Kikao cha CCM: RA Atema Cheche "Nitajiuzulu...."

Kwa mazingira yaliyopo ndani ya CCM hivi sasa, kweli mtu ambaye ana nia ya dhati ya kuleta mabadiliko anaweza kwenda kugombea kupitia CCM?

Mama Simba tayari ameishasema ndani ya CCM hakuna aliye msafi, kwa hiyo hata yeye mwenyewe ni mchafu na JK nae ni mchafu. Kauli hiyo ina maana kubwa sana kwa wale wenye nia ya kuingia kwenye siasa.

Mabadiliko ya kweli hayataletwa na hii CCM ya JK, EL na RA. Basically naweza kusema ni CCM ya RA na EL. JK ni boya tu amewekwa pale kama Mwenyekiti, lakini wenye final say ni akina EL na RA. Ndiyo maana hakuna lolote la maana linalofanyika, mikutano yao imekuwa ni kumbi za mipasho utadhani watu wako rusha roho pale Lango la Jiji.
.

Keil umenena, niko nyuma yako kwa asilimia 100% but only if Watanzania wa vijijini nao watafunguliwa macho na masikio yao, kwanza kwa kuelimishwa kuwa CCM haina hati miliki ya kuitawala nchi hii na mwenye uamuzi wa mwisho ni mwananchi mwenyewe. Watu waone madudu ya CCM na Kusikia huyo mbadala anakuja na ahadi gani.

Kama mpenda demokrasia ya dhati, bado nasikitishwa na upinzani uliopo, ndio maana nasema, kama upinzani wenyewe ni huu, basi CCM itatawala milele!.

Naungana na wewe pia kwenye hoja ya wale wenye fikra za mageuzi ya kweli, hatathubutu kugombea CCM kwani kwa hapa CCM ilipotufikisha, chama chochote kikija na sera nzuri za kueleweka, kampeni kubwa ya changing mind set za Watanzania kama ile ya Obama ya 'Change we can Belive in'.. 2 Wapinzani wote wakamkubali Dr. Slaa akasimama na Muungwana, 2010 CCM Chali!. Very unfortunately chama kama hicho bado hatuna.

Hivyo katika mazingira yaliyopo ya upinzani legelege, CCM bado ni Chama dola. Hivyo kwa maeneo ambayo hayana chachu ya mageuzi, then the right forum ni kugombea kupitia CCM halafu wachange from within kwa kuitumia ile formular ya 'if you can't beat them, join them'.
 
RA, kuwa mwangalifu na kile unachokiomba. Yanaweza kuja mengi zaidi ya Kagoda na Richmond......then what? Watanzania hawaitaji tu ujiuzuru bali utumikie kifungo na kurudisha pesa zetu, kisha urudi Iran. That's all.
 
DAWA ya mpasuko wa wabunge ndani ya CCM inaonekana kuwa ngumu, kutokana na kamati ya wazee wa CCM kushuhudia uhasama wa wazi, huku wakiendelea ‘kupashana’ kwa lugha kali.

Kamati hiyo inayoongozwa na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi imemaliza kazi yake, lakini wadadisi wa mambo ndani ya chama hicho wamekiri kuwa chuki na uhasama huenda visimalizike.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zilisema Katibu wa Itikadi na Uenezi, John Chiligati, alisema chanzo cha mpasuko ni wanamtandao ambao wamepasuka katikati hivyo kuwepo kundi la Edward Lowassa na Samuel Sitta.

Inadaiwa alisema watu hao ndio wamesababisha mpasuko mkubwa hivyo akashauri kamati hiyo ya wazee wa CCM, iwaite Lowassa, Sitta na watu wao wa karibu, Rostam Aziz na Katibu Mkuu, Yussuf Makamba.

Mpasha habari huyo alidai kuwa iwapo kamati hiyo itakaa nao ili kupata ufumbuzi wa kudumu, pia mmoja wa wajumbe, Abdulrahaman Kinana, asaidie kwa karibu. Ilielezwa kuwa Chiligati anaamini kuwa Kinana anaweza kusaidia kuondoa mpasuko huko kutokana na kuyajua makundi hayo vizuri.

Lakini wapasha habari hao walidai kuwa mbunge wa Nzega, Lucas Selelii alisema chanzo cha mpasuko huo ni Bunge kukubali kuunda kwa tume ya kuchunguza kampuni ya kufua umeme ya Richmond. Alisema wabunge tangu wakati huo waligawanyika wakiwamo waliounga mkono kuundwa kwa kamati na wengine wakawa wanapinga na akatoa mfano wa hoja ya mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga.

Mbunge huyo pia alisema kutokana na mgawanyiko huo ndiyo maana kamati ilipata wakati mgumu wa kutimiza majukumu yake ikiwamo kunyimwa baadhi ya nyaraka na watendaji wa Serikali kwa kile anachoamini kuwa yalikuwa maagizo kutoka kundi la Lowassa.

Inadaiwa alimtetea Spika Sitta kuwa hakuwa na hila kuunda kamati hiyo na akaeleza kuwa hata baada ya kamati kukamilisha kazi yake ilipeleka kwa Rais ripoti hiyo kabla ya mwezi mmoja kuwasilishwa bungeni. Alisema hata vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa vinajua kinachofanyika na kamati hiyo, hivyo akasema hakukuwa na mipango ya kuwaonea baadhi ya watu kama ambavyo baadhi ya wabunge wanataka jamii iamini.

Mbunge wa Kishapu, Freddy Mpendazoe, inadaiwa kwamba alishangaa kuwapo viongozi ndani ya CCM ambao wanapinga wabunge wanaopigia kelele ufisadi na akasema kama kufanya hivyo kwa mbunge wa CCM ni dhambi, basi chama hicho kibadilishe Katiba inayotamka kuwa rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala sitapokea rushwa. Mbunge huyo pia alishangaa viongozi wa CCM ambao wanamshambulia Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Reginald Mengi kuwa si wanachama wa CCM wakati wanakwenda kumwomba fedha za uchaguzi.

Wakati Mpendazoe anatoa shutuma hizo, Makamba alisimama na kutaka thibitisho wa madai hayo ndipo mbunge huyo inadaiwa akasema anazo taarifa zote. Lakini Mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombale-Mwiru aliomba mwongozo wa Mwenyekiti na kuhoji sababu ya mbunge huyo kumtukuza Mengi kwenye kikao hicho, wakati si mbunge ndipo Mpendazoe akajibu kuwa anafanya hivyo kwa vile kuna viongozi wa chama hicho walipinga wabunge wanaochangiwa fedha za Vicoba na Mwenyekiti huyo wa IPP.

Naye Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba alisema chanzo cha mpasuko wa wabunge ni madaraka na lengo ni kuwaondoa baadhi ya watu kama Lowassa kwenye ulingo wa siasa.

Naye Rostam Azizi alisema ni jambo la aibu wabunge wa CCM kuitwa mbele ya kamati ya wazee wa CCM na jambo hilo akasema halifai kujivunia kwani linaonesha namna chama hicho kilivyogawanyika. Alisema tuhuma juu ya kampuni ya Kagoda inayodaiwa kuwa ni yake hazina ukweli wowote na wanaofanya hivyo wanamsulubu bure kwani si ajenda ya CCM bali ni ya Chadema, akashangaa iweje wabunge wa CCM washikie bango jambo ambalo si ajenda yao. Alisema kwamba yeye anaamini kuwa kumsulubu yeye au Lowassa juu ya suala la Richmond ni kukikusulubu chama.

Rostam pia anadai kusema kwamba mpasuko kati ya wabunge na wabunge wa chama hicho ni uchaguzi wa mwaka 2005 baada ya watu kushindwa kupata urais ndipo wakaanzisha vita na kundi la watu ambao waliingia madarakani.

Mpasha habari alisema Rostam alisema kwa masikio yake aliwahi kuwasikia baadhi ya wabunge wakiapa kuwa wataiaibisha Serikali ya sasa wakati wakinywa chai kwenye mgahawa wa Bunge. Kada huyo wa CCM anadai pia kueleza kuwa kutokana na hali hiyo Sitta akawa adui mkubwa wa Lowassa na yeye mara kadhaa alijaribu kuwapatanisha, lakini ilishindikana
hivyo Sitta na wabunge wake wakawa na kasi ya kumfanyia hujuma Lowassa likiwamo suala la Richmond.

Kuhusu ripoti ya Richmond, Rostam alisema tangu mwanzo kulikuwa na hila mbaya ndio maana yeye alinyimwa fursa ya kutoa maoni yake mbele ya kamati hiyo.

Lakini Rostam pia alienda mbali na kutaka chama kuanzia sasa kiwachukulie hatua kali wabunge wanaoikosoa Serikali. Kuhusu kuumizwa kwake kisiasa alisema licha ya kuwa ameumizwa sana kuhusu jambo hilo yeye tayari ameshasamehe, kwani Mungu amemjaalia moyo wa kusamehe.
 
Habari nilizozipata toka ndani ya Kikao cha Tume ya Mapatano na Maridhiano ya CCM na wabunge wake kilichomalizika jana hapa mjini Dodoma, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ametema cheche na kukubali kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya Chama iwapo itaundwa tume huru kuthibitisha yale ya tume ya Mwakiembe.

Miongoni mwa Cheche alizotema, ni pamoja na kumlipua Spika Sitta kana kwamba ni kumkomelea msumari wa mwisho kuthibitisha chuki binafsi za Spika Sitta dhidi ya Edward Lowassa.

RA amesema Kamati ya Mwakiembe ni siasa chafu, ni ubia kati ya Spika Sitta na Mwakiembe dhidi ya Lowassa na Rostam.

RA anadai Six aliomba kwa El kupewa nyumba yenye hadhi yake Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ofisi yenye hadhi, Urambo, EL alimtilia ngumu kuwa ni kinyume cha taratibu. Pia aliomba lami toka Urambo-Tabora na Motorcade lakini EL alimgomea, hivyo jamaa akawa na hasira na kutafuta upenyo wa kufanya visasi.

RA alishauri iundwe Public Inquery ikigundua kuhusika kwake, yeye atajiuzulu nyadhifa zake zote.

Hata hivyo, RA hakuzungumzia kabisa issue za Kagoda kama uthibitisho wa dhati kuwa hahusiki aslan.:mad::mad:

Mkuu wa idara,

Wakati sisi tunakazania kukabana makoo na kulipiza visasi, waungwana Maalim na A.K wameamua kukutana faragha na kupata gahawa kidogo! (tutazamie Azimio la Zenji Party II?) nadhani washajionea kuwa nchi hii haina mwelekeo tena mara leo E.L kesho R.A kesho kutwa lioness Sofia. Hivi nani ni nani? nani wakuleta order katika nchi hii kwa sasa? inasikitisha kwakweli..

Amani.
 
Mkuu wa idara,

Wakati sisi tunakazania kukabana makoo na kulipiza visasi, waungwana Maalim na A.K wameamua kukutana faragha na kupata gahawa kidogo! (tutazamie Azimio la Zenji Party II?) nadhani washajionea kuwa nchi hii haina mwelekeo tena mara leo E.L kesho R.A kesho kutwa lioness Sofia. Hivi nani ni nani? nani wakuleta order katika nchi hii kwa sasa? inasikitisha kwakweli..

Amani.
Bantugbro haya ya kuanza kupachikana majina ya Mkuu wa idara yanatokea wapi?.

Hili la kukutana Maalim na AK ni ishara nzuri sana kwa siasa za Zanzibar. CUF itangaze kumtambua AK kama rais wa ZNZ, Karume awateu wale wawakilishi wawili wa CUF barazani akiwemo Juma Duni kwa kipindi kifupi kilichobakia, utekelezaji wa muafaka uridhiwe, ZNZ mambo mswano, kazi sasa ni huku kwetu bara, 2010 moto!
 
kitu mhimu cha kujiuliza ni kwanini mambo haya yote yaibuke baada ya taarifa ya dr mwakyembe? in maana haya hawakuyaona kabla ya Februari 2008? hamuoni kwamba chimbuko la yote ni baada ya wakubwa kukamatwa pabaya na kwamba wanachokifanya ni kujaribu kuzinusuru nafsi za walioguswa na maazimio hayo 23 ya bunge?
 
Jamani bunge lilitoa muda ktk kujadlili wengine walilia wameonewa. Lakini kwakuwa mkulu yumo hili ngonjera halitaisha isipokuwa km tukimweka raisi mwingie 2010
 
Naye Rostam Azizi alisema ni jambo la aibu wabunge wa CCM kuitwa mbele ya kamati ya wazee wa CCM na jambo hilo akasema halifai kujivunia kwani linaonesha namna chama hicho kilivyogawanyika. Alisema tuhuma juu ya kampuni ya Kagoda inayodaiwa kuwa ni yake hazina ukweli wowote na wanaofanya hivyo wanamsulubu bure kwani si ajenda ya CCM bali ni ya Chadema, akashangaa iweje wabunge wa CCM washikie bango jambo ambalo si ajenda yao. Alisema kwamba yeye anaamini kuwa kumsulubu yeye au Lowassa juu ya suala la Richmond ni kukikusulubu chama.

Rostam pia anadai kusema kwamba mpasuko kati ya wabunge na wabunge wa chama hicho ni uchaguzi wa mwaka 2005 baada ya watu kushindwa kupata urais ndipo wakaanzisha vita na kundi la watu ambao waliingia madarakani.

Kuhusu ripoti ya Richmond, Rostam alisema tangu mwanzo kulikuwa na hila mbaya ndio maana yeye alinyimwa fursa ya kutoa maoni yake mbele ya kamati hiyo.

Lakini Rostam pia alienda mbali na kutaka chama kuanzia sasa kiwachukulie hatua kali wabunge wanaoikosoa Serikali. Kuhusu kuumizwa kwake kisiasa alisema licha ya kuwa ameumizwa sana kuhusu jambo hilo yeye tayari ameshasamehe, kwani Mungu amemjaalia moyo wa kusamehe.

mmmh! jamani haya maneno ya Rostam yanaonyesha kuwa jamaa ni mtu hatari sana, either ni mjinga sana au ame-capitalize ktk ujinga wa wabunge wetu. Haya maneno anatamka mbele ya Mwinyi na wabunge.
 
Mkuu Mkandara,

Hoja yako ndiyo niliipigia sana kelele zama zile za msuguano wa wana-Kyela mara baada ya mwana JF kutangaza nia ya kugombea.

Kwa mazingira yaliyopo ndani ya CCM hivi sasa, kweli mtu ambaye ana nia ya dhati ya kuleta mabadiliko anaweza kwenda kugombea kupitia CCM? How many times wabunge wa CCM wamefungwa midomo wasiseme maovu ya wenzao ama ya serikali? Tena wengine kwa kutishiwa maisha.

Hivi kweli tuhuma inamhusu Makamba, ama RA au EL, utaingia kwenye vile vikao vya wabunge wa CCM uombe ridhaa ya kuongelea hoja hiyo Bungeni na uruhusiwe? Nape Nnauye isingekuwa huruma ya Muungwana leo hii asingekuwa mwana UVCCM wala mwana CCM, kisa aligusa tuhuma za kigogo wa CCM. Chama kimejaa untouchables (miungu watu) ambao hutakiwi kuwasema wala kwenda kinyume nao vinginevyo unaweza kufungishwa virago.

Hao wanaoitwa wapiganaji wameibuka kuinusuru CCM baada ya kuona chama kinapoteza umaarufu mbele ya wananchi. Baada ya Dr. Slaa kumwaga radhi ya LIST OF SHAME na Zitto kupeleka hoja ya Buzwagi ndipo akina Mama Kilango wakaibuka. Mama Kilango akiwa Bungeni alisema hawezi kukubali akae kimya awaachie akina Slaa na Zitto wapate umaarufu kwa kuibua kashfa na hoja nzito nzito, kisa anaogopa kushughuliwa na Chama ama serikali. Je, leo hii hao wapiganaji wanaitwaje ndani ya CCM? Hata kama una ka-doa kidogo, unaweza kujikuta unatwishwa kashfa ya mwaka 1947 ili kukunyamazisha usiseme. Ukiwauliza walikuwa wapi hawakukushughulikia, hawana jibu la kukupa.

Sasa hivi kamati ya Mzee Mwinyi inatapatapa tu, hawajui watachukua kipi waache kipi. Mama Simba tayari ameishasema ndani ya CCM hakuna aliye msafi, kwa hiyo hata yeye mwenyewe ni mchafu na JK nae ni mchafu. Kauli hiyo ina maana kubwa sana kwa wale wenye nia ya kuingia kwenye siasa.

Nikimsikia kijana anasema anakwenda kugombea Ubunge kupitia CCM ninamuona ni opportunist tu kwa kuwa kama yeye ana nia safi na dhamira njema, hawezi kwenda kujichanganya na waliovunda ama kuoza kabisa. Hivi kweli kama mtu ni msafi anaweza kwenda kukaa jalalani ama kujichanganya na wachafu? Umeambiwa kabisa hili ni jalala, ni sehemu iliyojaa takataka, bado mtu anakwenda kukaa hapo hapo. Hapo lazima ujiulize sana kama kweli mtu huyo ana nia na dhamira ya kweli ya kuwatumikia wananchi.

Hivi, ili ushinde Ubunge ni lazima upitie CCM? This is the opportune time for young men and women who wish to vie for MP posts kuingia kazini kumwaga sera za kueleweka. Unajua huu uchafu ambao CCM wanapakana sasa hivi utakuja kuwasumbua sana kuusafisha ikifika 2010, labda kwa kuwa ni mafisadi watatumia hela za ufisadi ili washinde. Lakini kama kuna mtu yuko serious na mapambano ya kweli, watanzania wa sasa wanasomesheka vizuri tu na wanaelewa. Ujinga unaoendelea ndani ya CCM ni faida kwa upinzani na wale wanaotaka kuingia kwenye siasa kupitia upinzani.

Mabadiliko ya kweli hayataletwa na hii CCM ya JK, EL na RA. Basically naweza kusema ni CCM ya RA na EL. JK ni boya tu amewekwa pale kama Mwenyekiti, lakini wenye final say ni akina EL na RA. Ndiyo maana hakuna lolote la maana linalofanyika, mikutano yao imekuwa ni kumbi za mipasho utadhani watu wako rusha roho pale Lango la Jiji.

NB: Kumradhi mwana JF ambaye ulitangaza kugombea kupitia CCM. Niliahidi kwamba ukishinda Ubunge nitaendelea kukumbusha mabandiko yako ya hapa ndani, unless na wewe upotee kama akina Dr. James Msekela ambao kwenye TANZANET walionekana wafurukutwa na walipoingia kwenye system wamemezwa na wamekuwa mute kama hawapo.
.


Huyo samwel sita na john malecela wamekuwa madarakani kuanzia lini? wamefisadi kiasi gani?
na leo nini kilichowagusa na kujiita wapiganaji?hamuoni kwamba ni interest binafsi.

huyu mwakyembe,usafi wake nini?kama ni msafi basi ahamie chadema.hizo kelele zake kwenye vyombo vya habari vitatusaidia au ndiyo anaendelea kuwaangamiza wana kyela.Jaman achen utani,kyela iko chini sana.hakuna kitu kule.hakuna ata A'level moja.taabu.
 
Mtanzania,
Mkuu wangu kwanza pole sana.. ndio siasa za Bongo hizo kwani hakuna jimbo lolote unaloweza gombea kwa tiketi ya CCM ukawa salama - HAKUNA..hivyo sii tu kina Sitta na Mwakyembe isipokuwa ni tabia zenu nyote kama chama. Sitta na Mwkayembe wote wamepata upinzani toka vyama vya Upinzani hna sikuona mauaji au kitu kinachokaribia hivyo. Utanisamehe nitakuja strong kidogo kukupa changamoto!

Nina swala, hivi Katika kujisafisha wewe... Je, unaweza kusema wazi EL na RA ni Mafisadi?.. au usafi ni wa mwili wako na sii kauli..Hivi Unafiki wa mtu ni usafi au?.. sasa kama wewe unataka kujisafisha nakuomba ulaani vitendo vya kina Lowassa, Rostam na wengine wote kwani usafi wa mtu huanza kwa kufahamu matendo mabaya..Hivi ukiona mtu kaua inabidi usireport hadi wewe utakapo kisafisha na makosa ya uasherati au kuchukua posho mbili!
Tofauti kubwa ya WApiganaji na wengine wote ni kwamba hawa wanatoa report ktk vyombo vya sheria na hao kina RA wanazungumza haya pembeni kazi kuita waandishi wa habari wakidai wapiganai nao sii wasafi...

Mkuu wangu tatizo lako na hao kina Mwakyembe na Sitta mnagombea kipande cha mkate ambacho kila mmoja wenu ndio shibe yake. has no interest in political balance towards social harmony and common good, na ndicho nilichjokiona hapa JF.. Kifupi mkuu wangu utanisamehe lakini usafi ungeuanza hapa JF, kila nilichosoma ktk kuburuzana kwenu nimewasoma kama ni selfintrest zaidi..Kila mmoja wenu anarusha magumi pasipo kukubali kujitazama yeye. It's been wewe hivi wewe vile, mimihivi mimi vile, na hakuna mmoja wenu anayekubali kujitazama na kutambua mapungufu yake..


Mwakyembe na Sitta wanaweza kutokuwa wasafi, but they represent our problem na our needs Kitaifa, hivyo sifa zangu kwa Sitta na Mwakyembe ni ktk maswala yanayolihusu taifa zima.. Hayo ya Kyela nawaachia wana Kyela.

Na kusema kweli nimeshindwa sana kukupa support moja kwa moja kwa sababu Mpiganaji wa kweli hujiunga Upinzani kwa lugha yangu kuwa Conservative kifikra ili upate kuisafisha system ilinayowabeba Mafisadi..Haramu ni Ufisadi, na ndicho kinachotakiwa kupigwa vita.. Usafi wa mtu unaanza na nafsi,uwezo wa kutambua mabaya na ukayakemea.

Kama ndio ingekuwa hivyo tusingekuwa na Mapadre, Masheikh na kadhalika wakitoa mawaidha na kufundisha neno la Mungu..Miyume wenyewe hawakuwa perfect ama niseme wasafi..kwanza hakuna mtu msafi na ndio maana tumeunda sheria, magereza na vyombo vya usalama.. Hiyo ndio kazi yao.. Sitta au Mwakyembe aren't clean wapelekeni ktk vyombo vya sheria..Na kama haiwezekani then system nzima inafail, systema mbayo wewe unataka kujiunga nayo..

Kama unataka kugombea Ubunge kwa sababu huridhiki na hali halisi ya Utawala uliopo na unataka kuleta mabadiliko ktk utawala basi jiunge na Upinzani wa sio kuwaletea wananchi mfumo ule ule wanaoupiga vita..Kyela haikuanza kutawaliwa na Mwakyembe, mapungufu ya Kyela hayakuanza miaka mitano iliyopita isipokuwa ni mlolongo wa viongozi wa CCM waliwakilisha wananchi wa Kyela kushindwa kuwaletea mabadiliko..And I believe wee pia utakuwa katika hesabu ya viongoz hao kwani changes haziletwi na kichwa kimoja isipokuwa policies za chama kinachoongoza.

lakini kama unagombea kwa sababu ya Mwakyembe au malalamiko ya wana Kyela, hapo mkuu wangu usiyachukulie mawazo yangu kwa uzito hivyo kwani all what ai'm for Upinzani wa system nzima iliyopo na sii WATU. Wapiganaji wana represent Upinzani na sii Upinzani wa jina la mtu...
Mkandara, sisi wana JF tunagombea kipande cha mkate na nani ili tushibe?mbona tunapiga kelekele kila siku?

Hasikudanganye mtu kaka yangu.hakuna anayekuwakisha wewe pale.wewe mwenyewe umekiri kuwa ccm sio wasafi na leo hii hao hao unasema wanakuwakilisha wewe kitaifa?kwali hapa kuna kazi.samwel sitta amekuwa kwenye madaraka kuanzia lini?alishindwaje kukuwakilisha wewe tangu mwanzo?ameshituka nini?amuka ndugu yangu.

Hakuna taabu usipo support,lakini mtu anapimwa kwa matendo yake na si vinginavyo.wananchi wengi wameelewa na wameishaona kuwa wanadanganywa na ukomedy wa waheshimiwa.
 
Huyu ROSTAM AZIZ ndiye aliyeifikisha nchi hapa ilipo. Ni mgeni aliyekuja kutoka Uajemi ili kuwaangamiza watanzania baada ya kuwapora raslimali zao akishirikiana na watu wenye uroho wa utajiri wa kupindukia kama vile LOWASSA. Hawa wengine wanaom-support kama Sofia Simba, Makongoro Mahanga, Kingunge, n.k. wanaambulia makombo tu ya akina ROSTAM na LOWASSA.
Tunafahamu 'war chest' yao ni kubwa na ndio maana unaona watu kama akina Sofia Simba wanaropoka ovyo na kujishushia hadhi kwani wana uhakika wa malipo mazuri kwa kazi yao chafu.
Sasa sisi wana wa nchi hii tunasema hivi: Enough is enough! Tunaingia rasmi kwenye mapambano ya kutetea uhuru wetu na raslimali zetu. Kwa wale wapiganaji wa kweli maelekezo yatafuata... Stay tuned.
 
Bantugbro haya ya kuanza kupachikana majina ya Mkuu wa idara yanatokea wapi?.

Hili la kukutana Maalim na AK ni ishara nzuri sana kwa siasa za Zanzibar. CUF itangaze kumtambua AK kama rais wa ZNZ, Karume awateu wale wawakilishi wawili wa CUF barazani akiwemo Juma Duni kwa kipindi kifupi kilichobakia, utekelezaji wa muafaka uridhiwe, ZNZ mambo mswano, kazi sasa ni huku kwetu bara, 2010 moto!

Haya ndugu yangu Pasco umekataa ukuu wa idara basi wee!

Kwakweli tuwaache tu huko zenji waendelee na shughuli zao maana bara kazi ni nzito sana kipindi hiki. Soon tutaanza kutoana macho, ni kiasi cha mwendawazimu mmoja tu kulianzisha!. Juma Duni ni mwanasiasa mzuri sana chuki tu ndo zinatufanya tushindwe kumtumia kwa maendeleo yetu wote.

Amani
.
 
Huyu ROSTAM AZIZ ndiye aliyeifikisha nchi hapa ilipo. Ni mgeni aliyekuja kutoka Uajemi ili kuwaangamiza watanzania baada ya kuwapora raslimali zao akishirikiana na watu wenye uroho wa utajiri wa kupindukia kama vile LOWASSA. Hawa wengine wanaom-support kama Sofia Simba, Makongoro Mahanga, Kingunge, n.k. wanaambulia makombo tu ya akina ROSTAM na LOWASSA.
Tunafahamu 'war chest' yao ni kubwa na ndio maana unaona watu kama akina Sofia Simba wanaropoka ovyo na kujishushia hadhi kwani wana uhakika wa malipo mazuri kwa kazi yao chafu.
Sasa sisi wana wa nchi hii tunasema hivi: Enough is enough! Tunaingia rasmi kwenye mapambano ya kutetea uhuru wetu na raslimali zetu. Kwa wale wapiganaji wa kweli maelekezo yatafuata... Stay tuned.

na ni uumbavu wa viongozi na waasisi wa taifa hili kuyajua haya yote na kumuacha mpaka leo anafika hatua hii..we need to blame ourselves first
 
Habari nilizozipata toka ndani ya Kikao cha Tume ya Mapatano na Maridhiano ya CCM na wabunge wake kilichomalizika jana hapa mjini Dodoma, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ametema cheche na kukubali kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya Chama iwapo itaundwa tume huru kuthibitisha yale ya tume ya Mwakiembe.

Miongoni mwa Cheche alizotema, ni pamoja na kumlipua Spika Sitta kana kwamba ni kumkomelea msumari wa mwisho kuthibitisha chuki binafsi za Spika Sitta dhidi ya Edward Lowassa.

RA amesema Kamati ya Mwakiembe ni siasa chafu, ni ubia kati ya Spika Sitta na Mwakiembe dhidi ya Lowassa na Rostam.

RA anadai Six aliomba kwa El kupewa nyumba yenye hadhi yake Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ofisi yenye hadhi, Urambo, EL alimtilia ngumu kuwa ni kinyume cha taratibu. Pia aliomba lami toka Urambo-Tabora na Motorcade lakini EL alimgomea, hivyo jamaa akawa na hasira na kutafuta upenyo wa kufanya visasi.

RA alishauri iundwe Public Inquery ikigundua kuhusika kwake, yeye atajiuzulu nyadhifa zake zote.

Hata hivyo, RA hakuzungumzia kabisa issue za Kagoda kama uthibitisho wa dhati kuwa hahusiki aslan.:mad::mad:
Kwako wewe huo utumbo aliosema rostam ndio AMETEMA CHECHE!!! and you invite us to share that gabbage!you r so foolish!!!
 
this is so insane, Hizo tume zote zilizoundwa na kutoa report zimeishia wapi!! watanzania tunafanywa wajinga!!
 
Hizo pesa zote zinazotumika kuunda tume ambazo hata matokeo ya uchunguzi wao yakitolewa hayakubaliki/kufanyiwa kazi, si zingetumika kuboresha huduma ya jamii? Kwa mfano kuweka CT-scanners katika hospitali zote za mikoa? MRI scanners katika hospitali zote za rufaa? Na mambo madogo tu kama gloves, nyuzi nk?

Ni aibu mtu unapofanya kazi huku katika hospitali za nchi za nje, na kuona mambo ambayo kwa kweli serikali ya TZ ingekuwa na nia tu, na nyumbani yangewezekana.

Kweli tunahitaji "damu mpya"...

Hivi mashuleni watoto wanapofundishwa uraia (civics) huwa swala la "patriotism" linagusiwa? Maana hio ndio namna ya kuandaa damu mpya itakayogeuza mwelekeo wa Tanzania
 
.

Keil umenena, niko nyuma yako kwa asilimia 100% but only if Watanzania wa vijijini nao watafunguliwa macho na masikio yao, kwanza kwa kuelimishwa kuwa CCM haina hati miliki ya kuitawala nchi hii na mwenye uamuzi wa mwisho ni mwananchi mwenyewe. Watu waone madudu ya CCM na Kusikia huyo mbadala anakuja na ahadi gani.
hata hao wa mjini wenye uelewa mkubwa hawapigi kura na wakienda kupiga kura wanasema sasa mimi nimpigie nani "bora zimwi ulijualo"
 
Habari nilizozipata toka ndani ya Kikao cha Tume ya Mapatano na Maridhiano ya CCM na wabunge wake kilichomalizika jana hapa mjini Dodoma, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ametema cheche na kukubali kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya Chama iwapo itaundwa tume huru kuthibitisha yale ya tume ya Mwakiembe.

Miongoni mwa Cheche alizotema, ni pamoja na kumlipua Spika Sitta kana kwamba ni kumkomelea msumari wa mwisho kuthibitisha chuki binafsi za Spika Sitta dhidi ya Edward Lowassa.

RA amesema Kamati ya Mwakiembe ni siasa chafu, ni ubia kati ya Spika Sitta na Mwakiembe dhidi ya Lowassa na Rostam.

RA anadai Six aliomba kwa El kupewa nyumba yenye hadhi yake Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ofisi yenye hadhi, Urambo, EL alimtilia ngumu kuwa ni kinyume cha taratibu. Pia aliomba lami toka Urambo-Tabora na Motorcade lakini EL alimgomea, hivyo jamaa akawa na hasira na kutafuta upenyo wa kufanya visasi.

RA alishauri iundwe Public Inquery ikigundua kuhusika kwake, yeye atajiuzulu nyadhifa zake zote.

Hata hivyo, RA hakuzungumzia kabisa issue za Kagoda kama uthibitisho wa dhati kuwa hahusiki aslan.:mad::mad:
..halafu jifunze kuandika majina ya watu vizuri!! ulisoma wapi wewe darasa la kwanza??
 
Back
Top Bottom