akilimtindi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 421
- 83
Kufanya kweli inayoongelewa hapa kwa JK ni ngumu, nionalo mimi kama imebidi kuhutubia bunge wakiwemo mawaziri huenda wanataka kumtoa sadaka mmoja wao (ambaye washaongea naye wakapatana) ili imani irudi kwa wananchi kuwa JK bado yumo
Kama kweli JK yumo mfano rahisi amweke pingu Lowassa au Rostam, upo ushahidi mwingi sana kuhusu hawa "mapapa" kwahiyo hakuna haja ya kuwaundia tume ingine. Ikitokea hiyo nitajua kweli JK yumo, hata wakifungiwa kwenye hoteli zilizojengwa juzi huko magereza ingawa italeta balaa kubwa kwa kuonyesha matabaka waziwazi.
Naamini kama ana akili hakutakuwa na nafasi ya kuunda chombo kingine chochote kumshughulikia yeyote, nadhani sasa kama imetokea kuwa akina Mwanyika walishindwa kuyafanya aliyoyaagiza basi natamani kumwona akiyatamka kwa mdomo wake kwenye hiyo hotuba ambayo kwa hakika lazima atavaa "bukta tatu" ili awe imara kwa matamshi yake.
Naamini, kama kuna kubwa aendalo kulifanya tungeshaona dalili zake maana halitakuwa jambo la kawaida kwenye uongozi wake. Sio siri pia kwamba hao wahusika watakaoshughulikiwa washazipata taarifa hizo na tayari weshafanya lolote kuhakikisha hakitatokea hicho tukionacho sisi kwamba kitaandika historia kwenye utawala wa msanii wetu wa komedi, JK - kiazi kizee akilini ila kionekanacho bado kibichi kwa nje. Nasema kizee kwasababu tukijidhania prezidaa ni mtu mzuri na safi...! basi akili yake inafaa kutibiwa maana imeoza kwa sasa...! vinginevyo tukikubali kuwa prezidaa ni mzima, basi tukubali ni mwizi mkubwa anayesimamia wenzake kuiba na kutumia mbinu zozote ziwezekanazo kuhakikisha wananchi hawashtukii mbinu zao.
Kama kweli JK yumo mfano rahisi amweke pingu Lowassa au Rostam, upo ushahidi mwingi sana kuhusu hawa "mapapa" kwahiyo hakuna haja ya kuwaundia tume ingine. Ikitokea hiyo nitajua kweli JK yumo, hata wakifungiwa kwenye hoteli zilizojengwa juzi huko magereza ingawa italeta balaa kubwa kwa kuonyesha matabaka waziwazi.
Naamini kama ana akili hakutakuwa na nafasi ya kuunda chombo kingine chochote kumshughulikia yeyote, nadhani sasa kama imetokea kuwa akina Mwanyika walishindwa kuyafanya aliyoyaagiza basi natamani kumwona akiyatamka kwa mdomo wake kwenye hiyo hotuba ambayo kwa hakika lazima atavaa "bukta tatu" ili awe imara kwa matamshi yake.
Naamini, kama kuna kubwa aendalo kulifanya tungeshaona dalili zake maana halitakuwa jambo la kawaida kwenye uongozi wake. Sio siri pia kwamba hao wahusika watakaoshughulikiwa washazipata taarifa hizo na tayari weshafanya lolote kuhakikisha hakitatokea hicho tukionacho sisi kwamba kitaandika historia kwenye utawala wa msanii wetu wa komedi, JK - kiazi kizee akilini ila kionekanacho bado kibichi kwa nje. Nasema kizee kwasababu tukijidhania prezidaa ni mtu mzuri na safi...! basi akili yake inafaa kutibiwa maana imeoza kwa sasa...! vinginevyo tukikubali kuwa prezidaa ni mzima, basi tukubali ni mwizi mkubwa anayesimamia wenzake kuiba na kutumia mbinu zozote ziwezekanazo kuhakikisha wananchi hawashtukii mbinu zao.