Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

kwenye vita lazima u identify your common enemy, wakati wa vita kuu ya Pili baada ya Hitler kuanzisha mashambulizi dhidi ya SOVIET UNION,America ambayo walikuwa maadui na wasoviet walipeleka msaadakubwa wa silaha, logistic, na vyakula kuwa support wasoviet kwenye ile vita dhidi ya fashisti Hitler, na hakuna mmarekani aliyekasirikia uongozi kwa nini mnajiunga na hao wasoviet, ukitilia maanani walikuwa ni wapinzani wao wakubwa, waliwekatofauti zao pembeni wakamshinda adui yao waliposhinda wakarudi kwenye tofauti zao.

Na history ni mwalimu mzuri ila watu sijui ni upeo, au chuki zinawafanya hadi wanashindwa kuona mantiki, au kuku bali kutawaliwa na hisia, ila tunaojitambua kuwa Adui yetu ni CCM tuko pamoja hadi tummalize. Ni wakati mzuri kwa wasiokubaliana na kulubali kutawaliwa na mihemko wa aidha kurudi CCM au kwenda cha chochote mwingine hata ACT, au kutopiga kura waone kama hiyo ndiyo njia ya kuleta mabadiliko
 
Mwanasiasa kuhama chama si ajabu.Na katika siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.Kama ANC ya Mandela iliweka maridhiano na makaburi sitashangaa CDM wakiafikiana na Lowasa.Nionyeshwe kwanza umalaika wa hao wanaomuhujumu ENL nami nitamkataa.
 
usiogope maneno ya watu..this was a very strategic move..
Umejiuliza haya..
  1. ataondoka na watu wangapi CCM?
  2. nguvu ya ushawishi wake katika jamii??
CHA MSINGI CCM IPARANYIKE....(by any means possible)..kumbuka hata wao wameshaapa watabaki madarakani hata kwa ''goli la mkono''..
nafahamu huipendi ccm lakini unaona aibu kwa baadhi ya njia za kuitoa ccm...
My friend hata Nchi Kubwa kama Marekani wakati mwingine hushirikiana na aliyepata kuwa adui ili wamwangamize common enemy...''sometimes friendship among foes has to be forged inorder to attain common interest''....

Tatizo la kuwa muadilifu...Ngoja nisubiri muda dawa....Kwani hata Sauli alibadilika na kuwa Paulo.
 
NANI KWENU MWENYE KONDOO MIA AKIPOTEA MMOJA ASIYEMAFTA!!????? lowasa umesamehewa dhambi zako ustende tena dhambi na uwatajee wenzakoo
 
Lowassa akihudhuria kikao Kamati kuu CHADEMA

View attachment 271482
Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa, akisalimiana na viongozi na wanachama wa CHADEMA

View attachment 271483
Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa akiwa Meza Kuu na viogozi wa CHADEMA

Nenda utuachie Chama chetu! Mafisadi mliobaki ccm mlango uko wazi, mwenzenu kanyolewa kama mnavizia ubunge jiandaeni KUKATWA.
 
Tarime one naona kazi mnayo, mwambie alie edit hizo picture si professinal,na arudishe pesa za watu,kwanza hajatoa hivyo viatu nyuma ya lowasa, pia nyuma ya babu slaa angetoa kichwa cha huyo jamaa, huu uzi ni upuuzi mtupu na inaonyesha ukawa hawana mtu wa kumsimamisha:iamwithstupid:

Acha kujitoa ufahamu unatoa maelezo kwa picha moja!? Hebu toa maelezo na picha ya pili Lowassa akiwa meza kuu na viongozi wa CHADEMA, unadhani aliye-edit hiyo picha ya pili angetoa nini kichwa au miguu?
 
Uko sahihi mkuu, binafsi siwezi kumpigia kura Lowassa hata malaika walijua hili ..urais umeuzwa? umegeuzwa biashara? raisi ananunua urais wazi wazi bila kificho? it's a very big shame on the planet
heri ya mtu anayejulikana wazi kuwa ni fisadi maana watu watajiandaa kukabiliana na wizi wake kuliko yule anayekuja kwa kuonekana kondoo kumbe ni mbwa mwitu, huyu ni mbaya zaidi, kwani tulipowachagua Mwinyi, Mkapa na Kikwete kuna aliyetegemea kungetokea matukio ya kuuzwa tausi wetu pale Ikulu, Ikulu ingegeuka kuwa pango la biashara (Nyerere rip), Waarabu wangeuziwa mbuga ngorongoro, kodi isingekusanywa sawasawa, nyumba zetu za serikali zingeuzwa, maadili na miko ya viongozi vingefutwa, epa, richmond, meremeta, tembo wangeuwawa, magogo yangeuzwa ovyo, escrow je? viwanda vyetu je vipo?, mashamba waliyopewa wawekezaji yanalimwa? kilimo na mifungo je? madini nayo yako salama? baharini huko samaki wanalingizia nini taifa, elimu na afya kumesalimika?, vijisenti havipo?. Hatutaki kuaminishwa hapa kuwa Lowassa ni fisadi hivyo hafai mtu anayesema hivyo anatafuta uungwaji mkono kwenye kutibu njaa yake sio wananchi. Kama ni rushwa chimbuko lake ni ndani ya ccm kwa kutumia sera yao ya takrima wakati wa chaguzi zao, akinya kuku kanya lakini akinya bata anaambiwa kaharisha. Mchawi mpe mwana alee, safari hii tujaribu "fisadi" tuone litafunyanye kwa miaka 5.
 
Lowasa, hapatakuwepo m2 yeyote atakayecmama mbele yako cku zote za maisha yako kama Mungu alivyokuwa pa1 na Musa ndivyo atakavyo kuwa pa1 na wewe ila uwe hodari na moyo wa ushujaa hilo 2!
 
Marhaba mdogo wangu. Kuna watu wanadhani kuwa mimi natengeneza hizi story kumbe ninazipata kutoka kwenye reliable source

Nimekukubali na nimekuheshimu sana mkuu ukipata zingine usisite tunaomba tuletee teh teh teh siasa hizi!
 
Nimefurahi sana kuziona post kama hizi.

Hii inaonyesha kuwa maccm mnajua kuwa mwisho wenu umefika.

Hii inaashiria kuwa kila baya/ovu lililofanywa na ccm linakwenda kuwekwa wazi.

Hili ndilo jambo lililotabiriwa na JK Nyerere kuwa ccm itaangushwa na wanaccm wenyewe.

NB:
Bunduki ikitumiwa na jambazi ni hatari/haramu ila bunduki hiyo hiyo ikitumiwa na Askari inakuwa ni chombo cha kiusaklama.

Huku ndio kukua kwa siasa, na tutayaona mengi mpaka October 25.

Hujanielewa ndugu. Ni kuwa kama kiongozi aliyebadili katiba na kuwa madarakani ki dicteta kapokea bil 10, je mkimpatia nchi itakuwaje? Mi napenda upinzani sana. Na tatizo siyo CCM, tatizo ni mfumo tulionao mbovu, kuanzia vyama vya siasa. Wewe cheki ni chama gani kina demokrasia zaidi ya CCM? CCM anagalu walionesha ukomavu Kwa kumuengua mla rushwa Edo. CDM walionesha ukomavu walipo muondoa Zitto. Leo CDM wanaturudisha huko huko tulikotoka. Kwanini Lowassa anataka kwenda ikulu? Kuna nini? Mwl alisema ukimuona mtu anatoa hela kwenda ikulu muogope sana kama ukoma. Leo hii nyie wa CDM mnarukwa na akili. Wewe kama Lowassa ni ndugu yako OK, ila mimi naongelea mstakabali wa taifa kama taifa. Lowasaa, Chenge na wengine walitakiwa wapigwe risasi wafe kabisa tusiwaone. Tunahitaji watu wenye maadili. Nchi haiwezi kuongozwa na watu wanaotaka kupiga dili. Watu wanaotaka kupeana rasilimali za nchi. Nauamini usala wa taifa langu kupitia Mwamunyage mpaka sasa wanajua rais ni yupi, nyie pigeni tu kelele. Lowasssa kosa lake kubwa ni kuandaa makundi, alitaka kumuangusha swahiba Wake JK kipindi kile. Mimi ninaushahidi kabisa, alikuwa anapita anawaandaa wakuu wa mikoa, wilaya na wa nec ili wampigie rais kura ya kumuondolea uenyekiti, ila mzee akazinyaka nyepesi, na kibaya zaidi akawa anapiga dili kumzunguka JK. Lingine alishawahi kumzunguka hata mzee malecela, alilamba hela toka Japan za kuiuzia serikali magari. Lowassa ni mwizi. Mi sikatai kama Lipumba au Dr. Slaa angesimama Kwa urais. Na tena UKAWA kama wana akili wangemsimamisha Lipumba kwani ndiye Kwa sasa angeweza kuchukua makundi yote. Dr. Slaa ni mzinzi.
 
CHADEMA ghafla kimetekwa nyara na wahamiaji ambao wengine hata ukiwauliza kirefu cha CHADEMA ni nini hawajui.Hivi ni sahihi kisiasa kukabidhi chama kwa wahamiaji? Naomba kesho na keshokutwa CHADEMA msije lalamika kuwa CCM imehusika kuua CHADEMA au kuua UKAWA chonde chone mwenye masikio asikie wakiwemo wafadhili wenu wasije piga yowe kuwa hela zao zimezama bure kufanya kampeni hewa.Hasa wale matajiri wa Arusha na MOSHI.

Mimi nadhani ni suala la uelewa wa la halihitaji mihemko hapa, maana kwa mihemko hata mantiki haitoweza kupatikana.

Kwanza Huyu Lowassa ukimpa cheo cha uwakala au anatumiwa na CCM haileti maana kila mwenye akili timamu unajua jinsi alivyotofautiana na wana CCM wenzake Katika zoezi la uteuzi,ana mapenzi gani na hao waliomdhalilisha hadi awafanyie kazi ya kuiangamiza CDM?

Lowassa ndani ya CDM ana msaada mkubwa kuliko nje, tunamhitaji
 
Wale matomaso wa humu jf bisheni na hii
 

Attachments

  • 1438007553496.jpg
    1438007553496.jpg
    66.9 KB · Views: 543
Kama kweli CHADEMA kwisha kazi. Wamejipeleka kaburini huku wakiona na kutizama. Inatia huruma kwa Watanzania waliokuwa na matumaini kwa chama chao cha CHADEMA. Watakimbilia wapi??? Sitashangaa wakirudi kwa CCM ambao wameonyesha kuanza vita dhidi ya ufisadi kwa kumuengua Lowasa kwenye kugombea urais wa nchi.

Nakumbuka maneno ya Makongoro Nyerere kwamba, chama chetu mnakipeleka wapi kufanyanacho nn cc mnatuacha wapi tukiwa tunafanya nn, maana yake alichukizwa na watu wa jinsi hiyo, ss magamba yamejivua yenyewe ndani ya ccm na yameamua kukiteka chadema kwa hiyo naami ccm umetua huo mzigo mzito, na wao chadema wlitegemea kupiga bao kutokana na ccm kama ingefanya kosa kumchagua Lowasa, make wananazo documents za kutosha kuhusu ukwasi wa Lowasa, baada ya kupatikana Makifuri imekuwa hali mbaya sana kwao, kwa sasa chama kitakwenda vizuri sana, na kampeni za ccm ss zimekuwa nyepesi sana sana hadi Ikulu.
 
Back
Top Bottom