Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,513
- 113,640
- Thread starter
- #141
.Kwa mazingira yaliyopo ndani ya CCM hivi sasa, kweli mtu ambaye ana nia ya dhati ya kuleta mabadiliko anaweza kwenda kugombea kupitia CCM?
Mama Simba tayari ameishasema ndani ya CCM hakuna aliye msafi, kwa hiyo hata yeye mwenyewe ni mchafu na JK nae ni mchafu. Kauli hiyo ina maana kubwa sana kwa wale wenye nia ya kuingia kwenye siasa.
Mabadiliko ya kweli hayataletwa na hii CCM ya JK, EL na RA. Basically naweza kusema ni CCM ya RA na EL. JK ni boya tu amewekwa pale kama Mwenyekiti, lakini wenye final say ni akina EL na RA. Ndiyo maana hakuna lolote la maana linalofanyika, mikutano yao imekuwa ni kumbi za mipasho utadhani watu wako rusha roho pale Lango la Jiji.
Keil umenena, niko nyuma yako kwa asilimia 100% but only if Watanzania wa vijijini nao watafunguliwa macho na masikio yao, kwanza kwa kuelimishwa kuwa CCM haina hati miliki ya kuitawala nchi hii na mwenye uamuzi wa mwisho ni mwananchi mwenyewe. Watu waone madudu ya CCM na Kusikia huyo mbadala anakuja na ahadi gani.
Kama mpenda demokrasia ya dhati, bado nasikitishwa na upinzani uliopo, ndio maana nasema, kama upinzani wenyewe ni huu, basi CCM itatawala milele!.
Naungana na wewe pia kwenye hoja ya wale wenye fikra za mageuzi ya kweli, hatathubutu kugombea CCM kwani kwa hapa CCM ilipotufikisha, chama chochote kikija na sera nzuri za kueleweka, kampeni kubwa ya changing mind set za Watanzania kama ile ya Obama ya 'Change we can Belive in'.. 2 Wapinzani wote wakamkubali Dr. Slaa akasimama na Muungwana, 2010 CCM Chali!. Very unfortunately chama kama hicho bado hatuna.
Hivyo katika mazingira yaliyopo ya upinzani legelege, CCM bado ni Chama dola. Hivyo kwa maeneo ambayo hayana chachu ya mageuzi, then the right forum ni kugombea kupitia CCM halafu wachange from within kwa kuitumia ile formular ya 'if you can't beat them, join them'.