Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Hivi wewe kwa akili yako nusu kijiko, kati ya Lowassa na ccm nani kikwazo cha maendlleleo hapa nchini? Bora lowassa au ccm.

Lowassa as an individual sio hasara au hatari hata kama ni corrupt kuliko ccm as a system ambayo ni corrupt as whole.

Ccm ni hatari zaidi kuliko lowassa, kikwazo cha maendeleo nchi hii ni ccm sio Lowassa.

Mkuu upo sawa kabisa make toka 2008 lowasa hana meno lakini maujinga yameendelea kuwepo mara mia kabla hajajiuzulu, emu cheki escrow ni cha mtoto kwa richmond ona katiba nzuri tuliopendekeza wananchi yalivyoifanya haya maccm. Watz wanatakiwa waelewe kudumaa kwa tz tatizo ni ccm, na lowasa sasaiv ni adui wa ccm kwa iyo tusiangalie ufisadi wa lowasa bali tutumie hasira za huyu bwana mamvi kuwavuruga haya ccm, kwa nguvu na umaurufu alionao huyu bwana ni mtaji tosha kwa ukawa kutokemeza hili zimwi, heko ukawa mpokeeni bwana mamvi tuwavuruge maccm.
 
ukweli mchungu lowassa akisimama ukawa basi ccm tumepoteza kiti cha uraisi na wabunge wengi watakua ni ukawa tukubali tu huyu mamvi ni shiiidaa yani katika watu ambao wanaacha legacy kwenye siasa na nchi hii Lowassa yumo
 
Huu ni usaliti mkuu kuwahi kutokea katika siasa za Upinzani... Dk slaa ataficha wapi uso wake, leo hii yule Fisadi ndo amekuwa mtakatifu #itsbetter
 
Wanaruka na kukanyagana!!bilioni kumi imewatoka iman haa haa kumbe hata chadema kuna mfumo kama kwny magamba duh ACT yangu inogileeeeeee
 
ukiona maccm yanakataa jambo ujue hilo ndo linalotakiwa na Watanzania. Ukiyaona yanakubali jambo jua hilo kwa Watanzania ni kifo. Ukitaka kusimama kwenye haki basi simama kinyume na ma ccm.

Teh teh teh teh teh teh!
 
Jamani watu wote sasa hivi wamekuwa wakiongelea lowassa kusimamishwa ukawa kupitia chadema. Lakini siyo chadema wala ukawa wanaojiuliza je, wakishindwa urais 2015 hatma yao itakuwaje?

lengo sio urais tu, wakiongeza idadi ya wabunge na madiwani ni mafanikio makubwa hayo
 
Mi binafsi naona kama ukawa wamenunua silaha tena ya maangamizi kwenye vita hii ya kuiondoa ccm ikulu. Nawapongeza sana mmecheza pele
 
sote tumeshuhudia jinsi ukawa ilivyoanza na hadi ilipofika. ni wazi ilipofika haikustahili kumeguka na kurudisha nguvu kwa ccm. ni dua za ccm kuona kuwa ukawa inavunjika lakini haitokei hivyo. ccm tayari wameshampata mwakilishi wao katika kinyang'anyiro cha oktoba. ngoma ilibakia ukawa ambapo mafahali wawili; chadema na cuf walitunishiana misuli ya kuwania nafasi ya kuwakilisha ukawa kwenye uchaguzi ujao. cuf kwa upande wao walishapata mwakilishi kwa upande wa visiwani anbaye ni maalim seif. ni jambo lililo wazi kwamba kwa upande wa bara chadema kamwe isingekubali kuona cuf tena wanapata nafasi ya uwakilishi. chadema ina nguvu kubwa sana bara lakini pia inahitaji usaidizi kuongeza nguvu zilizopo. ilikuwa ni nafasi ya chadema kuweka mwakilishi wa ukawa kwa bara lakini kwa ubishi na hulka ya cuf ni wazi kwamba wasingependa kuona hilo kinatokea. cuf ilibidi wawapishe chadema. lakini pia haiwezekani kupuuza nguvu ya cuf huku bara maana wana wafuasi na ushawishi wa kutosha. hivyo ni busara tu ilibakia ili itumiwe na ukawa inusurike. kama cdm wangeweka ngumu na kuamua kujitoa ukawa ni wazi kuwa cuf na nccr wangechafua hali ya hewa, hivyo kufanya 'tukose wote'. na ni wazi kuwa upinnzani kwa mara nyingine tena ungekosa nafasi ya kushika dola na ndio ingekuwa nwanzo na mwisho wa upinzani wa kweli na wenye nguvu.

ni katika mazingira kama hayo ndipo palipohitajika mtu wa tatu mbali na lipumba na slaa. awali niliwahi kufikiri kuwa angesimamishwa mzee makaidi lakini nikaona kuwa hana ushawishi wa kutosha kwa wananchi. ndipo ninapoona ujio wa lowassa ambaye alizungumzwa sana kujiunga na chadema na hatimaye ukawa. lowassa pamoja na mapungufu yake anaonekana kuunuauru upinzani kwa kuxhukua nafasi iliyokuwa ikiwaniwa na mafahali wawili.

katika hili pongezi ziende kwa chadema na dk slaa kwa maamuzi haya magumu japo hayatabiriki bado. kuna kazi mbele ya kunsafisha lowassa ambaye ana sifa kuu ya ufisadi. tuaiwabeze sana chadema kwani ukweli ni kuwa wasingefanya hayo dola ingerudi ccm tu kwani lazima upunzani ungetifuana na ingwkuwa heri kwa ccm.

kadhalika pamoja na tambo za zitto ni ukweli kuwa wanasubiri tu vumbi litulie ndipo na wao wajiunge na ukawa. kauli ya zitto kuwa ni lazima wajue maslahi yao kama watataka kujiunga na ukawa ni wazi kuwa mafasi yao ipo ukawa. katika siasa hakuna adui wa kudumu
 
ccm imekufa imeoza ni mfu mpaka muda huu.
Sasa mkae msubirie mafuriko ya viongozi wa ccm watakavyomiminika CHADEMA.
 
alisema, wanaomchukia waanze kujiondoa wao ccm, yeye atakuwa wa mwisho ....sasa mbona amekuwa wa kwanza.....
 
Hakika hii ni wiki muhimu sana kwa mstakabali wa maendeleo ya watanzania kwa siku zijazo kwa watanzania wanahitaji mabadiliko na wameyakosa ndani ya ccm hivyo wanayatafuta nje ya ccm na hivyo kila mwenye nia njema na nchi hii ajiunge na wanaukombozi oktoba mwaka huu kupata mabadiliko ya kuipeleka nchi yetu katika maendeleo na kuondoa umaskini miongoni mwa watanzania.
 
Jamaa anatumika vilivyo na MAGWANDA tena anatumika kisayansi zaidi hadi picha za kutengeneza. Nawasihi tu CHADEMA ruzuku ya serikali isipite mbali kwa TARIME ONE.
 
Back
Top Bottom