattan.
 
Bongo rhumba kali.........

Kuku wa kienyeji hashikiki kwa sasa Jogoo soko la buguruni anauzwa 13,000 - 16,000

Europe kwenye Euro zone watu mishahara mikubwa halafu kuku amefungashwa vizuri ni kama euro 2 hivi, ukipiga mahesabu hiyo itakuwa shilingi 3200 TZ shilings, sasa pale bongo ambapo watu mishahara midogo kwanini wawapige bei kubwa hivyo? si mauaji hayo? ndo maana nilisema bongo huwa wanaexagérate sana,utu unawekwa pembeni.
 
kada acha mchezo wewe bongo watu wana njaa ile mbaya mpaka wanatia huruma,does it make sense to you makada wenzako wanatanua na landcruisers za milioni mia mia huku wengine hata hawajui watoto wao watakula nini? na ubaya hizo pesa ni za walipa kodi ndio zinanunua hayo magari ...fikiria vizuri kuna umafia mbaya sana unaendelea nchi ile sio kushabikia tuu,kada najua unakaa nchi za watu ulishawahi kuona seriakli huko ina matumizi ya kununulia maofisa wake magari,mafuta,madereva na nyumba kama Tanzania...its unheard kwa wenzetu na kila mtu aende finance gari lake na mafuta yake na apige gear mwenyewe,lazima ukubali umaskini mwingi umesababishwa na serikali ya CCM inabidi waondoke tuu maana kwa mwendo huu umaskini utazidi...can you believe jengo la BOT cost 350m USD? hata California lisingecost hivyo ni wizi tuu na rushwa imejaa

sawa nitaacha mchezo !
 
Maneno yako yana msingi wa kujilinda lakini naona kipindi cha kumpima hakijafika wala hajatimiza nusu ya awamu ya kwanza,huyu mtu ndio kwanza ameanza kujenga si kweli hakuna mabadiliko katika uwajibikaji wa ahadi zake.

Mtu anapimwa baada ya kumaliza awamu? Alitoa ahadi atakazotimiza baada ya 2010?
Ajira, maisha bora aliahidi yatakuja baada ya kumaliza kipindi cha kwanza?

Tatizo aliifanya ikulu sehemu ya kujifunzia, yale ambayo Sumaye aliyosema kuwa IKULU SIYO SEHEMU YA KUJIFUNZIA.

Katika kujifunza kuna kudiqualify, anaelekea kudiSCO , I can say!
 
Kikwete aliahidi ajira milioni moja, aliahidi kupitia mikataba upya, aliahidi kuboresha maisha, aliahidi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu, aliahidi ujenzi wa miundo mbinu, aliahidi kusaidia michezo nchini, aliahidi kufanya vingi sana...

So far ameshindwa kuboresha maisha bora in two years kama inawezekana, lakini kwenye the rest yuko kwenye the right track, maana alitengeneza bara bara ya jimbo la mbunge Zitto bila kujali chama chake, mnyonge mnyongeni wakuu!

Ahadi zote mkuu Mwafrika, ni kweli alizitoa lakini kuna one thing hukisemi, nacho ni kama aliahidi muda, ni kwa sababu hakuahidi itamchukua muda gani kuyafanya hayo yote aliyoahidi.
 
hapana, SIJAUNGA MKONO, bali nimetoa mshangao, niwaunge tela lenu hilo linalosuasua bana msije mkaniacha njiani ! acheni tu nimalizie safari yangu na hao mnaowaita Mafisadi, kwanza kila mtu akibase upande mmoja (haipendezi) nyie kaeni huko huko mlipo, na sie tukae huku tulipo (au nyie mje huku tulipo maana binfasi sina hata chembe ya kusikia kampeni zenu chafu zilizojaa chuki na uwongo,angalau saa nyingine mnakuwa na hoja nzuri)!! hehe ehheeee, lakini ukweli !

hivi wewe ndiyo muda mwingine huwa unajiita kada mpinzani? nataka kujua ili nione kama nikae au nitoke kwenye hii mada
 
Kwa wale ambao wanafuatilia siasa za marekani watakumbuka kuwa miaka ya 90, serikali ya Clinton ilifanikiwa kuweka makubaliano na Korea kaskazini ili wamarekani wawapatie wakorea mafuta na chakula kwa uhakikisho kuwa wakorea wataachana na mipango ya kujenga nyuklia.

Joji Kichaka (ambaye alipondea sana alichofanya Clinton na democrats) alivyoingia madarakani alitishia kuwa angetumia nguvu ili wakorea waache nyuklia na vitisho vingine kibao. Haya, hata miaka haijapita, kichaka amedhihirisha kuwa mtu wa vitisho tu kwani wakorea wamejaribu kwa mafanikio nyuklia yao na pia Kichaka imebidi tu atume watu wakafanye mazungumzo na wakorea.

Mfano huu wa Kichaka na vitisho vya maneno ya democrats ni kitu ambacho Kikwete amejifunza toka kwa rafiki yake joji kichaka na sasa anakitumia Tanzania. Nilifuatilia sana maneno na ahadi za Kikwete wakati wa kampeni za kugombea uraisi. Maneno mengine sio tu yalikuwa kama ahadi za Joji Kichaka bali yalikuwa kama ahadi za mama anayebembeleza na kuhadaa mwanaye ili anyamaze na kulala.

Kikwete aliahidi ajira milioni moja, aliahidi kupitia mikataba upya, aliahidi kuboresha maisha, aliahidi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu, aliahidi ujenzi wa miundo mbinu, aliahidi kusaidia michezo nchini, aliahidi kufanya vingi sana...

Baada ya kuwa raisi, akaomba apelekewe majina wa mafisadi na wauzaji wa madawa ya kulevya, akaanzisha website ili kupokea maoni ya wananchi, akatoa namba za simu ili kupokea maoni ya watu na ahadi kibao.

Wakati watu wakisubiria sera zitekelezwe, waziri wake akasaini mkataba wa Richmonduli, buzwagi, mikataba kibao ya uchunguzi wa madini, nakadhalika. Wakati huo huo ikajulikana kuwa kuna upotevu mkubwa sana wa pesa BOT, akiba kubwa ya pesa za kigeni iliyoachwa na Mkapa ilikuwa ikipotea, nk.

Wakati haya yakiendelea, Kikwete akaanza safari za nje ambazo zimetumia mabilioni ya shilingi za watanzania, ukaguzi wa fedha ukaonyesha kuwa kuna matumizi zaidi ya bilioni moja ambayo hayana uthibitisho wowote huko ikulu, nk.

Hali ya wananchi ikazidi kuwa mbaya, mfumuko wa bei zaidi ya asilimia mia mbili kwa bidhaa muhimu, nk wakati serikali na viongozi wakitumbua mabilioni kwa ufahari wa magari na serikali yenye watu wengi sana (moja ya baraza la mawaziri kubwa kabisa barani Afrika).

Wakati wananchi wakisubiri vitendo, Kikwete anaendeleza trik ya Joji Kichaka (ndio maana hawa ni marafiki) ya kutoa maneno tu ambayo hayana vitendo. Hotuba yake ya Dodoma imejaa ahadi nyingi kuliko hata zile alizotoa wakati wa kampeni.

Kwa mara nyingine tena Kikwete amewadanganya watanzani. Swali ni kwamba, mpaka lini ataendelea kuwahadaa watanzania?

"Richmonduli" your freakin azz, godammit!! Wewe kila mada ni kumlaumu tuu Kikwete na lawama hizohizo za kuruduiarudia kila siku. Huchoki?!!! KAMA HUNA JIPYA KAA KIMYA!! PERIOD!

Nani kakwambia rais akiwa kama "mere mortal" anaweza miujiza ya kubadilisha mfumo mzima wa jamii na uchumi katika nchi ya watu milioni 40 kwenye muda wa chini ya miaka miwili? Mwache baba wa watu afanye kazi yake kwa amani.
 
People you are joking. Mnasema miaka miwili haitoshi, katika miaka hii miwili tungeona dalili nzuri lakini tumeone dalili mbaya, kama mkiendelea na hilo la kusema bado, mnaweza hata kusema miaka mitan haitoshi tumuongeze mingine mitano, na kumi ikiisha wendawazimu wanaweza kuanza kusema tubadilishe katiba tuongoeze vipindi vie vitatu. Let us face it people, JK ametudisappoint tuliomchagua, let us admit it. Tusipambe maneno na kujipendekeza nchi yetu inateketea.
 
People you are joking. Mnasema miaka miwili haitoshi, katika miaka hii miwili tungeona dalili nzuri lakini tumeone dalili mbaya, kama mkiendelea na hilo la kusema bado, mnaweza hata kusema miaka mitan haitoshi tumuongeze mingine mitano, na kumi ikiisha wendawazimu wanaweza kuanza kusema tubadilishe katiba tuongoeze vipindi vie vitatu. Let us face it people, JK ametudisappoint tuliomchagua, let us admit it. Tusipambe maneno na kujipendekeza nchi yetu inateketea.

Folks like you need a regular dose of reality. Nenda soma na kutafakari busara zilizomo kwenye "amri 6" alizoandika Padri Karugendo. If doesn´t help then nashauri urudi Bongo "for genuine reality check" badala ya kukandia serikali huku mmejichimbia Ughaibuni mkivuta muda mpate uraia wa kigeni.
 
When your creating argument concern development, you have to know development does not happen with in a week. When you look at development in any third world nation, you will find that development in this nations means something else, that me and you we doesn't know.
JK under estimate development and Economic integration of Tanzania. What i believe JK had little knowledge concern economic development of any third world. There is no one in this earth will create one million jobs with in a year in Tanzania, this is a fact.

Inflation has something to do with the president if and only if president affiliated with central bank. You need to know Central Bank(BOT) is responsible for inflation, because there responsibility is to conduct monetary system and not build twin towers for 180Million. However on the other side president is suppose to monitor unnecessary rising of price in good and services. Other than that market is responsible of what is the price, because demand and supply works in free market.

Politician sometime they say things so they can be elected, this can be either Hillary Clinton with nationalization of health-care or JK i will make Tanzania the land of honey and Milk. One thing i believe JK has little knowledge concern development and integration.

When you promised people of any developing nation that i will change your life over night, your total insane and probably your in deep sleep. What JK was supposed to tell Tanzania is i will try to boost our economy to the point that 60% will afford three mills a day, this is reasonable number.

What went wrong is, JK use his handsome face to promise changes, changes that will never exist if your teammates are Rostam Azizi and Lowassa. When you lead the poor country like Tanzania you need people who have talents and managerial experiences, and not people who have fat mouth to point out that we are doing amazing while the country is in deep sea.

JK was wondering about review and change mining contracts, what he forget is a contracts is a promise. You can't brake the promise under this globalization economy bullshit, when you sign it, your whole country is bounded into that peace of paper, and that is what we call FDI effects. Too bad too sad but I'm sorry. Also you can not chase this investors out, while your budget depends 40% from foreign aid.

JK still can flip and make changes, but not the changes that he was wondering. The number one change is to increase the number of people who afford basic needs (food, shelter and clean water). Then he have to set long plan, and not ask bank to loan people money for business, that is not your job MR president.

Fight of corruption, still JK is not yet fighting corruption even for a second. Forget this TUKURU bullshit he create, if the agent is under president that is dosari, it will work without a check and balance. Bunge need to create a free agency which will over-site corruption, and take action against those who participate in corruption activities.

Last, JK need to quit being a police by trying to control every thing. What he is creating is confusion and misleading to Tanzania.

He still have a chance, but i total can't see him catch it. God Bless Tanzania
 
"Richmonduli" your freakin azz, godammit!! Wewe kila mada ni kumlaumu tuu Kikwete na lawama hizohizo za kuruduiarudia kila siku. Huchoki?!!! KAMA HUNA JIPYA KAA KIMYA!! PERIOD!

Nani kakwambia rais akiwa kama "mere mortal" anaweza miujiza ya kubadilisha mfumo mzima wa jamii na uchumi katika nchi ya watu milioni 40 kwenye muda wa chini ya miaka miwili? Mwache baba wa watu afanye kazi yake kwa amani.


Naona watetezi wa msanii wetu mnazidi kuongezeka. ushauri wa bure ni kuwa mwambie achape kazi vitu vionekane kama alivyoahidi. Hii longolongo haisaidii. Hata mkisambaa kila kona ya dunia kumtetea haisaidii kama hata-deliver!
 
Folks like you need a regular dose of reality. Nenda soma na kutafakari busara zilizomo kwenye "amri 6" alizoandika Padri Karugendo. If doesn´t help then nashauri urudi Bongo "for genuine reality check" badala ya kukandia serikali huku mmejichimbia Ughaibuni mkivuta muda mpate uraia wa kigeni.


Now where is that "dose of reality" sir/madam? Usifikirii kukaa hapo bongo ndio umekuwa mtanzania wa maana kuliko waliopo nje, wala hakuna anayejivunia kwa kukaa nje. Watu wapo nje for a reasonable cause. Kukaa nje sio kijiwe cha kupotezea muda kama unavyofikiri. Kalaghabao!
 
,hivyo kinachotakiwa ni subira ya miaka mitano,hapo Watanzania ndio watampima uwezo wake wapi aliahidi na wapi amefikia na kipi kimekamilika.Haraka haraka haina baraka.

Yaani tusimpompima sasa hivi ila tusubiri miaka mitano, atajirekebisha lini agombee awamu ya pili?
 
Folks like you need a regular dose of reality. Nenda soma na kutafakari busara zilizomo kwenye "amri 6" alizoandika Padri Karugendo. If doesn´t help then nashauri urudi Bongo "for genuine reality check" badala ya kukandia serikali huku mmejichimbia Ughaibuni mkivuta muda mpate uraia wa kigeni.

Haha my bro/Sis i like this genuine reality check. That is very good, because it does not need a university degree to see what mess we are in, it does not need a microscope to see that there is a bacteria eating our economy. Huhitaji Padre kukufafanulia yanayoonekana hapa kila leo (no need to prove the obvious). Bado nasisitiza kuwa tukitaka tuwe na mwelekeo mzuri we must face the reality, and not kiss some peoples ...or burry our faces in sand or put tails between legs. Nchi yetu iko kwenye matatizo, hilo ni lazima tukubaliane, labda tunaweza kupingana kwenye namna ya kutatua tatizo hilo. Unless you tell me your reality check tells you otherwise, kama unakubaliana na EL kuwa uchumi wetu unapaa, Congrats!
 
hivi wewe ndiyo muda mwingine huwa unajiita kada mpinzani? nataka kujua ili nione kama nikae au nitoke kwenye hii mada

Ndio mimi KadaMpinzani, natumia jina hili kumwakilisha KadaMpinzani aliyekuwa banned. i know you'll choose kutoka kwenye mada, adios !
 
Back
Top Bottom