"Hatukujiunga na CHADEMA eti kwa sababu ulituahidi kazi, hapana tulijiunga na CHADEMA wakati mgumu kwa nchi yetu. Tulijiunga kwa kuwa tulitaka kuwa sehemu ya mapambano dhidi Rushwa, Ufisadi na Mafisadi.
Tuliingia CHADEMA kwa sababu tuliamini kile ambacho CHADEMA ilikisimamia na kukipigania, ndiyo maana tukawa sehemu ya mapambano.
Wewe Freeman Mbowe si sehemu ya Mapambo kwani umesharuhusu watu ambao tuliaminishwa kuwa ni mafisadi kuingia katika chama ambacho ndicho kilikuwa kimbilio la wananchi.
Wewe kaa na CHADEMA LOWASA yako Mimi nitabaki kuwa CHADEMA ASILIA.
Ni mimi mwana CHADEMA ASILIA