Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,604
Habari nilizozipata toka ndani ya Kikao cha Tume ya Mapatano na Maridhiano ya CCM na wabunge wake kilichomalizika jana hapa mjini Dodoma, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, ametema cheche na kukubali kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya Chama iwapo itaundwa tume huru kuthibitisha yale ya tume ya Mwakiembe.
Miongoni mwa Cheche alizotema, ni pamoja na kumlipua Spika Sitta kana kwamba ni kumkomelea msumari wa mwisho kuthibitisha chuki binafsi za Spika Sitta dhidi ya Edward Lowassa.
RA amesema Kamati ya Mwakiembe ni siasa chafu, ni ubia kati ya Spika Sitta na Mwakiembe dhidi ya Lowassa na Rostam.
RA anadai Six aliomba kwa El kupewa nyumba yenye hadhi yake Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ofisi yenye hadhi, Urambo, EL alimtilia ngumu kuwa ni kinyume cha taratibu. Pia aliomba lami toka Urambo-Tabora na Motorcade lakini EL alimgomea, hivyo jamaa akawa na hasira na kutafuta upenyo wa kufanya visasi.
RA alishauri iundwe Public Inquery ikigundua kuhusika kwake, yeye atajiuzulu nyadhifa zake zote.
Hata hivyo, RA hakuzungumzia kabisa issue za Kagoda kama uthibitisho wa dhati kuwa hahusiki aslan.
Miongoni mwa Cheche alizotema, ni pamoja na kumlipua Spika Sitta kana kwamba ni kumkomelea msumari wa mwisho kuthibitisha chuki binafsi za Spika Sitta dhidi ya Edward Lowassa.
RA amesema Kamati ya Mwakiembe ni siasa chafu, ni ubia kati ya Spika Sitta na Mwakiembe dhidi ya Lowassa na Rostam.
RA anadai Six aliomba kwa El kupewa nyumba yenye hadhi yake Dar es Salaam na Dodoma pamoja na ofisi yenye hadhi, Urambo, EL alimtilia ngumu kuwa ni kinyume cha taratibu. Pia aliomba lami toka Urambo-Tabora na Motorcade lakini EL alimgomea, hivyo jamaa akawa na hasira na kutafuta upenyo wa kufanya visasi.
RA alishauri iundwe Public Inquery ikigundua kuhusika kwake, yeye atajiuzulu nyadhifa zake zote.
Hata hivyo, RA hakuzungumzia kabisa issue za Kagoda kama uthibitisho wa dhati kuwa hahusiki aslan.