Kikwete apokea Ripoti ya EPA ajiandaa kuhutubia Taifa!

HABARI zilizonifikia hivi punde, zinaeleza kwamba sehemu ya hotuba ya RAIS inasema;

"Mheshimiwa Spika, nimepokea ripoti ya uchunguzi wa upotevu wa fedha za EPA na tayari nimekwisha vikabidhi vyombo husika kwa ajili ya utekelezaji." mwisho wa kunukuu, na baada ya hapo ataendelea na mambo mengine muhimu ya Kitaifa na suala hilo hapo ndio utakuwa mwisho wake kujadiliwa kwani, "liko mikononi mwa vyombo husika".

Hapa kuna maswali, vyombo husika ni vipi? Si ndio alivyovipa kazi, na badala ya kufanya kazi, vikaja na RIPOTI, kwa hiyo sasa tutegemee na kusubiri RIPOTI nyingine kutoka "VYOMBO HUSIKA"..... Hii inawezekana Tanzania pekee

Eti anataka kusema nini? kama anatarajia kuwa kauli hiyo itawashtua watanzania na kuwafanya wamashangilie, basi asubiri kushtuka yeye mwenyewe.
Waliomba muda tukawapa, kama wanadhani wataendelea kupewa muda wakati wote, they are in for surprise.
Hakuna atakayeacha kuyajadili haya hata kama yakipelekwa kwa nani, tunachotaka kuona ni hatua madhubuti zinachukuliwa dhidi ya watuhumiwa wote. Hiyo hadithi ya vyombo husika imeshapitwa na wakati
 
Jana kwenye taarifa ya kina Rweyemamu wanasema Rais aliwapongeza kwa kazi nzito na ngumu lakini nzuri.... kilichonishangaza ni kuwa hata kusoma ripoti yenyewe hakusoma ndio amekabidhiwa tu... sasa alijuaje ni nzuri?

Hapo ndipo mungwana alipo tokota labda walikuwa wanampa dondoo nini kimejili nani kakamatwa....ndo maana akaamua kuwapongeza.Kiundani ni usanii mtupu tabu lote kasoma saa ngapi?
 
kurasa za mbelel za magazeti siku ya ijumaa ziandikwe kwa umakini ili zisipotoshe ukweli wa mambo. Wasije wakatuletea mkanaganyiko wa taarifa hasa wale tukaokuwa kazini na kushindwa kumskiliza JK
 
Halisi,


Kumbuka ilitakiwa wachukuliwe hatua na si kuwasilisha report kwa mbwembwe na kuwaita waandishi wa habari.

Muungwana kaona si vyema kufanya mbwembwe cha muhimu zaidi ni hatua za kuchukuliwa.

Safi sana Muungwana!

.....Akiwachukulia hatua ni sawa na kujichukulia mwenyewe hatua......hakuna awezaye kufanya ujinga huo....amka!
 
Back
Top Bottom