Elections 2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

Status
Not open for further replies.
Freeman Mbowe 2005 mikutano yake ilikuwa inajaza watu kama hii ya Wilberd Slaana matumizi ya HELKOPTA na la kushangaza Mbowe alikubali kushindwa kwa kishindo tena alihunduria kuapishwa kwa JK wakati CUF na TLP walikataa kukubali matokeo! jee DR. Slaa atakuwa tayari kufuata nyayo za Mwenyekiti wake Mbowe kukubali matokeo ya ushindi wa CCM wa TSUNAMI

CHADEMA munaota ndoto za mchana! hata mwaka 2005 mulikuwa na ndoto hizi hizi za kudai ushindi hewa! sasa ngojeeni 31 october mtakavyo garagazwa! ila tunamuomba Slaa akubali matokeo kama alivyofanya Mbowe 2005!

CHADEMA wacheni FITINA na UMBEA wa kuwasingizia viongozi wa CCM kuwa wananjama za kuwauwa viongozi wenu! huu ni uongo wa wazi kabisa na kama munaushahidi toka kwa USALAMA wenu wa TAIFA si mupeleke tuhuma zenu POLISI? munangoja nini? WACHENI KUWADANGANYA WANANCHI KUWA SLAA ATASHINDA! HUKO VIJIJINI NA MIKOA YA PWANI, KUSINI NA KUSINI MAGHARIBI, MIKOA YA KATI NA ZANZIBAR HAKUNA ANAEMJUWA SLAA ILA HUKO MBULU, UCHAGANI NA BAADHI YA MIKOA YA MAGHARIBI LABDA NDIPO ANAPOWEZA KUAMBULIA KURA CHACHE! TAKWIMU NILIZIWEKA HAPA LAKINI ZIMEFUTWA NA LA KUSHANGAZA NI KUWA FORUM HII INATAKA MAWAZO YA KUMSIFIA SLAA NA CHADEMA NA HUU NI UWOGA! KWANI WANAOAMUA NANI ATAKUWA RAIS SIO JAMII FORUM BALI NI WA TZ! NA WA TZ WENGI WANATEGEMEWA KUMPA KURA ZAO KIKWETE!

SASA KAMA NYINYI HAMTAKI KIKWETE AU LIPUMBA AWE RAIS HAKUNA ANAEWALAZIMISHA LAKINI SIO MULAZIMISHE WATU WOTE WAMPENDE DR.SLAA NA CHADEMA!

MUNASIKIAEEE!!
Chadema hatuna mtu anayeitwa hivyo!!
 
Lisemwalo kumbe lipo, hata Mbowe anajua tayari tafit za hawa jamaa zinasema nini:

"Mbowe alitoa kauli hiyo jana katika Viwanja vya Isanja...........Alisema tayari chama hicho kina matokeo kamili yaliyofanyiwa kazi na taasisi hiyo hivi karibuni, ambayo yanaonyesha Dk. Slaa, anaongoza kwa asilimia 44, huku mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete akifuatia kwa asilimia 41.....

Mbowe USIBWETEKE!
 
Wewe mjamaa yaani umeingia tu na kutuletea ujumbe kama huu, nadhani hii ni post yako ya kwanza - je kabla ya hapo ulikuwa wapi? Au umetumwa kuja kutafuta taarifa? Ulivyopata hii habari ilikuwaje ukimbilie hapa ili hali ulikuwa hupajui?

Naomba nitoe mashaka niliyonayo.
Mkuu hata mie nina mashaka na hii ishu maana inaweza ikawa imeletwa kutupumbaza na kuanza kusheherekea ushindi ambao umepangwa kuibiwa.
Dawa ni kuwaelimisha wabongo zaidi na zaidi watambue kuwa maamuzi wanayo wao na wafanya maamuzi sahihi ya kupiga kura na kumchagua Dr. Slaa hapo oktoba.

Ila pia kwa upande wa pili takwimu kama hizi ni vyema kuwa published kwani majambazi wakiona wanapata kihoro na kisebusebu pia wananchi wanaondoka uoga kwamba KUMBE INAWEZEKANA!!
 
Mwaka wa mavuno huu!
CCM kazi wanayo lazima wajiandae kuchakachua.
Vyama vya upinzani kuweni macho na idadi ya wapiga kura pamoja na vituo
 
Data ni nzuri zinaridhisha lakini,hayo majimbo ambayo wapinzani hawajaweka wagombea ni vichochoro tosha vya ccm kupata kura za ziada na ziada
 
Kwani haiwezekani? Mahali fulani mwaka fulani saa fulani kitu lazima kitokee. Usishangae kwa Watanzania kukataa KUDANGANYWA kuanzia sasa na sio kesho. Hata watoto hufika mahali wakamchoka baba yao! Changes is NOW! Msije mkashtuka sana na nawashauri msije mkaingia MSITUNI ikiwa mtashindwa. Inabidi CCM na vyama vingine wakubaliane na matokeo maana hayo yatakuwa maamuzi sahihi ya Watanzania.
 
Ni kweli kabisa nakubaliana na wewe. Lakini naomba nikuulize swali dogo, REDET na Synovate kwanini hawajatoa matokeo ya tafiti zao? Hivi kweli unaweza kuamini kwamba Synovate walifanya utafiti unaogusa coverage ya kampeni za wagombea kwenye vyombo vya habari tu? I think hako kakipengele kalitakiwa kuwa sehemu ya major report kuhusu perception ya watu kuhusu wagombea na pia iwapo uchaguzi ungefanyika wangempa nani kura na kwanini. Kitendo cha Synovate kutuletea utumbo wa utafiti ule unaashiria something is wrong some where na ndio maana hujasikia REDET wala Synovate.

Mwaka 2005, mpaka mwezi mmoja kabla ya uchaguzi walishatoa set mbili za polls na zote CCM ilikuwa inaongoza. Utafiti wao ulianza hata kabla ya nominations, na kama unakumbuka Prof. Mwandosya ali-discredit hizo polls za REDET. Mzee Kingunge baada ya Kikwete kuwa nominated na Mkutano Mkuu wa CCM, akasema kwamba wasomi wa REDET walishatoa matokeo hata kabla ya nominations na ndio uzuri wa kuwa na tafiti ambazo ni credible.

Sasa mwaka huu kigugumizi kinatoka wapi? Hao Synovate wanakuja na report ya kitoto mpaka unaanza kujiuliza hivi hawa walichokuwa wanafanya ina maana watanzania hatujui? Au hatusomi magazeti, au hatuangalii TV au hatusikilizi radio? Maana huo utafiti hauhitaji hata kupoteza resources au kuita waandishi wa habari eti unaenda kuwapa report kuhusu utafiti ambao uko wazi mbele ya kila mtu. Tuambie kilicho jificha ndani ya wapiga kura ili tuone ni kitu gani ambacho wapiga kura wanaangalia, wangapi wameishafanya maamuzi ya kura zao na wangapi ambao hawajafanya maamuzi.


Mkuu umesema ukweli! Synovate walikuwa na taarifa ila inaelekea walitishiwa na CCM wasitooe sehemu hiyo.

Refer gazeti la leo la mwananchi. Tanzania News - Tanzania Business News, Tanzania Sports News, Tanzania Newspaper, News Tanzania!
 
Ndugu zangu hali ni tete kama CCM imefikia hatua kuwalipa wapiga kura wahudhurie mikutano yao kwa kusombwa kwenye boat, malori na mabus mjue karibu mtu mzima anaumbuka watu tumechoka na siasa za kusadikika.
 
CCM hayo ni maji ya PUA sio ya shingo! JK hata ukimtumia na Mtabiri wako Shekh Yaya bado ngoma mbichi, kubali tu matokeo. Tunajua mnajipanga kwa mchezo mchafu wa wizi wa kura ndio mlichobakiza ila kumbukweni 2010 wananchi HAWADANGANYIKI.

CCM watabaki kuhonga tshirt,skafu,kofia, vitenge na khanga pamoja na kukodishia watu usafiri wa kuwabeba kwenye mikutano yenu na hizo 5000/ mnazogawa lakini fainal ni 31-10-2010 mtagalagazwa vibaya, na ninahisi harufu ya kuridia uchaguzi mwaka huu maana CCM hawata amini kama wamepigwa chini pamoja na juhudi zenu zote za kutumia mabilioni ya pesa kwenye uchaguzi huu.

My take: Mkigawa hela sie tunakula tuuuuuuuuuuuu hakuna kususa ila kura ni kwa Dr. Slaa tu
 
Kama ni kweli hizo data then mambo sasa yanakwenda vizuri. Ila sijapenda huyu jamaa kupewa hiyo taarifa sasa hivi, ingekuwa safi sana kama angeipata hiyo taarifa baada ya NEC kumaliza kuhesabu kura huku wakisimamiwa na Umoja wa Mataifa. Hawa jamaa wanapopewa habari za mshtukizo kama hizi hawakawii kupanga mchezo mchafu wa kuiba kura au kuufanyia fitina uchaguzi. Nafikiri ni wakati muafaka kwa vyama vya upinzani kufikiria namna ya kulidhibiti hili katika level za juu kwani kama waliweza kuibiana wao kwa wao, fikiri wakiunganisha nguvu za kiwizi na kuamua kuibia wapinzani.

Ila kama angepewa hiyo taarifa mara baada ya filimbi kulia kuwa si Rais wa miaka mitano ijayo, sijui angeongeza mshahara tena kwa wafanyakazi au angelia au angezirai. Sitamani kutafakari Makamba na wapambe wa JK wangesemaje....!!
 
hizi habari mi nilizisikia baa, mlevi akiropoka kama hana akili nzuri kisha kufuatia dharau yangu; "ah huyu jamaa hamna lolote- drunken master tu."
 
Naamini CHADEMA wana kamkakati ka kulinda kura zetu...!!!

Maana nimekutanan na picha ya Mnyika ina maneno "TAFUTA KURA, PIGA KURA, na LINDA KURA" Kwa maneno haya nina uhakika changamoto ya kuhujumiwa itakuwa imechukuliwa maanani!!!
 
He was lucky alisema "Is It" instead of Aiseee maana kingefuata kilichotokea Jangwani
 
Mwenye kuamini hizo statistics kwa kweli hana tofauti na aliyeamini kwamba CCJ ni chama tishio... Hivi Watanzania tutaacha lini kuamini mazingaombwe?

Kama wewe unamwamini anayeanguka mara kwa mara, ahadi zake ni hewa. Watz kwanini wasiamini kinachoelezea ukweli wa hali halisi.
 
This is gud news definitely...

Change is finally here...Lets hope for nothing but the best!

Nothing is impossible under the sun!
 
huu ni uongo ulio karibu na ukweli.... Katika nchi zinazoendelea zenye teknolojia duni, Utafiti si jambo la haraka kama ilivyo kwa mataifa yaliyoendela. Utafiti si taarifa za kuandika kwenye vyombo vya habari kama vile uchambuzi na tathmini ya hali ya uchaguzi.

Ni juha tu anayeweza kuamini kuwa utafiti wa wiki tatu zilizopita unaweza kuwa wa kweli. kwanza utafiti huo ulikuwa karibu sana na tarehe ambayo Slaa alitangazwa rasmi kugombea urais lakini pia kwa nchi maskini kama tanzania utafiti wake ni wa mtu kwa mtu kwa sababu ya teknolojia duni. kutokana na mazingira haya, ni vigumu kuamini utafiti huo kuchukua muda mfupi kiasi hicho.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom